Thursday, 31 December 2009

BLOGU HII INAWATAKIA NYOTE HERI NA BARAKA KWA MWAKA 2010.NAAMINI TUTAENDELEA KUSHIRIKIANA KWA MICHANGO YA MAWAZO NA KUKOSOA PALE INAPOBIDI,NAMI NAAHIDI KUWEKA MABANDIKO ZAIDI KATIKA MWAKA UJAO.

ASANTENI SANA

Tuesday, 29 December 2009


THE NATION

AND BEYOND

THE Publishers of

MwanaHALISI,

your enviable Kiswahili weekly

in Tanzania,

wish to convey to you, our

warmest Season Greetings

that bring with them

a New Year – 2010.

We have always done

our piece in Investigative

and Public Journalism;

we are now engaged in

marshalling more skills,

improving methods and

producing quality copy

for IMPACT.

We continue to rely

on your readership;

appreciation of our efforts

to produce a copy worthy

your money; attempt at becoming

a real people’s voice;

and your kind and material

support already rendered

and anticipated.

We pledge to do more

to your satisfaction.

Happy New Year!

Hali Halisi Publishers Limited, Tel/Fax 022 - 2760560

Kasaba Street, Plot 57/31A Kinondoni e-mail: halihalisi06@yahoo.com

P. O. Box 67311 Dar es Salaam, TANZANIA website:www.halihalisi.com.tz

Cel: 0784 440 073/0777 773347


Thursday, 24 December 2009


There will always be bad,or even worse,Santas.Look at THIS,for example.

ANYWAYS,WISHING YOU ALL MERRY CHRISTMAS.

Saturday, 19 December 2009


Ahadi za urais 2005 zamtesa Kikwete uchaguzi wa mwakani

Rais Jakaya Kikwet, mzigo mzito wa ahadi zake za mwaka 2005 unamkabili uchaguzi ujao 2010.
Na Mwandishi Wetu
MIEZI michache ikiwa imebaki kabla ya kuanza kwenda kwa wananchi kuomba ridhaa ya kuongoza nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano, Rais Jakaya Kikwete anaonekana kukabiliwa na mzigo mzito wa kutekeleza ahadi nyingi alizozitoa wakati wa kampeni za mwaka 2005.

Kikwete alipata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 baada ya kunyakua takriban asilimia 80 ya kura, akiwa pia ameshinda kwa kishindo dhidi ya wapinzani wake kwenye uteuzi wa mgombea wa CCM.

Lakini kadri muda unavyokwenda ndivyo umaarufu wake unaonekana kupungua huku tafiti mbalimbali zikionyesha kuwa umaarufu aliokuwa nao wakati akiingia madarakani unaendelea kuporomoka, ikiwa ni miezi tisa kabla ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Wakati akizunguka sehemu mbalimbali nchini kuomba kura za wananchi, Kikwete alikuwa akitoa ahadi kem kem ambazo alizielezea kwa kifupi kwenye kauli mbiu yake ya â€Å“Naisha Bora kwa Kila Mtanzania” ambayo mkakati wake wa kuitekeleza ulikuwa ni â€Å“ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya”.

Mbali na ahadi ambazo alikuwa akizitoa kwa wananchi kila sehemu alipoelezwa tatizo, ikiwa ni pamoja na matatizo sugu ya maji, miundombinu, huduma za afya na pembejeo, Rais Kikwete pia alitoa ahadi za ujumla kabla na baada ya kushinda uchaguzi kumrithi Benjamin Mkapa.

Baadhi ya ahadi hizo za Rais Kikwete kabla na baada ya kuingia madarakani ni pamoja na kuweka kipaumbele katika kilimo, akitumia kaulimbiu ya Kilimo Kwanza, kupitia upya mikataba ya madini ili inufaishe nchi na wawekezaji, na kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi wa elimu ya juu anayekosa masomo kwa kukosa karo.

Ahadi nyingine ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za umma, kuumaliza mgogoro wa Zanzibar, kuimarisha uhusiano wa kimataifa, kukomesha tatizo la ufisadi, kupambana na tatizo la uhalifu, ikiwa ni pamoja na biashara ya dawa za kulevya na ujambazi, kuandaa mdahalo wa kitaifa wa michezo kwa lengo la kuinua michezo na ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma....INAENDELEA HAPA

Thursday, 17 December 2009


Waziri wa Sheria adai Bunge la sasa halina ubavu kwa serikali
Na Leon Bahati
WAZIRI wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe amezidi kutoa kauli tata baada ya kuligeukia Bunge la Jamhuri ya Muungano, akisema halina nguvu ya kuilazimisha serikali kufanya mambo na kwamba kazi yake ni kuishauri.

Hiyo ni kauli ya pili ya waziri huyo katika kipindi kisichopungua wiki moja baada ya kukaririwa Jumatatu akisema kuwa Rais Jakaya Kikwete hana uwezo wa kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi kwa kuwa mfumo wa utawala wa sheria hauruhusu vitendo kama hivyo.

Kauli hizo mbili zinazohusu mamlaka ya kisheria zimetolewa katika kipindi ambacho mjadala mkubwa wa hatua zinazostahili kuchukuliwa dhidi ya watuhumiwa katika kashfa ya utoaji zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) ukiwa umemgeukia rais.

Pia Chikawe ametoa kauli hiyo wakati Bunge likiishinikiza serikali kutoa taarifa ya utekelezaji wa maazimio yake 23 dhidi ya wahusika kwenye kashfa hiyo kubwa iliyotikisa nchi baada ya Edward Lowassa kujiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu kutokana na ushauri uliotolewa na kamati teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza kashfa hiyo....INAENDELEA HAPA

Wednesday, 16 December 2009


Prof Shivji asema Rais Kikwete ana mamlaka kisheria kuwabana mafisadi
*WENGINE WAMTAKA WAZIRI CHIKAWE AACHE KUKURUPUKA
Na Sadick Mtulya

SIKU moja baada ya Waziri wa Sheria na Katiba Mathias Chikawe kusema Rais Jakaya Kikwete hawezi kutumia mamlaka yake kuwabana mafisadi, baadhi ya wanasheria nchini, akiwamo Profesa Issa Shivji, wamepinga kauli hiyo kwa kusema sio kweli.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana wanasheria hao walisema rais anaweza kuwabana mafisadi kwa kutumia mamlaka yake ndani ya chama na serikali.

Profesa Issa Shivji alisema Rais Kikwete anaweza kupambana na watuhumiwa wa ufisadi kwa kuwavua madaraka walionayo katika chama au serikali.

Gwiji hilo la Sheria na Mwenyekiti wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere, alisema kama watuhumiwa watakuwa watumishi wa serikali au watendaji katika mashirika ya umma, rais anaweza kuwawajibisha kwa kutumia sheria na kanuni za utumishi wa umma.

"Kumwajibisha mtuhumiwa sio iwe kumpeleka mahakamani, unaweza kuchukua hatua za awali ikiwemo kumvua nyadhifa zote. Kama ni mwanasiasa au mtumishi katika serikali na mashirika ya umma, unaweza kumwajibisha kwa mujibu wa sheria za umma," alisema Profesa Shivji.

Alisisitiza Kusema Rais Kikwete hana uwezo wa kuwabana mafisadi sio kweli na Watanzania wanatakiwa kuelewa hivyo kwamba rais anaweza.

Kauli ya Profesa Shivji iliungwa mkono na Profesa Abdallah Safari, aliyetia ngumu akisema sheria za nchi ikiwemo ya utawala, inampa uwezo na mamlaka rais kupambana na vitendo vya ufisadi ndani ya serikali yake na hata katika chama chake.

Rais kukasimu mamlaka yake kwa Takukuru (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ) na kwa DPP haimaanishi kwamba sasa yeye hana uwezo wa kupambana na watu wanaojihusisha na ufisadi. Bado anao, alisema Profesa Safari....INAENDELEA HAPA

Alifafanua kwamba, Rais Kikwete anayewajibika katika kupambana na ufisadi kwa kuwa yeye ndiye anayewajibika moja kwa moja kwa wananchi wa Tanzania.

Monday, 14 December 2009



Waziri Chikawe asema Kikwete hawezi kuwabana mafisadi
*Asema Rostam, Dk Hoseah hawakamatiki
*Asikitika DPP, DK Hoseah kuparuana

Na Leon Bahati

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe amesema Rais Jakaya Kikwete hana uwezo kutumia mamlaka yake kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wa ufisadi kwani hilo ni jukumu la vyombo alivyoviteua kuchunguza na kuchambua nani afikishwe huko baada ya kujiridhisha kwa ushahidi.

"Huu ni utawala wa sheria, Rais Kikwete hawezi kutoa amri za kukamata watu wakati kuna vyombo alivyoviteua kuchunguza na kuchukua hatua." Waziri Chakawe alisema hayo jana alipokuwa katika mahojiano maalumu na gazeti hili ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Alisema kitendo cha baadhi ya Watanzania kumshinikiza Rais Kikwete awafikishe mahakamani watuhumiwa wa ufisadi kinaashiria kuwa wanataka aamuru watuhumiwa hao wapelekwe mahakamani bila kutumia vyombo husika jambo ambalo haliwezekani katika mfumo wa kibepari.

"Enzi zile za mfumo wa ujamaa na chama kimoja cha siasa, hilo lingewezekana lakini wakati huu ambao nchi inatumia mfumo wa kibepari, haiwezekani," alisema Chikawe.

Hivi karibuni, wanasiasa na hata baadhi ya viongozi waliowahi kuwa serikalini awamu zilizopita, wakichangia mada ya mustakabali wa taifa kwenye kongamano la taasisi ya Mwalimu Nyerere, waliitaka CCM imtose Rais Kikwete asigombee tena ili kumalizia ngwe ya miaka mingine mitano, iwapo atashindwa kufanya maamuzi magumu ya kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi.

Alionya kwamba Rais Kikwete akikurupuka katika hilo, kesi nyingi zitakwaa kisiki mahakamani na itabidi hao wanaoitwa mafisadi kulipwa mabilioni ya fedha kama fidia ya usumbufu.

Chikawe alisema mawazo ya namna hiyo yanatokana na watu wengi kuendelea kuwa na mtazamo wa mfumo wa kijamaa na chama kimoja na kusahau kuwa tayari nchi imeingia katika mfumo wa kibepari.

Waziri Chikawe alitumia mfano wa enzi za waziri mkuu, hayati Edward Sokoine alipopambana na wahujumu uchumi kwa kutoa amri ya kukamatwa watu ovyo na kutaifishwa mali zao kuwa moja ya mifano ya uongozi katika mfumo wa ujamaa.

Alisema amri hizo zilikubalika kulingana na mazingira ya wakati lakini, ulipoanza kuingia mfumo wa kibepari waliopoteza mali kupitia operesheni hiyo walidai haki kupitia mahakama na walishinda hivyo serikali ikabidi iwafidie pamoja na usumbufu.

Waziri huyo mwenye dhamana ya kusimamia katiba na sheria za nchi, ambaye amekuwa kimya licha ya kuwepo na mijadala mingi inayokosoa utendaji wa vyombo vya sheria nchini hasa suala la ufisadi, alisema polisi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wana haki ya kuchunguza makosa ya jinai, lakini pia mkurugenzi wa mashtaka (DPP) ana mamlaka ya kutoruhusu kesi hizo zisiende mahakamani kama hakutakuwa na ushahidi wa kutosha.

Alitoa mfano wa Mbunge wa Igunga, Rostam Azizi (CCM) ambaye wengi wamekuwa wakimtuhumu kwa ufisadi kupitia kashfa ya kampuni tata ya Richmond iliyopewa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura mwaka 2006, akisema hakuna ushahidi wa kumfikisha mahakamani.

"Wewe jaribu kuipitia ile ripoti ya Kamati Teule ya Bunge ya (Dk Harrison) Mwakyembe, hata uipitie mara 10. Mimi nimeipitia mara nane, sijaona sehemu ya kupata ushahidi wa kumshtaki," alisema Chikawe.

Kuhusu anwani ya barua pepe ya kampuni ya Caspian ambayo inamilikiwa na Rostam kutumiwa na kampuni iliyoirithi Richmond, alisema: "Ni sawa, lakini hadi sasa hakuna mahali popote ambapo kampuni ya Dowans inatuhumiwa. Yenyewe ilipokea jukumu ambalo Richmond ilishindwa lakini wao wakatekeleza. Ingekuwa Dowans wana matatizo, basi hata Rostam angeweza kuhusishwa."

Alizungumzia shinikizo la kutaka Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hoseah awajibishwe kwa madai ya kuficha madhambi ya Richmond ambayo kamati ya Dk Mwakyembe iliyaweka wazi, alisema:

"Takukuru ilichunguza mwenendo wa utoaji wa zabuni kwa Richmond na kwenye ripoti yake ikaeleza haikuona fedha zilizotumika kurubuni mtu yeyote. Na hata kamati ya Dk Mwakyembe haikubaini kitu cha namna hiyo.

"Kamati ya Dk Mwakyembe imebaini udhaifu wa serikali kuchunguza Richmond kabla ya kuingia mkataba na hili ndilo lililofanya Lowassa na wenzake kujiuzulu na Baraza la Mawaziri kuvunjwa."

"Lakini uzuri ni kwamba Rais Kikwete alikuwa ameagiza wasipewe fedha hadi wawe wameleta mitambo nchini na hilo lilifanyika. Kampuni ya Richmond haikuchukua hata senti ya serikali. Kama ilihonga watu kwa siri huko, ilikula kwao. Ila tunachojua walishindwa kuleta mitambo ya kuzalisha umeme wakatoa kazi hiyo kwa Dowans ambao walifanikisha."

Pamoja na hali hiyo, Chikawe alisema Mtanzania yeyote mwenye ushahidi unaoweza kuwashtaki wanaotuhumiwa ni vyema akawasiliana na Mpelelezi Mkuu wa Makosa ya Jinai (DCI) au Takukuru.

Kuhusu majibizano yaliyotokea hivi karibuni baada ya Dk Hosea kumlaumu DPP, Elieza Feleshi kwa kukalia mafaili zaidi ya 60 ya kesi za ufisadi na baadaye Feleshi kumjibu kuwa ni muongo, Chikawe alisema ni jambo ambalo halikumpendeza.

"Kwa kweli imekuwa bahati mbaya vyombo hivi vya serikali kulumbana vyenyewe, lakini nafikiri ilikuwa ni bahati mbaya tu, wakati mwingine hilo halitatokea," alisema Chikawe.

Hata hivyo, alisema huenda lilichangiwa pia na vyombo vya habari kwa kuchokonoa mambo hayo hivyo kuwafanya kutoa kauli ambazo pengine zilionekana kuhitilafiana.

Chikawe ambaye ni Mbunge wa Nachingwea alisisitiza kwamba DPP amekuwa akipelekewa mafaili mengi na anapoona hayana ushahidi wa kutosha huwashauri wahusika mambo ya kufanya na pengine kuwaeleza kwamba hakuna kesi ya kujibu.

CHANZO: Mwananchi

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget