Wednesday, 31 January 2007

Asalam aleykum,Katika makala ya wiki iliyopita niliwaletea mchapo kuhusu kasheshe iliyokuwa imetawala vyombo vya habari vya hapa Uingereza kuhusiana na kipindi cha “Celebrity Big Brother”.Kasheshe hiyo iliyovuka mipaka na kuchukua sura ya kimataifa,iliwahusisha washiriki watatu ambao ni wazaliwa wa hapa dhidi ya Shelpa Shetty,staa wa filamu za Bollywood aliyealikwa kushiriki katika kipindi hicho kutoka India.Watatu hao walilalamikiwa na maelfu ya...

Tuesday, 23 January 2007

KULIKONI UGHAIBUNI-47Asalam aleykum,Kwa zaidi ya wiki sasa, habari iliyotawala zaidi hapa Uingereza ni kasheshe iliyojitokeza ndani ya jumba walimohifadhiwa washiriki wa kipindi kiitwacho “Celebrity Big Brother.”Hii ni Big Brother kama ile aliyoshiriki Mwisho kule “Sauzi” lakini hapa washiriki ni watu maarufu (au waliowahi kuwa maarufu). Kipo kipindi kingine kinachofanana kabisa na kile cha akina Mwisho ambacho kinawashirikisha watu wa kawaida (wasio...

Tuesday, 16 January 2007

KULIKONI UGHAIBUNI-46Asalam aleykum,Wiki hii ilianza vizuri kwa Watanzania wanaoishi hapa Uingereza kutokana na ziara ya Rais Kikwete.Kama nilivyoonyesha wasiwasi wangu katika makala iliyopita kuhusu iwapo ningehudhuria mkutano wa JK na wabongo hapo London,ndivyo ilivyotokea.Kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu sikubahatika kuhudhuria mkutano huo uliofanyika Jumapili iliyopita.Labda ntabahatika atakapokuja tena mwezi ujao kama alivyoahidi.Kwa...

KULIKONI UGHAIBUNI-45:Asalam aleykum wasomaji wapendwa.Naomba nami niungane na Watanzania wengine kumpongeza Mama Asha-Rose Migiro kwa kuteuliwa kwake kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.Kwa hakika uteuzi huo unaiweka nchi yetu katika nafasi nzuri zaidi kwenye siasa za kimataifa na pia unasaidia kuitangaza nchi yetu.Pamoja na ukweli kwamba katika siku za hivi karibuni baadhi ya nchi duniani zimeanza kupoteza imani na Umoja wa Mataifa,chombo...

KULIKONI UGHAIBUNI-44Asalam aleykum,Heri nyingine ya Mwaka Mpya 2007.Nimesema “nyingine” kwa vile nilishatoa salamu kama hizo kwenye makala ilopita.Naona mwaka mpya umeanza kwa kasi nzuri sana huko nyumbani.Hatimaye TANESCO wametangaza kuwa mwaka huu hakutakuwa na mgao wa umeme,na kama utatokea basi sababu itakuwa ni matatizo ya kiufundi au hujuma. Nadhani hujuma hizo ni pamoja na wizi wa mafuta ya transfoma…mafuta ambayo inadaiwa hutumiwa na baadhi...

KULIKONI UGHAIBUNIAsalam aleykum,Nadhani pilika za Krismasi zimekwisha salama.Sasa tunausubiria mwaka mpya ambao tutauanza Jumatatu ijayo.Makala yangu ya leo inaambatana na salamu zangu za mwaka mpya lakini kwa mtazamo wangu binafsi.Kwanza naomba niseme mie naweza kuitwa mhafidhina linapokuja suala la sikukuu.Jinsi navyoziadhimisha baadhi ya sikukuu inaweza kabisa kuonekana kama ni dharau kwa siku hizo.Hapana,sio dharau bali kwa mtizamo wangu nadhani...

KULIKONI UGHAIBUNI-42 Asalam aleykum,Natumaini wengi wenu mko katika maandalizi ya sikukuu ya Krismasi.Uzuri wa Bongo ni kwamba sikukuu za kidini zinakuwa kama za kitaifa na ndio maana inapokuwa siku kama Idd utaona Wakristo wakijimwayamwaya sambamba na Waislam kama ambavyo kwa wakati huu Waislam nao wanajumuika na wenzao Wakristo kwa maandalizi ya Krismasi.Na ndivyo inavyopaswa kuwa na kudumishwa milele.Sikukuu ni furaha na furaha hiyo inapaswa...

KULIKONI UGHAIBUNI-41Asalam aleykum,Leo nawaletea habari mbalimbali zilizotawala kwenye anga hizi.Kwanza nianze na uzinduzi wa matangazo kwa lugha ya kiingereza ya kituo cha televisheni cha Aljaazera.Japo huduma hiyo imeanza hivi majuzi tu lakini tayari imeonekana kuwavutia watu wengi wanaofuatilia habari za kimataifa.Miongoni mwa “hobi” zangu ni kuangalia runinga na vipindi navyopendelea zaidi ni vya habari.Na nilikuwa na kiu kubwa ya kujua kitachotokea...

KULIKONI UGHAIBUNI-40Asalam aleykum,Kesho nchi yetu inatimiza miaka 45 tangu ipate uhuru.Kwangu,itakuwa ni zaidi ya sherehe ya uhuru.Kesho ni siku yangu ya kuzaliwa.Natimiza miaka 35.Natanguliza asante zangu kwa wale wote watakaonipa “hepi bethdei ” na kwa wenye husda “watalijua jiji.”Kwa namna flani ni kama nimebahatika “kushea” siku moja ya kuzaliwa na nchi yangu.Siku maalumu kama hiyo hutumika kuangalia wapi umetoka,wapi ulipo na wapi unaelekea.Kadhalika,wakati...

KULIKONI UGHAIBUNI-39:Asalam aleykum,Leo ni siku ya UKIMWI duniani.Ni siku ambayo kwa wengi ni ya majonzi kwa vile ni kumbukumbu ya wapendwa wao ambao wamepoteza maisha kutokana na gonjwa hili ambalo hadi sasa halina tiba.Pia ni siku ngumu kwa mamilioni ya wenzetu ambao wameambukizwa na virusi vya ugonjwa huo hasa kwa vile ni mwaka mwingine unakamilika pasipo dalili kwamba lini zahma hii itaondoka katika uso wa dunia.Kadhalika siku hii inawagusa...

KULIKONI UGHAIBUNI-38Asalam aleykum wasomaji wapendwa.Katika makala yangu moja ya hivi karibuni nilibashiri kuwa Rais George W Bush na Chama chake cha Republican wangepewa hukumu yao stahili katika uchaguzi wa katikati ya muhula ulofanyika hivi karibuni,na hukumu hiyo ingeelemea zaidi kwenye suala la vita ya Irak.Na ndivyo ilivyokuwa.Japo miaka kadhaa nilishawahi kuwa “mtabiri wa nyota” kwenye magazeti ya Komesha na Kasheshe (unazikumbuka nyota za...

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget