Baadhi ya Watanzania wanaoishi hapa Uingereza waliendesha harambee ya kuchangia wahanga wa milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam. Picha za harambee hiyo katika mji wa Reading. ...
Yayumkinika kuhisi kuwa laiti Baba wa Taifa angefufuka leo huenda angeishia kutoa machozi.Taifa alilohangaika na wenzie kulipigania uhuru limegeuka kituko.Upande mmoja tunamwona Rais wetu akijibidiisha kusaka amani Ivory Coast ilhali wakazi wa Gongo la Mboto wanaporwa amani na usalama wao na wazembe...
Katika harakati zake duni za kujinasua uhusika wake katika suala la ujambazi wa Dowans,Rais Jakaya Kikwete alijaribu kuwahadaa Watanzania kwa kudai,pamoja na mambo mengine,kuwa "hawajui wamiliki wa Dowans". Na kwa bahati nzuri kwake,vyombo vyetu vya habari vikaishia kumnukuu tu.Lakini kwa minajili ya...
Maandamano ya kupinga tawala dhalimu,ambayo yamesambaa maeneo kadhaa ya Afrika Kaskazini,yanaanza kuonyesha dalili za kusambaa sehemu nyingine za bara la Afrika hadi Cameroon,Gabon,Zimbabwe na Mauritania. Nchini Cameroon,kulikuwa na mpango wakufanya maandamano jana kwa lengo la kumwondoa madarakani...
Kuna taarifa kwamba mtu aliyetambulishwa kama mmiliki wa kampuni ya Dowans, Brigedia Jenerali (Mstaafu) Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi ni kiini macho. Chanzo cha kuaminika kinaeleza kuwa tukio zima la "mmiliki wa Dowans kuzungumza na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari" ni sehemu tu ya mkakati...
Picha hizi za kutisha zinajieleza zenyewe.Hakuna maelezo yanayotosheleza kueleza kwa ufasaha kuhusu janga hili.Lakini kwa vile kamwe hatutoelezwa chanzo cha milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto,kama ambavyo hatukuelezwa chanzo cha milipuko iliyotokea mwaka juzi huko Mbagala,ni muhimu kwa kila Mtanzania...
Tunaendelea kuwaletea updates za tukio la milipuko ya mabomu jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali,hadi sasa inakadiriwa zaidi ya watu 20 wamepoteza maisha katika tukio hilo.Tovuti ya Shirika la Habari la Uingereza (BBC) Idhaa ya Kiswahili inaripoti:Hali ya taharuki imetanda mji wa Dar...
Habari kutoka Dar es Salaam zinaeleza kuwa milipuko kadhaa imetokea maeneo ya Gongo la Mboto.Hata hivyo habari nyingine zinadai kuwa milipuka hiyo imetokea maeneo ya Kisarawe Bado hakuna taarifa rasmi kuhusu eneo na chanzo cha milipuko hiyo japokuwa habari zilizopo zinadai milipuko hiyo imetokea kwenye...
Pichani ni Mbunge John Komba wa CCM 'akiwa makini' kwa kuuchapa usingizi Bungeni Dodoma.Hata huyu naye anastahili 'zawadi' ya milioni 90?Hivi kweli inaingia akilini kusikia kwamba Serikali ya Kikwete ina mpango wa kuwapatia wabunge shilingi milioni 90 kila mmoja "kwa sababu inazojua yenyewe?Majuzi tu...
Hatimaye mmoja wa wanasoka mahiri kabisa duniani,Ronaldo wa Brazili,ameamua kuundika madaluga.Staa huyo mwenye kipaji cha hali ya juu ametangaza kustaafu rasmi soka.Katika makala hii nawaletea video za kumbukumbu ya nguli huyo wa kandanda.Picha zote hizo ni kwa hisani ya gazeti la Daily Mail la hapa...
Leo ni Siku ya Mtakatifu Valentine,maarufu kama Siku ya Wapendanao,au Valentine's Day kwa kimombo. Pengine ni vema kuadhimisha siku hii kwa kutafakari umuhimu wa upendo.Binafsi,si muumini mzuri wa siku zinazoambatana na matukio.Kwa mfano,mara nyingi huwa naadhimisha siku yangu ya kuzaliwa kwa sala na...
Kumekuwa na tetesi za muda mrefu kuwa hali ya uchumi wa Tanzania ni mbaya.Hata hivyo,kama ilivyozoeleka,wahusika serikalini wameendelea kuwanyima Watanzania haki yao ya msingi ya kufahamishwa hali ya uchumi wa taifa lao. Hivi karibuni Gavana wa Benki Kuu,Profesa Benno Ndulu,alizungumza na waandishi...
Zoezi la ujenzi wa jarida kamili mtandaoni linaendelea vema.Lakini kama ilivyo pindi mtu anapohama kutoka sehemu moja kwenda nyingine,kuna vitu vinavyochukua muda kuwa timilifu.Naomba nichukue fursa hii kuwashukuru wanahabari-mtandaoni wenzangu waliokubali ombi langu kwao kunitundikia katika blogu zao tangazo la mabadiliko ya anwani ya mtandao huu.Nawashukuru sana.Na pia nawakaribisha sana kushirikiana nami katika tovuti hii shirikishi.Kwa wale niliowatumia...
Serikali ya Uswisi imetangaza kutaifisha mali zote za Dikteta Hosni Mubarak,ambaye jioni hii ameng'olewa madarakani na nguvu ya umma.Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa,haijafahamika iwapo serikali za Uingereza,Marekani na nchi nyingine za Magharibi ambako Mubarak ana mali zake (na kujichumia...
BLOGU HII YA Kulikoni Ughaibuni INAPENDA KUWAFAHAMISHA KUWA INAHAMIA KATIKA ANWANI MPYA MTANDAONI.AWALI BLOGU HIYO IMEKUWA IKIPATIKANA KATIKA ANWANI http://chahali.blogspot.com/ LAKINI SASA INAHAMIA KATIKA ANWANI MPYA YA http://www.blogger.com/goog_939388498 . http://www.chahali.comPAMOJA...
Mlolongo wa ushahidi kuwa Kikwete ni sehemu muhimu ya ustawi na mafanikio ya ujambazi wa Dowans,na uthibitisho kuwa nchi imemshinda.www-freemedia-co-tz www-mwananchi-co-tz www-freemedia-co-tz (1) www-mwananchi-co-tz (1) www-freemedia-co-tz (2) Www Uhurupublications Com ...
So CCM has turned 34!It's almost certain that you'll end up in confusion,if not a severe headache,or to make matter even worse feeling nauseated when you take time to reflect on where this exceedingly corrupt party came from.I remember back in the days when CCM used to be as important as one's...
Due to the growing demand and popularity of the hit reality show "Growing Up African" there have been several inquiries pertaining to television access. Growing Up African has become a huge success in several countries including the United States and U.K through the internet especially on their youtube...
Kuna jitihada zinazofanyika huko nchini Misri katika jitihada za kumaliza machafuko yaliyodumu kwa zaidi ya siku 10 sasa kushinikiza kung'oka madarakani kwa Rais Hosni Mubarak.Jitihada hizo zinafanywa na kundi linalojumisha "Kamati ya Watu wa Busara" (ni kama Wazee wa Busara lakini sio kama wale walioimbwa...
Dear all our Valued, Fans we are pleased to introduce to you our New track named Jiachie by Victor Mrisho (Producer Kita) Rama Records enjoy the song as we are approaching to Valentine enjoy.On Behalf of Umabe Arts CompanyFredy NjejeProject and Design Manager.Kwa pamoja Tunaendeleza Burud...