Wednesday, 8 July 2009


Neo-Nazis are plotting a 'spectacular' terrorist attack on Britain to fuel racial tension, Scotland Yard's counter-terrorism officers fear.

Senior officers have increased their surveillance of suspects to monitor their ability to carry out a deadly attack aimed at causing a 'breakdown in community cohesion'.

The chilling warning comes after last month's startling gains by the BNP in the local and European elections which many fear may 'embolden' violent Far-Right extremists.

Commander Shaun Sawyer, from the Met's specialist operations wing told a meeting of British Muslims last night: 'I fear that they will have a spectacular ...

'They will carry out an attack that will lead to a loss of life or injury to a community somewhere. They're not choosy about which community.'

His comments came after Commissioner Sir Paul Stephenson asked officers to examine what effect the recession could have on far-right violence.

And the news mirrors similar warnings of the threat from far-right sympathisers issued in America in recent months.

While countering a threat from Islamic extremists remains the priority many officers now believe that funds need to be funnelled towards preventing a possible strike by the Far-Right.

Threat level in the UK may be downgraded, says terror chief

Despite the warning, Assistant Commissioner John Yates today warned that counter terrorism police face budget cuts.

He admitted savings must be made in two years time despite the risks posed by the looming London 2012 Olympic Games.

The senior officer, who took control of Scotland Yard's specialist operations wing three months ago, said it would be "naive" to think counter terrorism work would escape the recession.

Last weekend it was revealed that a network of suspected extremists with access to 300 weapons and 80 bombs has been uncovered by counter- terrorism detectives.

Thirty-two people were questioned by police and 22 properties were raided over an alleged plot to bomb mosques.

It was the biggest terrorist arms haul since the IRA mainland bombings in the 1990s.

Sir Norman Bettison, the chief constable of West Yorkshire, said: 'The big bad wolf is still the Al-Qaeda threat.

'But my people are knocking over right-wing extremists quite regularly. We are interdicting it so that it doesn't first emerge into the public eye out of a critical incident like an explosion.'

It is more than 10 years since neo-Nazi nail bomber David Copeland attacked three targets in London in 1999.

Three people died at the Admiral Duncan gay pub in Soho.

Copeland also targeted the Muslim community in Brick Lane, east London, and a supermarket in Brixton, south London.

Abdurahman Jafar of the Muslim Safety Forum, where the concerns were raised, said:

'Muslims are the first line of victims in the extreme right's campaign of hate and division and they make no secret about that.

'Statistics show a strong correlation between the rise of racist and Islamophobic hate crime and the ascendancy of the BNP.'

Mark Gardner, of the Community Security Trust, which monitors violence against Jews, said there has been a surge in right-wing incidents.

He said: 'Ten years after the Nazi nail bombings in London, we are seeing increasing numbers of neo-Nazis being arrested in their attempts to start some kind of so-called race war.

'It is the Muslim community that appears to be most targeted, but all of society is at risk, and we are in regular discussion with police about the problem.

'Worse still, the recent electoral successes for the BNP may cause some would-be terrorists to be further emboldened in their actions.'

Last year neo-Nazi Martyn Gilleard, 31, was convicted of three terrorism offences and jailed for 16 years.

Gilleard idolised Adolf Hitler and urged sympathisers to act to preserve the 'purity of the white race'.

When police raided his flat they found bullets, swords, knives and four nail bombs under a bed used by his five-year-old child.

Officers also found DIY bomb manuals, a guide on making a sub-machine gun and internet instructions on carrying out assassinations by poison.

A speech he had recorded in a notebook mentioned 'killing Muslims, blowing up mosques and fighting back'.

No one at the Muslim Safety Forum was available for comment. The Metropolitan Police declined to comment.

Last month a white supremacist with links to the BNP shot dead a security guard at Washington's Holocaust Museum in a racially-motivated killing.

Before launching the attack, 88-year-old James von Brunn sent out an email claiming: 'It's time to kill all the Jews.'

Von Brunn was shot and wounded by museum security officers after he walked into the packed tourist attraction and began firing indiscriminately.

Saturday, 4 July 2009



KWANZA Merged

Picha kwa hisani ya KENNEDY

Wanasema siasa ni mchazo mchafu.Lakini siasa katika bara letu la Afrika ni zaidi ya mchezo mchafu.Ni mchanganyiko wa kanyaboya,songombingo,mbinde,usanii,ufisadi na what have you.Hiyo sio kumaanisha kuwa siasa katika maeneo mengine,kama Ulaya na kwingineko ni safi kihivyo.Lakini angalau hawa wenzetu check-and-balance mechanism zinafanya kazi kwa kiasi kikubwa.Sie tunazo lakini aidha wenye majukumu ya kuzitumia wako bize sana na posho au nyumba ndogo au hawajui kwa nini wapo mahala panapopaswa kufanya hiyo check na balance.

Hivi CCM walikuwa wanafikiri nini mwaka 2005 kuahidi kuwa wangeshughulikia uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi?Binafsi sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama hiyo as long as suala hilo linafanywa kwa uangalifu.Sio priority kwa sasa lakini kwa vile ni haki kwa Waislamu,then hakuna budi kuangalia uwezekano huo.Kwahiyo,CCM hawakufanya kosa "kukubali" kuanzisha Mahakama ya aina hiyo baada ya uchaguzi mkuu wa 2005.Hawakufanya kosa kwa vile wazo hilo sio baya au la hatari kama baadhi ya watu wanavyofikiria.Nitatafuta wasaa mwafaka siku nyingine kuelezea kwanini Waislam wako sahihi kudai mahakama hiyo na kwanini uanzishwaji wake hauna madhara kwa wasio waislam.In fact,suala sio "kuanzisha" bali "kurejesha" kwa vile mahakama za aina hiyo zilikuwepo wakati wa ukoloni na muda mfupi baada ya uhuru.

Kosa la jinai (yes,ni jinai) la CCM ni kutoa ahadi nyeti kama hiyo wakati inafahamu fika kwamba haina muda wa kuishughulikia.Ni kosa pia kwa vile pamoja na ahadi hiyo ya kuanzisha mahakama ya kadhi tayari chama hicho kilikuwa kimeshatoa ahadi nyingine lukuki kana kwamba kinaomba kutawala kwa miaka 100 na sio mitano (2005-2010)!Kulikuwa na ahadi za kuwakalia kooni wala rushwa,kushughulikia kero za Muungano,kuboresha maisha ya Watanzania,na ahadi nyingine kedekede.Si tu kwamba wakati tunaelekea mwishoni mwa miaka hiyo mitano rushwa imeshamiri na ku-mutate into ufisadi (kumbuka,neno hili limejitokeza katika kipindi hiki),kero za Muungano sio tu kuwa bado zipo ila tumeshuhudia "kibiriti kikitikiswa mpaka kinataka kulipuka",na hayo maisha bora kwa kila Mtanzania sanasana yamewezekana kwa mafisadi na washirika zao....

Hili la kuahidi kushughulikia masuala yanayogusa imani (ya kiroho) ilhali hakuna dhamira au uwezo wa kufanya hivyo ni jambo hatari mno.Dini ni hatari zaidi ya ukabila kwani inahusisha uhai na kifo (mtu akifa kwa ajili ya dini ni martyr,at least dini nyingi zinaamini hivyo).

Kauli za viongozi kuhusu suala hili sio tu zimekuwa za kujichanganya bali zimechangia kukuza tatizo hilo.Mara mchakato unaendelea,mara sheria za kiislam zitaingizwa kwenye sheria za mahakama za sasa (hicho tayari kinafanyika),mara hili,mara lile.Kama kawaida,wahusika wanasubiri lilipuke ndio watafute chanzo cha mlipuko.Unfortunately,milipuko mingine ikianza hata huo muda wa kutafuta chanzo hautokuwepo.Waulize Nigeria!

Tuiombee nchi yetu.












Michael Jackson mithili ya chura!?The Jacko mithili ya Bikira Maria!?Ukishangaa yanayohusu maisha na kifo cha the King of Pop basi hujakutana na "kazi za sanaa" zinazomhusu the Jacko.Picha za juu ni baadhi tu ya "kazi" hizo.Unajua,fani yenyewe ya sanaa imetawaliwa na ujanja ujanja wa namna flani.Kwa mfano nenda maeneo ya Msasani kwa wauza vinyago wa Kimakonde.Utakutana na kinyago cha Nyerere,kwa mfano,lakini zaidi ya ukweli kuwa kinyago hicho ni cha mpingo (kama alivyodai mchonga kinyago),the rest havifanani kabisa na Nyerere,unless uwe hujawahi kuona sura ya Baba wa Taifa.Pita pita mitaani,utakutana na wasanii wanaodai wanaweza kukuchora na wakikamilisha mchoro utadhani unajiangalia kwenye kioo.Of course,wapo wenye vipaji vya namna hiyo.Lakini kuna " wasanii" pia.Atakuchora,kisha akikupatia "picha yako" unaweza kuishia kutamani kumkaba loba (kabali) ya mbao!

Na kifo cha Michael kinaelekea kuwa dili la nguvu kwa WASANII kwa maana ya ARTISTS na WASANII kwa maana ya CONFIDENCE ARTISTS (con artists).Ama kweli kufa kufaana!



Friday, 3 July 2009


Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Mufti Issa bin Shaaban Simba, amekasilishwa na uamuzi wa serikali kuhusu Mahakama ya Kadhi.

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.

Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.

Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.

Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka .


CHANZO: Mwananchi


KWA MWENENDO HUU SI AJABU KUSIKIA HATA WATANZANIA WALIOAHIDIWA MAISHA BORA NAO WAKAJITOKEZA KUDAI HAWAITAKI CCM....HOJA IKIWA MAISHA BORA YALIYOAHIDIWA YAMEISHIA KWA KUNDI DOGO LA MAFISADI PEKEE!



In a recent interview with MTV News, The Game relayed Michael Jackson’s attempts to end the beef between him and 50 Cent. Although the rappers eventually laid the feud to rest (without Jackson’s help) the tension between the two still remained.However, The Game has finally taken it upon himself to give a formal apology, not just to 50, but to the whole Interscope label.“For 50, I’m just gonna apologize to him, just as a man,” he told MTV. “It has nothing to do with music, or beef, or nothing like that. It ain’t about being the bigger man. He can take it and say, ‘Game is apologizing,’ ‘Game’s a sucka, he’s apologizing.’ I’m apologizing for me to him, to [Dr.] Dre, to Jimmy Iovine, to Eminem, to all the fans. Because if you think about what Interscope was when we were gellin’, man we were it. We were an unstoppable force.”

He explained that while he was a member of G-Unit, there were some things he needed to do “for my career to have longevity, and for me to survive in Hip Hop music,” and this may have played a part in the dissolving relationship between himself and 50 Cent. He also expressed some regret that G-Unit and the Interscope label did not get to experience the success that it could have had, potentially.

“Now, four albums in, I can say as a man that G-Unit, Game, Aftermath, Black Wall Street, Interscope, Geffen, Eminem, Shady, from [Lloyd] Banks to [Young] Buck to [Tony] Yayo to Dre to whoever; If it woulda kept going: endless paper. Millions of albums sold. Because we were great together.”

The Game also expressed his strong belief that, had he and G-Unit (and perhaps Young Buck) not parted ways, many things would have been different.

“Me and Fif’s chemistry is what Method Man was to Redman when they get in. Red ain’t from Wu-Tang but you know when Meth gets wit' Redman it’s goin’ down… [Me and 50’s] biggest records were together. Whether I was on them or I wasn’t on them. Whether he was on them or he wasn’t on them. When we were in gellin’ writing together as a family, we had it man. If we never would have [broken] up, I think Detox would have been out and we all would have been selling millions from Banks to Buck, and Tony Yayo. I’m going to apologize for my role.”

50 Cent and the Aftermath camp have not yet issued a response.

SOURCE: Hiphopdx.com


Wednesday, 1 July 2009


CCM wafanya mkutano kanisani, wampiga kiongozi wa kigango

Na Frederick Katulanda, Biharamulo

WAFUASI wa CCM juzi walivamia Kanisa Katoliki, Kigango cha Nyantakara kilicho Kata ya Lusahunga na kufanya mkutano wao, huku wakimshambulia na kumjeruhi katibu wa kanisa hilo baada ya kuwaamuru watoke.

Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 3:00 asubuhi wakati wafuasi hao wa wanawake wa CCM, wakiongozwa na mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja la John, walipoingia kanisani humo kwa madhumuni ya kuchukua viti kwa ajili ya mkutano wao. Badala ya kuchukua viti, waliamua kutotoka na kufanyia mkutano huo kanisani.

Akizungunza na Mwananchi katekista wa kigango hicho ambacho kipo katika parokia ya Kaniha, jimbo la Kahama, Faustine Damas alisema wafuasi hao wa CCM waliingia kanisani na kuchukua meza ya kuendeshea ibada na kuigeuza kuwa meza ya wageni wao na baadaye kuendesha mkutano wao.

Alieleza kuwa alipofika kanisani alistaajabu kusikia nyimbo wa 'Tieni, tieni' ukiimbwa na baada ya kuingia ndani alikuta wakiwa wanaendelea na mkutano wao huku wakitumia meza kuu ya ibada, jambo ambalo lilimfanya ampigie simu katibu wa kigango hicho, Festus Masumbuko ambaye baada ya kuwaomba waondoke na kuwanyang'anya meza hiyo ya ibada, wafuasi hao wa CCM walianza kumpiga.

"Waliamua kugoma kuondoka na ndipo alipowanyang'anya meza ya ibada, lakini wakamvamia na kumpiga mateke na ngumi. Wamemjeruhi vibaya na pia wamemchania shati," alieleza katekista huyo.

Alisema kutokana na hali hiyo alilazimika kupiga kelele na ndipo wananchi walipofika na kumwokoa. Lakini wakati hali hiyo ikiendelea, mfuasi mmoja wa CCM alipiga simu polisi na kuwaeleza kuwa walikuwa wakifanyiwa vurugu na ndipo polisi walipoenda eneo hilo na kuwakamata wananchi waliokuwa wanataka kumuokoa katibu.

Wananchi hao wanashikiliwa na polisi kwa kufanya vurugu katika mkutano huku wana CCM wakiachiwa huru na kuondoka zao.

Kutokana na hali hiyo paroko wa parokia ya Kaniha, Padri Isaya Bahati ambaye pia ni msaidizi wa askofu wa jimbo la Kahama, alisema muda mfupi baadaye akiwa polisi kuwa amesikitishwa na vurugu hizo na kusisitiza kuwa kanisa kama nyumba ya ibada inapaswa kuheshimika kwa vile si uwanja wala ukumbi wa mikutano.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, naibu katibu mkuu wa CCM, George Mkuchika alisema hana taarifa ya vurugu za wafuasi wake kanisani na kwamba kwa kuwa amepokea taarifa hizo, atazifuatilia kwa kina.

“Ngoja nifuatilie kwa kina kujua ni nini kimetokea,” alieleza Mkuchika.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Henry Salewi alisema kuwa hakuwa kwenye eneo la uchaguzi na kumtaka mwandishi awasiliane na kamishina Telesphol Anaclet ambaye ndiye amekuwa akishughulikia masuala hayo. Hata hivyo, kamishna huyo alisema jeshi la polisi linaendelea na masuala yake hivyo lipewe nafasi ya kufanya kazi.

“Naomba mtuache tufanye kazi yetu sina cha kukueleza kwa sasa,” alisema kamishina huyo wa oparesheni maalumu ya uchaguzi na akakata simu.

Waliokamatwa na jeshi hilo la polisi wametajwa kuwa ni Evarist Dotto, Semen Elias, Mosha Makoye, Batista na Timetheo ambao walitambulika kwa jina moja.

CHANZO: Mwananchi

HITIMISHO LISILOHITAJI TAFAKURI YA KINA NI KWAMBA CCM IMEFILISIKA KISIASA,NA KATIKA KUTAPATAPA KWAKE IKO TAYARI HATA KUWEKA REHANI AMANI NA UTULIVU WA TAIFA LETU.

NA KWA JINSI ILIVYOSHINDWA KUJINASUA NA TUHUMA KWAMBA INAKUMBATIA UFISADI NA MAFISADI,NI DHAHIRI KAMPENI ZA 2010 ZITASHUHUDIA MAZINGAOMBWE,UHUNI NA UPUUZI ZAIDI YA HUU.DINI NI KITU HATARI KINAPOTUMIWA KWA MINAJILI YA UBINAFSI WA KISIASA JAPO BINAFSI SINA KIPINGAMIZI NA KUCHANGANYA DINI NA SIASA ALIMRADI WAHUSIKA WAWE MAKINI KUTENGANISHA LIPI LA KAIZARI NA LIPI LA KIROHO.

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget