Monday, 6 August 2012
Sunday, 5 August 2012
BOLT AKIVUKA MSTARI NA KUSHINDA |
USAIN BOLT AKIMALIZA MBIO NA KUSHINDA |
USAIN BOLT AKIONYESHA POZI YAKE MAARUFU YA 'RADI' (LIGHTNING BOLT) BAADA YA KUSHINDA |
USAIN BOLT AKIWEKA POZI YAKE BAADA YA KUSHINDA |
USAIN BOLT AKIINAMISHA KICHWA ARHDINI BAADA YA KUSHINDA |
USAIN BOLT NA YOHAN BLAKE WAKISHANGILIA NA MASHABIKI |
USAIN BOLT AKIWA NA MDOLI (MASCOT) WA OLIMPIKI |
USAIN BOLT HAKUANZA VIZURI SANA KWENYE MSTARI (LANE) WA SABA LAKINI AKAMUDU KUSHINDA KWA KISHINDO |
BINADAMU WENYE KASI KULIKO WOTE DUNIANI |
NI USAIN BOLT TENA |
USAIN BOLT AKIMALIZA MBIO KWA KISHINDO |
BINADAMU MWENYE KASI ZAIDI USAIN BOLT AKIWEKA REKODI MPYA YA OLIMPIKI HUKU PATNA WAKE WA MAZOEZI ,MJAMAIKA YOHAN BLAKE (WA TATU KULIA) AKISHIKA NAFASI YA PILI NA MMAREKANI JUSTIN GATLIN (WA TATU KUSHOTO) AKISHIKA NAFASI YA TATU |
USAIN BOLT AKIWEKA REKODI MPYA |
MATOKEO |
MWANARIADHA WA MAREKANI JUSTIN GATLIN ALIYESHIKA NAFASI YA TATU AKIMWANGALIA USAIN BOLT |
USAIN BOLT AKIPITA PEMBENI YA 'MWENGE WA OLIMPIKI' BAADA YA KUSHINDA MBIO ZA MITA 1OO WANAUME |
MWANARIADHA WA JAMAIKA ASAFA POWEEL AKIWA AMESHIKA TAMA BAADA YA KUMALIZA WA MWISHO KUFUATIA MATATIZO YA MISULI |
MASHABIKI KATIKA KITONGOJI CHA BRIXTON JIJINI LONDON WAKISHANGILIA USHINDI WA USAIN BOLT |
MASHABIKI WAKISHANGILIA KWENYE UWANJA WA O2 HUKU WAKIONYESHA POZI YA USAIN BOLT |
DUKE NA DUCHESS WA CAMBRIDGE NA PRINCE HARRY WAKIWA NA 'WAZIRI' WA UTAMADUNI JEREMY HUNT (NYUMA YA DUKE) |
DUKE NA DUCHESS WA CAMBRIDGE (PRINCE WILLIAM NA MKEWE KATE MIDDLETON-WA KWANZA NA WA PILI KUSHOTO) WAKIFUATILIA KASI YA USAIN BOLT HUKU PRINCE HARRY AKIWA AMEJITUNDIKA BENDERA YA JAMAIKA |
YOHAN BLAKE, PATNA WA MAZOEZI WA USAIN BOLT ALIKUWA AKITARAJIA KUTOA UPINZANI MKALI LAKINI AKAISHIA KUWA WA PILI |
USAIN BOLT AKIFANYWA MBWEMBWE KABLA YA MCHUANO |
JUMUIYA YA WAJAMAIKA KATIKA KITONGOJI CHA BRIXTON,JIJINI LONDON WAKIFUATILIA USHIRIKI WA WANARIADHA WAO |
CHANZO: Daily Mail
Saturday, 4 August 2012
17:35
Unknown
DMV, Watanzania Marekani
No comments
Makada wa CCM wakiwa na kadi za uwanachama kwa wanachama wapya katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.
Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akipata picha na tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha CCM, katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.
Tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha Mapenduzi CCM
Baadhi ya waTanzania mbali mbali waliohudhuria kwenye futari hiyo ilioandaliwa na tawi la CCM DMV
Baadhi ya waTanzania waliovalia rangi za chama cha CCM wakiwa kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.
Watanzania waliojumuika kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.
Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akiwakaribisha rasmi wageni walikwa kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.
Baadhi ya wanachama wa CCM Tawi la DMV wakipata picha ya pamoja baada ya futari walioiyanda
Wanachama wa CCM Tawi la DMV na baadhi ya wageni wawili kutoka Londan Uingereza
Wageni wawili majirani wapendanao kutoka jijini London pia walihudhuria katika futari hiyo ilioandaliwa na ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani
Katibu wa CCM DMV Jacob Kinyemi, kushoto akipata picha ya pamoja na Halima baada ya kumkabidhi rasmi kadi ya uwanachama wa CCM, Jana Ijumaa na kuwa mwanachama rasmi wa CCM
Chanzo: SWAHILIVILLA
06:30
Unknown
rap, The Arab Spring
No comments
The Arab Spring: Dawn of a musical revolution
Across North Africa and the Middle East people have risen up and demanded a voice. And while the calls may have been political in nature, protestors have used various cultural means to express their desire for change, including music and, specifically, rap.
Media has been at the very heart of the demands for change, with the young using tools such as the internet to spread their message. Music has been another weapon. So often a voice for the disenfranchised, rap music has political defiance and revolutionary ideals at its very core. So it is hardly surprising that the genre has taken off in North Africa in the past 18 months, providing people with the means to express themselves.
The changing voice of rap music
Coming out of the U.S. in the 70s, rap became a global phenomenon in the 80s and has had a presence in North Africa since the 90s. But it is only with the demise of dictatorships in Tunisia, Egypt and Libya that the genre was able to free itself from censorship.
Previously, few had dared to speak out against their governments, fearful of retribution. But the Arab Spring has given young musicians the confidence to speak out. Some of the biggest artists in this musical groundswell are Tunisia's El General, DJ Costa and Psyco-M; Egypt's Ahmed Mekky, Ramy Donjewan and Arabian Knightz; and Libya's Emad Abbar and Hamza Sisi. The popularity of these and other artists continues to grow by the day.
The revolution will be televised… online
The internet has made it easier than ever to share music and in the face of state censorship artists relied on the Web to spread their message enabling their songs to spread from city to city and cross national boundaries.
Traditional media channels such as newspapers and television may have been muted by state control, but crumbling regimes were powerless to contain Twitter and Facebook. These social tools gave young people across North Africa a way to connect with others who felt the same and unite behind the revolutionary ideals expressed in the lyrics of their songs.
SOURCE: Yahoo! News
Friday, 3 August 2012
19:28
Unknown
RAIA MWEMA
No comments

KUNA msemo mmoja ninaopenda sana kuutumia kusisitiza hoja katika maongezi, ambao unasema, “Ili uweze kulielewa giza inabidi utoke au uende katika mwanga, na kinyume chake (vice versa).”
Huwa ninautumia msemo huu kubainisha ‘faida’ tuliyonayo baadhi yetu (Watanzania) tulio nje ya nchi yetu. Kwamba, kuwa kwetu huku kwa namna fulani kunatusaidia kuwa kama kile kinachofahamika katika tafiti kuwa ni “participant as an observer,” yaani kwa tafsiri isiyo rasmi ‘mshiriki ambaye pia ni kama mwangalizi.’
Kwa kuwa huku ughaibuni sio tu tunapata fursa ya kulinganisha tofauti ya mambo kati ya hapa na huko nyumbani bali pia tunaweza kuiangalia jamii yetu inayotuhusu lakini tukabaki watazamaji.
Hata hivyo, kuna wakati baadhi yetu tulio nje hukumbanana wakati mgumu kuzungumzia mambo ya huko nyumbani, hususan, kutokana na madai kuwa yanayotokea huku hayatugusi moja kwa moja.
Baadhi ya ‘wapinzani wetu’ hudiriki kwenda mbali zaidi na kutulinganisha na Watanzania ‘tusio kamili’ kwa maana ya kwamba shida au raha za huku hazitukabili katika namna zinavyowakabili wao.
Huu ni mtizamo potofu hasa ikizingatiwa kuwa wengi wetu, kama si sote, bado tuna ndugu, jamaa na marafiki huko nyumbani. Kimsingi, kuwa nje ya Tanzania hakumpunguzii mtu Utanzania wake, isipokuwa tu kwa wenzetu wachache ambao kuwa kwao huku kunamaanisha ‘talaka’ kati yao na asili yao.
Ni katika kuiangalia nchi yetu kwa mtizamo huo wa ‘mshiriki ambaye ni kama mwangalizi’ ndipo nimejikuta nikifikia hitimisho kwamba mwenendo wa mambo huko nyumbani una mushkeli.
Kati ya wiki iliyopita na muda huu ninapoandaa makala hii kumejitokeza matukio kadhaa yanayoweza kuashiria kuwa nchi yetu inakwenda ‘ndivyo sivyo.’
Nitatoa mifano machache. Habari ambayo imetawala katika vyombo vingi vya habari kwa sasa kuhusu mambo yalivyo huko nyumbani ni hili suala la baadhi ya wabunge kutuhumiwa kupokea rushwa.
Habari hiyo inapata uzito mkubwa zaidi pale inapotanabahisha kuwa licha ya baadhi ya wabunge kuandamwa na tuhuma hizo, baadhi ya Kamati za Bunge pia zinatuhumiwa kujihusisha na rushwa, hali iliyopelekea Spika wa Bunge kuamua kuivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.
Lakini tuhuma hizi za rushwa zimefichua kitu ambacho binafsi ninakiona kama tatizo la msingi katika jamii yetu. Katika siku chache zilizopita, nimekuwa nikitumia muda wangu mwingi katika mtandao wa kijamii wa twitter kuzungumzia tuhuma hizo dhidi ya wabunge, hususan, wale wanaodaiwa kupokea mlungula ili kulifisadi Shirika la Umeme (TANESCO).
Jumapili iliyopita mmoja wa tunaoweza kuwaita watu maarufu (celebrities) alionekana kuchukizwa na twiti zangu ambazo kimsingi zilikuwa zinaelekezwa kwa mbunge mmoja wa chama cha upinzani ambaye ametangaza dhahiri kuwa ana nia ya kuwa rais wetu huko mbele.
Katika mazingira ya kawaida tu, mwanasiasa anayetamka hadharani kuwa anataka kuwa rais ni lazima aangaliwe kwa makini ili wapiga kura wapate fursa nzuri ya kumuelewa.
Kwa sababu anazozijua yeye binafsi, celebrity huyo wa kike alinivurumishia maneno makali akidai kuwa tuhuma nilizotoa dhidi ya mwanasiasa huyo zina dalili za chuki binafsi, hasa kwa ile haijathibitishwa kuwa mwanasiasa huyo ni fisadi.
Lakini kabla sijatulia, mwanamama mwingine msomi na mwenye wadhifa kwenye taasisi moja ya umma naye akanihoji ni mahali gani mwanasiasa huyo ametajwa kuwa ni mwizi. Labda hadi hapa msomaji unaweza kujiuliza kwanini ‘utetezi’ dhidi ya mwanasiasa huyo unaonekana kwa jinsia moja tu.
Huyu mtu wa pili kukerwa natwiti zangu kuhusu mwanasiasa huyo ndiye aliyenigusa zaidi, kwa sababu kimsingi, elimu na madaraka yake yanamweka katika kundi la kijamii linalofahamika kama tabaka la kati.
Nilishawahi kuandika katika makala moja huko nyuma kuhusu jinsi tabaka hili la kati linavyoshindwa kuwa kiunganishi cha kupigania maslahi ya tabaka la chini la walalahoi.
Nilieleza katika makala hiyo kwamba tabaka la kati lingeweza kuwa nguvu muhimu ya kupigania maslahi ya tabaka la chini kutambuliwa, na hatimaye kufanyiwa kazi na tabaka la juu (ambalo hujumuisha tabaka tawala).
Nikinukuu maneno ya binti huyo wa pili, alinieleza kuwa “wanamchukia mwanasiasa huyo wajinyonge, kwani njia yake kuelekea Ikulu ipo wazi.” Niliguswa sana na maneno haya kwa sababu wakati mwanasiasa huyo anaonekana kupata utetezi katika tuhuma zinazomkabili kuhusu kuifisadi TANESCO, sio tu kuna watuhumiwa wengine wasiotetewa bali pia hata huko nyuma baadhi ya wanasiasa waliotuhumiwa kuwa mafisadi hawakuwahi kutetewa kiasi hicho.
Japo ninatambua na kuheshimu haki ya kila Mtanzania kumtetea mwanasiasa anayempenda, ukweli ni kwamba licha ya utetezi huo kuwa wa ‘upendeleo’ (kile kinachoitwa na Waingereza kuwa ni haki ya upendeleo-selective justice), kwa maana ya kuwa watuhumiwa wengine kwenye kashfa hiyo hawapati utetezi kama ilivyo kwa mwanasiasa huyo, tunapotetea tuhuma za ufisadi kwa vile tu ‘tuna mahaba’ na tunaowateta, tunaweza kuwafahamasisha mafisadi wengine waendelee kuitafuna nchi yetu wakijua watatetewa.
Moja ya mambo yanayokwaza sana maendeleo yetu ni kile ninachokiita ‘siasa za mahaba.’ Kwamba mgombea uongozi hapimwi kutokana na sifa na/au uwezo wa kutumikia umma bali kinachoangaliwa ni urafiki, haiba na vitu kama hivyo visivyoweza kuwa vigezo vya uongozi bora
Bado ni mapema kutoa hitimisho kuhusu wabunge wanaotuhumiwa kujihusisha na rushwa, hususan hiyo ya kuihujumu TANESCO, ukweli kwamba tuhuma hizo zimewekwa hadharani unaeleza bayana kuwa ufisadi umeingia katika hatua mpya na ya hatari zaidi ambapo baadhi ya watu tuliowakabidhi dhamana ya kutunga sheria (ikiwa ni pamoja na zile za dhidi ya ufisadi) nao ni sehemu ya tatizo la ufisadi.
Nimebainisha hapo mwanzoni kuwa matukio ya hivi karibuni yanaashiria kwamba hali ya mambo si shwari. Jingine lililonigusa ni suala la mgomo wa walimu ambapo japo kumekuwa na taarifa za kukanganya, kuna dalili kuwa mgomo huo unaendelea.
Lakini tukio lililotokea katika shule ya msingi ya Maili Moja, Kibaha, linaweza kutufumbua macho zaidi kuhusu mwenendo wa nchi yetu. Inaelezwa kuwa katika tukio hilo, wanafunzi wenye hasira waliamua kuvurumisha mawe shule yao. Sina hakika kama walifanya hivyo kama ishara ya kupinga mgomo wa walimu wao au kuwaunga mkono, lakini kilicho wazi ni kuwa pindi inapofika mahala wanafunzi wa shule ya msingi wanachukua ‘sheria mkononi’ basi ni wazi kuwa Taifa letu limefika mahali pabaya.
Wanafunzi hawa ndio kizazi cha kesho, ndio mawaziri na wabunge wetu, ndio viongozi wa kesho. Sasa inapofika mahala nao wanaingia katika utamaduni mpya wa ‘vurugu kama ufumbuzi wa matatizo’ sijui huko mbele itakuwaje.
Majuzi tu tulishuhudia mgomo wa madaktari ambao bado unaelekea kuwa haujaisha kwa utimilifu (taarifa kwenye mtandao mmoja wa jamii inaeleza kuwa baadhi ya madaktari wameonyesha dhamira ya kutaka kurejea tena kwenye mgomo). Kabla hatujasahau kuhusu mgomo huo tunasikia jinsi baadhi ya wabunge wanavyoshiriki kuihujumu TANESCO.
Wakati huohuo tunashuhudia baadhi ya walimu wakiamua kutimiza azma yao ya siku nyingi ya kugoma. Lakini pengine kubwa na la kutisha zaidi ni taarifa kuwa mmoja wa viongozi maarufu wa dini amekumbwa na kashfa ya shule yake kuiba uniti za umeme wa TANESCO. Haya yote (na mengine ambayo nafasi hairuhusu kuyataja) yanaashiria kuwa hali si shwari huko nyumbani.
Je, viongozi wetu wanafanya nini kukabiliana na hali hii? Usidhani hiki ni kichekesho lakini siku moja kabla sijaandaa makala hii kulikuwa na taarifa kuwa Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai alionekana anaongea na simu wakati kikao cha Bunge kinaendelea.
Labda ilikuwa ni simu muhimu kutoka kwa Spika au pengine Rais, lakini taswira ilivyotokana na tukio hilo inaweza kutanabaisha ni jinsi mtizamo wangu kuwa hali ya mambo si shwari huko nyumbani ilivyotofautina baadhi ya viongozi wetu, ambapo hata kwenye majukumu muhimu ya kuogoza Bunge wanamudu kuongea na selula zao.
Funga kazi ni uamuzi wa Serikali kulifungia jarida la Mwanahalisi kwa muda usiojulikana kwa madai kuwa jarida hilo limekuwa likiandika habari za uchochezi.
Katika toleo lililopita jarida hilo kulikuwa na habari kuhusu suala la Dk. Steven Ulimboka na mtumishi wa taasisi nyeti ya serikali alihusishwa nayo. Je, serikali haidhani kuwa uamuzi wake kulifungia jarida hilo unaweza kutafsiriwa kama unalenga kulizuia kuibua ‘makubwa zaidi’ kuhusu sakata hiyo?
Hivi isingewezekana kulifikisha jarida hilo mahakamani ili haki si tu itendeke bali ionekane imetendeka? Na je, uamuzi wa kulifungia unasaidiaje kuzifanya habari zilizoandikwa nalo zionekane ni uchochezi tu.
Nimalizie kwa kutoa rai ya haja ya mjadala wa kitaifa kuhusu hatma ya Taifa letu. Tunakoelekea si kizuri. Na hili la mjadala si kuhusu tabaka tawala (walio katika bunge, serikali, nk) bali pia kuna haja ya mjadala wa kitaifa kuhusu nafasi ya tabaka la kati katika kuhamasisha, kutetea na hata kupigania maslahi ya tabaka la chini la walalahoi linaloelekea kuachwa bila mtetezi wala msomaji.
Tanzania ni yetu sote. Tuweke kando siasa za mahaba, tuepuke kutanguliza maslahi binafsi badala ya maslahi ya Taifa, tutatue tofauti zetu (migomo, nk) kwa njia za kidiplomasia, na kubwa zaidi tuungane kwa pamoja kuhangaikia kuipeleka nchi yetu katika mwelekeo sahihi.
Inawezekana, timiza wajibu wako.
Wednesday, 1 August 2012
02:45
Unknown
ZITTO KABWE
No comments
MAELEZO BINAFSI YA MHE. ZITTO ZUBERI KABWE DHIDI YA TUHUMA ZA RUSHWA HUSUSAN KUELEKEA KATIKA KUPITISHA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
MAELEZO BINAFSI YA MHE. ZITTO ZUBERI KABWE DHIDI YA TUHUMA ZA RUSHWA HUSUSAN KUELEKEA KATIKA KUPITISHA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
Ndugu Waandishi,
Nalazimika kukutana nanyi kutoa maelezo juu ya tuhuma zenye shinikizo la kisiasa zinazoelekezwa kwangu binafsi kwamba hata mimi nimeshiriki katika vitendo vya rushwa, kwa nafasi yangu kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma. Taarifa hizo, kama kawaida ya uzushi mwingine wowote zimesambazwa kimkakati na kwa kasi kubwa kiasi cha kuukanganya umma.
Nafahamu nabeba dhamana kubwa ya uongozi, taswira yangu ya uongozi daima imeakisi njozi na matumaini ya wananchi wa Kigoma Kaskazini, wananchi wanyonge na vijana kote nchini bila kujali itikadi zao za kisiasa, jinsia zao, makabila yao na rika zao. Hivyo, nawajibika kupitia kwenu kuwatoa hofu juu ya hisia potofu zinazopandikizwa kwao na wale wasiopenda kuona baadhi yetu tukiwaunganisha na kuwasemea watanzania wasio na sauti, dhidi ya vitendo vya hujuma na vyenye dhamira ovu kwa taifa.
Mkakati huo wa kuniunganisha na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wanaotuhumiwa kwa kupokea Rushwa unatekelezwa kwa njia zifuatazo:
- Kumekuwa na kauli za watendaji wa serikali ambao wamekuwa wakizieneza na hususan kutoa taswira kwamba baadhi ya kauli zangu zinatokana na ushawishi wa rushwa;
- Kuna taarifa ambazo zimeandikwa tena katika kurasa za mbele za baadhi ya vyombo vya habari zikidai ’’Zitto kitanzini’’ ama ’’Zitto sawa na popo nundu’’ zikiashiria kwamba na mimi ni mla rushwa; na
- Waandishi wa habari na jamii kwa ujumla wamefikia kuaminishwa habari hizi kiasi cha wengine kuuliza kwa nini Mhe. Zitto Kabwe hakutajwa katika orodha iliyotolewa na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani.
Ndugu Waandishi,
Naomba kutoa ufafanuzi wa hicho kinachoelezwa kwamba nina ushiriki katika masuala ya rushwa hususan kwenye masuala yanayohusu sekta ya Nishati na Madini:-
- Mara baada ya bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Usambazaji wa Umeme Tanzania (TANESCO) chini ya Uenyekiti wake Meja Jenerali Mstaafu Robert Mboma kutangaza kwamba imemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Nd. William Mhando ili kupisha uchunguzi wa baadhi ya vitendo/mwenendo wake, Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) ambayo mimi ni Mwenyekiti wake ilimuandikia Mhe. Spika kumuomba aridhie ili Kamati iweze kuwaita Bodi ya TANESCO, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali (CAG) na pia Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kujiridhisha na tuhuma zote zinazotajwa zinafanyiwa uchunguzi wa kina na hatua kuchukuliwa;
- Kamati ya POAC ninayoiongoza ilimuomba Mhe. Spika kuwaita wahusika tajwa kwa kuwa zilikuwapo tetesi kuwa kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi huyo siku chache kabla ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kulikuwa na lengo la kufunika ’madudu’ makubwa zaidi kwa kulichagiza Bunge na tukio hilo dogo, mkakati ambao naona umefanikiwa sana. Isitoshe, Kamati kutaka kujiridhisha na hatua za Bodi ni sehemu ya msingi ya utekelezaji wa majukumu ya Kamati yaliyowekwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge na pia Shirika la TANESCO ni moja kati ya mashirika ambayo yanawajibika kwetu kwa hesabu zake na pia ufanisi wake kwa ujumla. Tumefanya hivyo pia katika mashirika mengine, hili la TANESCO sio tukio la kipekee;
- Kitendo hiki cha halali na kwa mujibu wa Kanuni kilichofanywa na Kamati yangu kimetafsiriwa kwa makusudi na baadhi ya watu kwamba ni ishara ya kuwa sisi au zaidi kwamba mimi nina maslahi binafsi na TANESCO na hususan Mkurugenzi wake Injinia Mhando, ndio maana tumetaka maelezo ya Bodi. Ukweli kwamba Kamati ya POAC tumewaita pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu (CAG) na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa jambo hilo hilo umefichwa kwa makusudi!
- Baada ya tukio hilo, nikiwa hapa Dodoma, mwandishi wa habari wa gazeti moja alinifuata akiniambia kuwa wamekutana na Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake, Nd. Eliachim Maswi hapa hapa Bungeni na wamewaambia kuwa mimi nimepewa rushwa. Hakutaja nimepewa rushwa na nani, kiasi gani na wala kwa lengo gani!
- Nimejaribu kumtafuta kwa simu Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake ili wanipe ufafanuzi juu ya mimi na Kamati ya POAC kuhusishwa na tuhuma hizi bila mafanikio, hali ambayo inaniondolea mashaka juu ya ushiriki wao katika kueneza au kuthibitisha uvumi huo. Najaribu sana kujizuia kutokuwa na mashaka na ushiriki wao huo ikizingatiwa uzito na taswira ya nafasi zao katika jamii, lakini wameshindwa kunidhihirishia tofauti.
Sasa naomba kutoa ufafanuzi rasmi kuhusu mlolongo wa matukio hayo tajwa ambayo yanatumiwa na baadhi ya wanasiasa kuonesha kwamba eti nimehusika na vitendo vya rushwa.
- Binafsi sijawahi kuwa na mawasiliano ya aina yeyote na uongozi wa TANESCO kushawishiwa juu ya hatua ambazo POAC ndio imezichukua za kutaka kujiridhisha juu ya utaratibu uliotumika. Ieleweke wazi kabisa kuwa, hakuna wakati wowote, popote ambapo mimi binafsi au Kamati yetu imekataa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO kuchunguzwa kwa tuhuma zozote. Ambacho tumesisitiza wakati wote ni ufuatwaji wa taratibu, kanuni na sheria, hili nitalisimamia iwe masika au kiangazi;
- Ni kwa sababu hiyo, na kwa kujiamini kabisa nimeunga mkono suala la tuhuma za rushwa zinazotajwa zichunguzwe na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kina;
- Nimekwenda mbali zaidi kukiomba chama changu CHADEMA kifanye pia uchunguzi na tathmini yake kwa kina kujiridhisha na tuhuma hizo;
- Natumia fursa hii pia kuomba vyombo vya Dola vichunguze tuhuma hizo kwa nafasi yake ili kuweza kupata ukweli;
- Ninaahidi kushiriki kikamilifu iwapo nitatakiwa katika uchunguzi wowote utakaofanywa na niko tayari kuwajibika iwapo nitakutwa na hatia yeyote.
Napenda niwatoe hofu wananchi wa jimbo la Kigoma Kaskazini walionituma kuja kuwawakilisha hapa Bungeni na Watanzania wote kwa ujumla kwamba:-
- Mimi Zitto Zuberi Kabwe sina bei, sijawahi kuwa nayo na sitarajii kuwa nayo huko mbeleni. Daima nimesimamia kidete maadili ya uongozi bora katika maisha yangu yote ya siasa, na nawaahidi sitarudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa katika nchi hii pamoja na mikakati ya aina hii ya kunidhoofisha na kunivunja moyo;
- Nafarijika na salam mbali mbali zinazotolewa kunifariji na kusisitiza kuwa nisilegeze kamba katika mapambano haya, nimepokea ujumbe mwingi kwa simu, sms, tweeter na hata facebook na niko pamoja nanyi Watanzania wenzangu kamwe sitarudi nyuma hadi kieleweke. Naamini katika nchi yetu tunazo rasilimali za kutosha mahitaji/haja ya kila mmoja wetu lakini si ‘tamaa/ulafi’ wa baadhi ya watanzania wenzetu;
- Napenda kuweka rekodi sawa kwa Watanzania kwamba nimekuwa Mbunge hiki ni kipindi cha pili, Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) huu ni takriban mwaka wa saba sasa, Kamati yangu inasimamia mashirika 259 ya Umma na si TANESCO peke yake. Mchango wa Kamati hii katika Bunge na kwa ustawi wa Mashirika ya Umma ni bayana na haujawahi kutiliwa shaka. Kamati yetu imeokoa upotevu mkubwa wa mali za umma na kuokoa fedha za umma kutokana na umakini wake. Tumefanya hivyo CHC hivi karibuni, Kiwira na kwenye mashirika mengine mengi. Kote huko uadilifu na uzalendo wa Kamati hii haujawahi kuhojiwa. Inatuwia vigumu kuona kuwa tunahojiwa katika suala hili la TANESCO. Hapa pana kitendawili.
- Zipo hoja pandikizi za kutaka Kamati ya POAC ivunjwe na haswa zikinilenga mimi binafsi. Nafahamu kiu ya wasioitakia mema nchi yetu kuiona POAC ikivunjwa au sura zikibadilishwa kwa kuwa Kamati hii imekuwa mwiba kwa mikakati yao ya kifisadi. Kwa maoni yangu, Kamati ya POAC isihusishwe na tuhuma hizi kwa vyovyote vile. Niko tayari nihukumiwe mimi kama mimi na sio kuhusisha wajumbe wengine ambao hawatajwi mahala popote katika tuhuma hizi mbaya sana katika historia ya Bunge letu. Nitakuwa tayari kunusuru Kamati ya POAC na maslahi ya taifa letu kwa kujiuzulu Uenyekiti iwapo itathibitika pasipo shaka kuwa nimehongwa. Kamati ya POAC ni muhimu zaidi kuliko mimi.
- Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.
- Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa.
- Ni lazima tufike mahali kama viongozi kwamba utaratibu unapokiukwa na yeyote yule, au uongo unapotolewa hadharani tuseme bila kuogopa. Hili ndio jukumu letu kama wabunge na viongozi. Kusimamia ufuatiliaji wa utaratibu ni jukumu letu kama Kamati ya POAC na ndio sababu ya msingi ya kuanzishwa kwa mamlaka kama CAG na PPRA. Haiwezekani, tuwe na set ya kanuni kwa kundi fulani na nyingine kwa makundi mengine, au kuhukumu ufuataji wa taratibu kwa kuangalia sura ya mtu usoni
Mwisho
Kumejengeka tabia hivi sasa ya kuwamaliza wanasiasa wenye kudai uwajibikaji na uzalendo. Kumeanzishwa kiwanda kwenye medani ya siasa cha kuzalisha majungu na fitna zenye lengo la kuwachonganisha wanasiasa wa aina hiyo na wananchi kwa kutumia vyombo vya habari na nguvu ya fedha. Naamini mbinu hizi chafu, kama nyingine nyingi zilizojaribiwa kwangu huko nyuma nazo zitashindwa.
Naamini katika kweli na kweli daima huniweka huru. Naamini kuwa mwale mdogo wa mwanga wa mshumaa hufukuza kiza. Kwa imani hiyo, sitasalimu amri mbele ya dhamira zao ovu hata nitakapobaki peke yangu katika mapambano hayo ya kulinda na kutetea rasilimali za taifa zinufaishe watanzania wote.
Daima nitaongozwa na busara ya Hayati Shabaan Robert isemayo, ‘Msema kweli huchukiwa na marafiki zake, nitakapofikwa na ajali hiyo, sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga”.
Ahsanteni sana.
CHANZO: Zitto na Demokrasia
Subscribe to:
Posts (Atom)