Niliposikia mara ya kwanza nilidhani ni stori tu za mjini.Jana nimesikia tena,na safari hii ni kutoka kwa mwanafunzi aliyehitimu kidato cha sita hivi majuzi.Ishu yenyewe iko hivi:eti wanafunzi wa kidato cha sita waliletewa mashuleni fomu za kuomba udhamini wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu.Hadi hapo hakuna tatizo,Bodi inawajali wanafunzi hai inawaletea fomu shuleni.Mgogoro unaanzia kwenye taratibu za kurejesha fomu hizo ambapo kila mwanafunzi alipaswa kulipia shs 10,000/= ambazo ni non-refundable.Mgogoro zaidi ni ukweli kwamba zoezi zima la kujaza na kurejesha fomu hizo lilifanyika hata kabla wanafunzi hao hawajafahamu matokeo yao.Kwa maana hiyo,mwenye kufaulu na kufanikiwa kupata admission ya chuo anakuwa amenufaika lakini kwa aliyepata maksi zisizomruhusu kuendelea na masomo ndio ameliwa.This is what we call daylight robbery.Kwanini wasingechukua hiyo elfu 10 baada ya matokeo ili wale wasio na sifa wasiliwe fedha zao bure?Deadline ya kurejesha fomu hizo ilikuwa tarehe 30/04 na matokeo ndio yametoka majuzi.Sipendi kuona mikopo ya wanafunzi inageuzwa kuwa kama bahati nasibu flani,or to be more precise,ujambazi wa mchana kweupe.
Tuesday, 13 May 2008
Saturday, 10 May 2008
07:55
Unknown
MAKALA, RAIA MWEMA
No comments

Saturday, 3 May 2008
09:10
Unknown
DAR IN PICS
No comments
Hivi karibuni,eneo la Mlimani (UDSM) liligeuka Baghdad kwa muda kufuatia ghasia kubwa kati ya wanafunzi na vyombo vya dola.Hali sasa ni shwari,na majuzi walifanya uchaguzi wa viongozi wapya wa DARUSO japo inasemekana kwamba turnout ilikuwa ndogo sana.Ni kutokana na ushwari huo ndipo nami nilibahatika kuwatembelea wanazuoni flani hapo,na kufanikiwa kunyaka picha hii inayoonyesha eneo la Ubungo kama sijakosea,japo halionekani vema sana.
08:49
Unknown
DAR IN PICS
No comments
Miongoni mwa maeneo ya hapa jijini yanayotuwezesha kuendeleza libeneke la bloggin-japo nyakati nyingine kwa kusuasua-ni cafe moja iliyopo Millennium Tower.Kuna jamaa kanidokeza kuwa yeye huwa mwenyeji sana eneo hili kwa ajili ya kuangalia MIGONGO!Well,inawezekana alikuwa anazungumzia mgongo wa Twiga huyu,jirani na mwanga wa taa,ambaye ni kivutio mwanana!

06:19
Unknown
MAKALA, RAIA MWEMA, UFISADI
No comments

Wednesday, 23 April 2008
07:00
Unknown
CCM, MISS TANZANIA, RAIA MWEMA, TAZARA, UFISADI
1 comment

Pia kuna picha kadhaa kutoka maeneo mbalimbali ya Bongo.

Nadhani kuna wanaoikumbuka joint moja ya maeneo ya Namanga kuelekea Msasani iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Studi Becker.Sasa hivi inaitwa New Angel.Pengine kwa vile ni ya "Malaika Mpya" ndio maana toilets zao ziko kizani kama inavyoonekana (au isivyoonekana?) katika picha.

Picha hizi nzuri (hapo juu na zinazofuata chini) zimepigwa na dada mmoja mrembo wa Hoteli ya Kempinski (ameomba jina na sura yake vihifadhiwe) kutoka ghorofa ya sita ya hoteli hiyo.Dada huyo mdau wa blogu hii anadai amepatwa na wazo la kupiga na kunitumia picha hizo baada ya kuona kile "kimbembe cha zule" cha picha za matope ya barabara ya Ifakara.Picha zote zinaonyesha mandhari ya bandari ya Dar es Salaam,minus ufisadi wa Mamlaka ya Bandari na TICTS.



Tuesday, 22 April 2008
NINA LUNDO LA PICHA LAKINI LEO INTERNET IKO SLOW SANA.KEEP ON VISITING THE BLOG FOR MORE PICS.PICHA TATU ZA CHINI NI KUTOKA HOSPITALI YA MTAKATIFU FRANCIS IFAKARA (KUNA SANAMU YA MTAKATIFU HUYO KATIKA PICHA YA TATU).PICHA YA NNE NI MAHINDI YALIYOANIKWA KWENYE LAMI.SIJUI NDIO TEKNOLOJIA AU VIPI LAKINI THE IDEA IS SIMPLE:LAMI INAPATA JOTO UPESI NA KWA KUANIKA MAHINDI KWENYE LAMI BASI YANAKAUKA UPESI,NA MASUALA YA UGALI YANAWEZEKANA NDANI YA MUDA ULIOPANGWA.HIKI NI KIPINDI CHA MAVUNO,KWAHIYO NADHANI VIBAKA WA MAHINDI SIO WENGI.SIDHANI KAMA KATIKA KIPINDI CHA NJAA VIBAKA WATAYANUSURU MAHINDI YALIYOANIKWA BARABARANI.



Subscribe to:
Posts (Atom)