Soma mengine zaidi....
Saturday, 25 May 2013
Friday, 24 May 2013
10:04
Unknown
Matangazo
No comments
MKALI WA VODACOM:
Je, unajiamini kuwa na kitu kinachokufanya uwe mkali mtarajiwa? Vodacom inatafuta mtangazaji mpya wa kipindi cha TV kitakachoanza hivi karibuni. Soma namna ya kushiriki na unaweza kuwa mmoja ya watangazaji wa kipindi hiki.
Kazi ni kwako
Thursday, 23 May 2013
Wakati Rais Dokta Jakaya Kikwete Anasema Nchi Haijamshinda, Hii ndio hali halisi huko Mtwara (PICHA)







HEBU JIULIZE, LINI ULISHUHUDIA HALI KAMA HII IKITOKEA TANZANIA?
BADALA YA KUSAKA CHANZO, OUR DEAR LEADER DOKTA KIKWETE ANADAI "ATAKATA MAPEMBE" YA ANAYESABABISHA VURUGU. WELL, YEYE MWENYEWE NI PEMBE PIA KWANI UTAWALA WAKE UMEZIDI KUISUKUMA TANZANIA YETU KUELEKEA MAHALA KUSIKOFAA: UFISADI UMEKUWA KAMA SEHEMU YA MAISHA YA MTANZANIA, UDINI SIO TU UMEONGEZEKA BALI PIA UMEANZA KUWAFARAKANISHA WATANZANIA HUKU BAADHI YA WENZETU WAKIPOTEZA MAISHA YAO, UHUNI USIOELEZEKA MIONGONI MWA WATU WALIOCHAGULIWA NA KUPEWA DHAMANA YA KUWAKILISHA WATANZANIA (WABUNGE), MGAO WA UMEME USIOISHA LICHA YA AHADI KEDEKEDE KUTOKA KWA KIKWETE...MENGINE ONGEZEA MWENYEWE MSOMAJI.
NASEMA HIVI, IFIKE MAHALA KIKWETE AAMBIWE UKWELI KUWA KAMA KWELI ANA LENGO LA KUKATA PEMBE BASI AJIWEKE KANDO YEYE MWENYEWE KWANI YEYE NDIYE PEMBE KUBWA ZAIDI.
Tuesday, 21 May 2013
09:40
Unknown
CHADEMA, PROFESA JAY
No comments
Profesa Jay akipokea kadi ya unachama wa Chadema kutoka kwa Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) Mh. Joseph Mbilinyi (a.k.a Sugu)
Profesa Jay akiwa na Mh 'Sugu' na Mbunge wa Ubungo (Chadema) Mh John Mnyika.
Ni Mtanzania gani kijana (na hata wazee wa kati) asiyemjua Profesa Jay, msanii mahiri wa Bongoflava ambaye jina lake halisi ni Joseph Haule (au Jay wa Mitulinga). Msanii huyo, pengine katika hali ambayo haikutarajiwa kabisa, leo amejiunga na chama cha upinzani cha Chadema.
Uamuzi wa Profesa Jay kujiunga na Chadema unaweza kuwa na manufaa makubwa sana kwa chama hicho hasa kwa vile mabadiliko ya kisiasa huko nyumbani yanategemea zaidi hamasa ya vijana.
Nitaandika zaidi baadaye kuhusu tukio hili muhimu kwa Chadema, muziki wa bongoflava na vijana kwa ujumla, lakini kwa sasa burudika na kibao hiki cha "Nikusaidiaje" cha Profesa Jay akimshirikisha Ferouz
Friday, 17 May 2013
Popote ulipo,ktk nafasi yoyote uliyonayo, tafadhali msaidie mwananchi huyu anayenyanyaswa pasi hatia
Tumekuwa wepesi wa kulaumu zaidi kuliko kutenda. Sote twatambua uonevu unaofanywa na baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola hususan Jeshi la Polisi. Lakini kulaumu au kulaani pekee hakuwezi kumaliza tatizo husika, hususan katika nyakati ambazo kuna wenzetu wanateswa pasi hatia. Basi ombi langu kwako ni kutumia nafasi yako-iwe ni mtu maarufu, mfanyabiashara, mwanasiasa, nk-kumsaidia mwananchi huyu.Mie nimeanza kwa kuweka hadharani kilio chake.
Subscribe to:
Posts (Atom)