Showing posts with label CYBER WAR. Show all posts
Showing posts with label CYBER WAR. Show all posts

Thursday, 26 August 2010

Inaelezwa kuwa vita vya mtandao (cyber war) ni tishio kubwa kwa Marekani kama ilivyo ugaidi.Na katika kujipanga vema kupambana na maadui wa nchi hiyo wanauweza kutumia mtandao kufanya mashambuli,Makao Makuu ya "Wizara" ya Ulinzi,Pentagon,imeanzisha mkakati wa kuajiri vijana wadogo wenye kipaji cha hali ya juu katika kuhujumu mtandao na kuufanya utekeleze matakwa ya mhujumu husika (hacking).


Katika kufanikisha zoezi hilo la kupata makuruta mwafaka,Pentagon ilisimamia shindano la uhujumu huo wa mtandao ambapo hackers vijana kadhaa walishiriki.Kichekesho ni kwamba katika kuonyesha uhodari wake katika fani hiyo,mmoj wa hackers hao alifanikiwa kuhujumu alama alizopewa na wasimamizi wa shindano hilo kabla matokeo hayajatangazwa.

Habari hii imenikumbusha kauli ya mwalimu wangu mmoja pale Mlimani,Profesa Ngware,aliyetupa "ukweli mchungu" kwamba "hivi kama wakati watoto wenu wanachezea vifuu ilhali wanangu wanacheza na kompyuta,mnatarajia watapokuwa wakubwa watakuwa na uwezo sawa wa akili?"


Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget