Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts
Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts

Monday, 13 June 2011

Window on the world: Gone are the small aircraft windows in the 'vitalising zone' which provides a panoramic view for passengers

Pichani juu ni muundo wa ndege za kizazi kijacho ambazo badala ya vijidirisha vidogo tulivyovizowea,ndege hizo zitakuwa transparent.Hiyo inamaanisha abiria wataweza kuona ndege inavyopasua anga...na hapo ndio shughuli kwa waoga wa vina.

Hata hivyo,kama wewe ni miongoni mwa waoga hao,basi usihofu sana kwani inatarajiwa kuwa ndege za aina hiyo zitaanza kazi miaka 40 ijayo.

CHANZO (NA KWA HABARI KAMILI): Daily Mail

Monday, 19 April 2010

Ni dhahiri unapokutana na kitangulizi 'http://...' unafikiri kuwa kinachofuata ni anuani ya tovuti flani.Lakini je 'http://' (kifupisho cha Hypertext Transfer Protocal)bado ina umuhimu katika mazingira ya sasa ambapo unaweza kuitambua anuani ya tovuti hata bila kitangulizi hicho? . 
Wanateknolojia wa Google Chrome hawadhani kama kitangulizi hicho bado ni muhimu na wameamua kukificha katika toleo jipya la browser hiyo.

Hata hivyo,ufumbuzi huo sio rahisi kama inavyoonekana kwani unaweza kuficha kitangulizi hicho unapoandika anuani ya tovuti lakini bado kipo.Pia inatarajiwa kuwa maendeleo hayo yanaweza kuzua mkanganyiko kwa baadhi ya watumiaji wa intaneti.

Makala hii imetafsiriwa (katika tafsiri isiyo rasmi) kutoka mtandao wa Mashable

Wednesday, 23 January 2008

Alfajiri hii nimepata barua-pepe kutoka kwa mtu mmoja anayeelekea kuumia moyo kwa namna navyoshutumu ufisadi na mafisadi.Mzembe huyo ametoa shutuma lukuki kuhusu makala zangu magazetini na humu "bloguni" kuhusiana na suala la ufisadi.Kwa kutompa ujiko aliokuwa anatafuta,nimeamua kupuuza barua-pepe hiyo na sikumjibu.Binafsi,nilikuwa natambua bayana kwamba mafisadi wameshabaini kwamba mtandao una nguvu pengine zaidi ya magazeti yetu huko nyumbani,hasa ikizingatiwa kwamba ni machache tu yaliyopo kwenye mtandao.Mapepe aliyeniandikia barua-pepe amejitahidi kadri ya uwezo wake mdogo alionao kuni-discourage kuandika chochote dhidi ya mafisadi,huku akidai kwamba sie tulio ughaibuni tuna tabia ya kujifanya tunajua kila kitu (cha ajabu ni kwamba naye anadai yuko ughaibuni,tena hapahapa Uingereza).

Sitaki kuifanya case yangu kuwa universal lakini naamini kwamba teknolojia ya habari kupitia mtandao imetokea kuwa silaha kubwa dhidi ya wanyonge na wakati huohuo ikiwa mwiba mkali dhidi ya ufisadi na mafisadi.Kuna watakaopambana nasi tunaopigia kelele ufisadi kwa vile wao ni vibaraka wa mafisadi na wengine watasigishana nasi kwa vile wao wenyewe ni mafisadi.Wito wangu kwa wale wote ambao kwa namna moja au nyingine wameamua kusimama kidete kupigania haki na usawa kwa kila Mtanzania,Mwafrika na raia wengine wa dunia wanaonaoporwa stahili zao,ni huu:kila kelele ya fisadi itafsiriwe kama full tank za mafuta ya mtambo wa kukabiliana na maovu kwenye jamii.

Kwa fisadi "wangu" Mapepe,pokea zawadi hii kutoka kwa Ludacris kwenye clip ya Get Back (Caution: explicit lyrics)


Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget