Kibonzo kwa hisani ya FEDE
Saturday, 4 September 2010
Tunafahamu kuwa mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,ni mahiri sana katika kutoa ahadi.Wakati wa kampeni zake za kuwania urais kwa mara ya kwanza mwaka 2005 alitoa rundo la ahadi ambazo hata angekuwa na uwezo wa kutekeleza basi ingebidi awe rais wa milele.Kwa makusudi,badala ya kufanya marejeo ya ahadi zake lukuki za 2005,Kikwete ameendelea kutoa ahadi zaidi akijaribu kuwaghilibu Watanzania kuwa safari hii akipewa madaraka atazitekeleza.Swali la msingi ni kipi kilichomzuia kuzitekeleza katika kipindi hiki (2005-2010) na kipi kitamwezesha kutekeleza ahadi hizo katika awamu ijayo (2010-2015).
Alipokuwa kwenye kampeni zake huko mikoani aliahidi (bila aibu) kuwa tatizo la umeme sasa litakuwa historia.Last time aliposema hayo,walikuja matapeli wa Richmond.Sijui safari hii watakuja wasanii gani "kuvuna wasichopanda".Angekuwa na busara,angewaeleza Watanzania kwanini umeme umeendelea kuwa tatizo sugu nchini.Ufumbuzi wa tatizo hilo hauwezi kupatikana kwa ahadi zaidi ya zilizokwishatolewa.Kikwazo kikubwa katika upatikanaji wa ufumbuzi wa tatizo la umeme ni maslahi binafsi na ufisadi.Kuna watu wanaoombea Tanzania iwe kizani kila siku ili wauze jenereta zao.Kuna wengine wanaotaka umeme uendelee kuwa tatizo ili wapate fursa ya kutengeneza dili za kifisadi kama za IPTL,Richmond na Dowans.Na Kikwete anawajua sana watu hao lakini hana nia wa kuwachukulia hatua.Ikumbukwe kabla ya kuukwaa urais,Kikwete alishawahi kuwa Waziri wa Nishati!!!
Kadhalika,katika mwendelezo wa ahadi,Kikwete ameahidi kuleta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la maji jijini Dar es Salaam.Utadhani kwamba tatizo hilo halikuwepo wakati wa utawala wake,au limeanza majuzi.Na kama hiyo haijatosha,akaahidi tena kuwa daraja la Kigamboni litajengwa kwa vile zabuni ya kumpata mkandarasi imeshakamilika.Kwanini iwe baada ya kumchangua tena na sio alipochaguliwa 2005?Haihitaji hata elimu ya chekechea kutambua kuwa ahadi hizi ni hewa.ZITAENDELEA KUWA AHADI TU.
Ukimsikiliza kwa makini utagundua kuwa Kikwete hayuko serious na anachoongea.Pengine ni kwa vile anafahamu kuwa hahitaji kuwa serious kupata tena nafasi ya urais.Pengine ni tatixo la upeo tu.Hata hivyo,kumlaumu JK ni kumwonea kwa vile kama ilivyokuwa Desemba 2005,come Oktoba this year HATAJICHAGUA MWENYEWE KUWA RAIS BALI ATATEGEMEA KURA ZA WATANZANIA.Mwaka 2005 waliompigia kura na kumpa ushindi wa kishindo wanaweza kuwa na excuse kwa kudai walikuwa HAWAMJUI VEMA.Five years later,naamini kila Mtanzania anafahamu udhaifu wa kiongozi huyu.Kumrejesha tena Ikulu kwa miaka mingine mitano ni kosa ambalo litawagharimu sana Watanzania.
Ikumbukwe kuwa kama atarejea tena madarakani,kuna uwezekano mkubwa wa kuendesha nchi kwa mtindo wa BORA LIENDE kwa vile hiyo itakuwa awamu yake ya mwisho kwa mujibu wa Katiba.Kama ameweza kuwapuuza Watanzania katika kipindi hiki cha miaka mitano inayoisha huku akielewa fika kuwa itambidi awabembeleze tena wampigie kura mwaka huu,kwanini basi asiwapuuze zaidi kwa vile hatagombea tena urais hapo 2015?
Ni muhimu kwa Watanzania kutambua kuwa tusipoziba ufa tutajenga ukuta.Ufa wetu kwa sasa ni Kikwete na CCM yake.Tukiwarejesha tena madarakani hapo Oktoba tutakuwa tumejichimbia kaburi refu.Tuweke kando ushabiki wa vyama vya siasa na tuangalie maisha yetu na hatma ya taifa letu.Tusifanye mzaha kwa kuendekeza kauli "JINI LIKUJUALO HALIKULI LIKAKWISHA" (i.e. Bora Kikwete na CCM kwa vile tunawajua kuliko hao akina Dkt Slaa na Chadema tusiowajua).Problem is,jini hili safari hii litatumaliza na kutukomba kila kitu.Wameiba mabilioni ya EPA,wametutapeli na Richmond,Dowans,IPTL,Kiwira,Meremeta,Tangold,nk na hawajatosheka.Tukiwarejesha tena madarakani watatukomba kila kitu.
Bahati nzuri Mungu si Athumani.Ametuonea huruma na kumwibua mkombozi Dokta Wilbroad Slaa.Hii ni nafasi adimu,na ndio maana nguvu za giza zimekuwa zikimwandama.CCM wanajua bayana kuwa Dkt Slaa ana dhamira ya dhati kuwatumikia Watanzania.Hawampingi kwa vile ni mwanasiasa wa upinzani bali wanahofia atawafungua macho waliolala,na pia atawapora mtaji wao- yaani masikini wanaonunuliwa kwa pishi za mchele na sukari huku wakiahidi maisha bora "hewa".
Kama wewe si fisadi basi unapaswa kuwa na NIA,SABABU na UWEZO wa kumtosa JK na CCM yake hapo Oktoba.Maisha Bora ya Kweli (na sio ya kuzugana) Yanawezeka,Ila tu sio kwa wazushi hawa waliopo madarakani bali kupitia kwa Dokta Slaa na CHADEMA.
Kwa mujibu wa blogu ya Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua (mwanahabari mahiri Ansbert Ngurumo),Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa alionekana Ikulu siku ya Alhamisi majira ya saa 9 alasiri ambapo inaelezwa alikutana na Rais Jakaya Kikwete,mgombea wa CCM ambaye amelalamikiwa na Chadema kwa kukiuka Sheria y Gharama za Uchaguzi.Awali,Tendwa alisema kuwa angetoa "hukumu" keshokutwa (Jumatatu).
Kwa hakika,haihitaji utaalam wowote kuhusisha tukio hilo (la Tendwa kukutana na Kikwete) na pingamiz la Chadema.Na haihitaji ujuzi wa sheria kubashiri matokeo ya "hakimu kukutana faragha na mshtakiwa" siku chache kabla ya hukumu.
Wengi wetu tunafahamu Tendwa atasema nini hiyo Jumatatu.Most likely,ameshafanya maamuzi ila kinachoshughulikiwa sasa ni usanii wa lugha ya utoaji wa maamuzi hayo.Na ni katika hilo ndio maana inamlazimu awasiliane na JK ili "ajenge mazingira ya hukumu ya haki".Katika mazingira tuliyonayo ambapo Msajili wa vyama vya siasa ni kama kibaraka wa CCM,haiwezekani kabisa kiongozi huyo kutoa maamuzi ya haki yatakayokiathiri chama hicho.
Na dalili za "usanii" zimeonekana tangu Chadema wawasilishe malalamiko yao.Hivi Tendwa anaweza kuwaambia Watanzania kwanini imchukue takriban wiki nzima kutoa maamuzi kuhusu malalamiko ya Chadema?Je hiyo pekee sio dalili ya uzembe na kutowajibika ipasavyo?Awali aliwaeleza waandishi wa habari kuwa angetoa maamuzi Jumatatu lakini hakueleza kwanini itachukua muda wote huo kutoa maamuzi hayo muhimu kwa mustakabali wa demokrasia nchini mwetu.Jibu jepesi ni kwamba hana ubavu wa kutoa maamuzi kabla ya kupata ridhaa ya CCM.Na kwa vile CCM ndio watuhumiwa,ni dhahiri maamuzi ya Tendwa yataelemea kuipendelea CCM.
Nafahamu kuna wataosema "aah,sasa kelele za nini wakati maamuzi hayajatolewa?" Wana haki ya kusema hivyo lakini wanapaswa pia kutambua vema mapungufu ya Katiba yetu yanayomfanya mgombea wa chama tawala kuwa na advantage kubwa dhidi ya wagombea wengine kutokana na ukweli kwamba Katiba inampa rais nguvu kubwa mno.
Kikwete ameendelea kupuuza malalamiko ya Chadema kwa kuzidi kutoa rushwa ya ahadi katika mikutano yake ya kampeni.Sote tumemsikia akiwazuga wapigakura huko Mbagala kuhusu daraja la Kigamboni na ahadi nyingine hewa ya huduma ya uhakika kwa maji jijini Dar es Salaam.Huyu mtu hana aibu kwa sababu ahadi anazotoa sasa zinatoa picha ya mgombea anayeomba idhini ya kuingia madarakani kwa mara ya kwanza na sio aliyekuwa rais wetu kwa miaka mitano iliyopita.Kama tangu 2005 hadi leo ameshindwa kuwezesha ujenzi wa daraja hilo la Kigamboni,kwanini tumwamini kuwa ataweza katika mhula wake wa mwisho (2010-2015) hasa ikizingatiwa kuwa kipindi hicho cha pili kitatumika zaidi kwa yeye kujitengenezea mazingira ya "kustaafu kwa amani"?
Jeuri ya Kikwete inasababishwa na ufahamu kuwa Chadema,na vyama vingine vya upinzani,havina mahala pa kukimbilia pindi wasiporidhishwa na mwenendo wa kampeni za Kikwete na CCM kwa ujumla.Anafahamu kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa,Mahakama na taasisi nyingine za kusimamia uchaguzi na sheria nza nchi kwa ujumla,ziko mikononi mwa CCM.Hata hivyo,wapinzani hawapaswi kukata tamaa kwa vile nchi yetu kama masikini wa kutupwa inategemea sana misaada ya wafadhili.Japo kuwapigia magoti wafadhili kunaweza kutafsiriwa kama "kuegemea kwenye ukoloni" lakini tufanyeje kama nchi yetu inaendeshwa kiholela.Binafsi,nina matumaini makubwa kuwa nchi wafadhili zinafuatilia kwa karibu mwenendo wa kampeni za vyama vya siasa nchini na hazitasita kuchukua hatua mwafaka pale CCM itakapotumia ubabe wake kulazimisha ushindi.
Hata hivyo,wakati we keep on hoping for the best and expecting the worst,Tendwa afahamu kuwa he wont get away with this issue as easily as he might think.Blogu hii inaamini kuwa Chadema ni chama makini na chenye rekodi nzuri ya ufuatiliaji mambo.Ni katika mantiki hiyo basi blogu hii inatarajia kuwa Chadema hawatamruhusu Tendwa kufanya uhuni wa aina yoyote ile katika maamuzi yake.Ni heri uchaguzi uvurugike lakini haki ipatikane.Kutoa fursa ya sheria za nchi kupindishwa kwa namna watawala wanavyotaka ni hatari sana hasa tukizingatia ulevi wa madaraka unaowakabili viongozi wengi wa "dunia ya tatu".
Kama alivyoandika Ngurumo katika blogu yake,nami narejea kumkumbusha Tendwa kuwa HATUDANGANYIKI!
Friday, 3 September 2010
14:47
Unknown
YUSUPH MAKAMBA
1 comment
Wenye busara zao wanatuusia kuwa pindi ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo then sio wazo jema ku-entertain kurusha mawe.Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una ishu zenye utata katika maisha yako then sio wazo jema kuanza kushupalia ishu za watu wengi lest flani akakugeuzia kibao.
Lakini usemi huo umeonekana hauna maana kwa Katibu Mkuu wa CCM,Yusuph Makamba,ambaye kwa siku kadhaa sasa ameamua "kuvalia njuga maisha binafsi ya Dokta Wilbroad Slaa" na kuligeuza suala la ndoa ya mgombea huyo wa Chadema kuwa ajenda ya uchaguzi.
Pengine ni dharau au ujinga,Makamba alijisahau kuwa wakati anamnyooshea kidole Dkt Slaa,yeye mwenyewe (Makamba) alikuwa na doa linaloweza kabisa kumpeleka jela.Kwa mujibu wa taarifa zilizozagaa mtandaoni,Makamba anatuhumiwa kumbaka mwanafunzi wakati akiwa mwalimu mkuu wa shule moja na hatimaye kufukuzwa ualimu.
Hizi ni tuhuma nzito sana kwani licha ya kumtia doa Makamba kama mwanasiasa,ni suala linaloweza kumpeleka jela endapo victim wake atajitokeza hadharani,na kupatiwa msaada wa kisheria.Lakini tukiweka ishu za kisiasa kando,hapa kuna suala la binti asiye na hatia ambaye inadaiwa alibakwa na mtu aliyekabidhiwa dhamana ya kumpatia elimu na mwongozo katika maisha yake,mwalimu wake,lakini akaishi kubakwa.
Blogu hii inatoa ombi maalum kwa yeyote yule anayeweza kuipatia taarifa za uhakika kuhusu binti huyo anayedaiwa kubakwa na Makamba.Lengo si kumkomoa mtuhumiwa bali kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake as well as kutoa reminder kwa watu wengine wanaotumia vibaya dhamana walizokabidhiwa,iwe mashuleni,makazini au hata katika ngazi ya familia.
Je unamfahamu binti anayedaiwa kubakwa na Makamba?Kama jibu ni ndiyo basi tafadhali sana tuwasiliane kwa barua pepe kwa anuani hii epgc2@yahoo.co.uk.
Subscribe to:
Posts (Atom)