Saturday, 11 December 2010



WAKATI biashara ya magogo ikiendelea kutikisa vichwa vya viongozi wa serikali, imebainika kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, kada wa CCM, wakuu wa polisi na maafisa wa Takukuru ndio wanaomiliki vibali vya kuvuna magogo katika msitu wa serikali wa Sao Hill ulio wilayani Mufindi.Biashara ya magogo ambayo ilishamiri mwaka 2005/06 ilipigwa marufu baada ya kuonekana kasoro kwa wasafirishaji magogo nje ya nchi ambao walionekana kukiuka masharti ya leseni zao na wiki iliyopita Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alisema marufuku hiyo inaendelea kwa kuwa ni kinyume cha sheria za nchi.
Lakini msimamo huo wa Waziri Maige utakuwa mgumu kuutekeleza baada ya Mwananchi kubaini kuwa wanaomiliki vibali vya kuvuna magogo ni baadhi ya viongozi wa serikali ambao badala ya kuvitumia kwa malengo waliyoombea, wamekuwa wakivikodisha kwa wafanyabiashara.

Baadhi ya vigogo mbao majina ambayo yamo kwenye orodha watu wanaomiliki vibali hivyo ni pamoja na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyril Chami, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera, Uratibu na Bunge-, William Likuvi, mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Evalista Kalalu, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita na wengine waliotumia majina ya jamaa zao.

Wengine ni Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene na kampuni ya Rombo Green View inayomilikiwa na mmoja wa mawaziri wa zamani katika serikali za awamu tofauti. Katika orodha hiyo pia yamo majina ambayo ubini wake unafanana na baadhi ya viongozi kama vile Selemani KIKWETE, Aneth P. Msekwa na Juma Abdallah Zombe.

Hata hivyo, haikufahamika mara moja kama watu hao wana uhusiano wa moja kwa moja na watu ambao majina yao ya ubini yanafanana na ya viongozi wa serikali.Vyanzo vyetu vya habari vimebainisha kuwa vigogo walioficha majina yao wanafahamika na kwamba itakapohitajika watatajwa hadharani na raia wema walioapa kuwa tayari kufanya hivyo.
Habari za kiuchunguzi zimebaini kuwa kuwepo kwa watumishi hao wa serikali katika biashara ya magogo kumezua mgogoro mkubwa wa kimaslahi kati yao na wavunaji wadogo wanaolalamika kupunjwa kwenye mgao wa vitalu vya uvunaji.

Uchunguzi umebaini kuwa mgao wa kitaifa unaelekeza meneja mradi wa Sao Hill kugawa magogo yasiyozidi mita za ujazo (cubic metre) milioni moja kwa mwaka.Hata hivyo, katika hali inayoweka mashaka, mgao huo unaonekana kuwapendelea zaidi vigogo hao wanaotumia nyadhifa zao kupata vibali bila kuwa na sifa za kupata mgao huo, huku wengine wanaonufaika wakitajwa kuwa ni baadhi ya wawekezaji wakubwa.Imeelezwa kuwa masharti yaliyowekwa na serikali kwa kila kibali ni kwamba lazima muombaji awe na vifaa kama malori makubwa ya kukokota magogo (break down), mashine zenye uwezo mkubwa wa kuchana magogo na lazima muomba kibali awe ameajiri wataalamu toka chuo cha misitu kinachotambuliwa na serikali, masharti ambayo Mwananchi imedokezwa kuwa hayajatekelezwa na vigogo hao.

Katika kipindi ambacho Rais Jakaya Kikwete amewataka mawaziri na wasaidizi wao kuwa tayari kutoa habari kwa wananchi, katibu mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk Ladslaus Komba hakuweza kuzungumzia suala hilo kila mara Mwananchi ilipowasiliana naye kuanzia Jumatano iliyopita.Badala yake, katika simu zote sita alizopigiwa kati ya Jumatano na jana jioni, Dk Komba alipokea lakini baada ya mwandishi kujitambulisha na kueleza kile anachotaka kufahamu kutoka kwake, alijibu:
"Kwa sasa niko kwenye kikao nitakutafuta baadaye.Hata hivyo, hakutekeleza ahadi hiyo hata mara moja.

Katika moja ya simu hizo, Dk Komba alisema: “Kuna kitu hapa nakinukuu, naomba unipe muda nitakujulisha.”
Hata hivyo alipotafutwa baadaye simu yake ilikuwa haipatikani.
Hata alipofuatwa ofisini kwake, katibu muhtasi wake alieleza kuwa Dk Komba alikuwa ameenda kikazi nje ya ofisi na kumtaka mwandishi amsubiri.

Mmoja wa vigogo waliotajwa kwenye orodha ya mgao wa magogo, WaziriLukuvi alikiri kupokea mgao huo, lakini akasema aliomba kwa ajili ya ujenzi wa shule za sekondari zilizo jimboni kwake Isimani na si kwa nia ya biashara.

Kwenye mgao huo, Lukuvi amepewa kibali cha kuvuna magogo yenye mita za ujazo 1,000, kulingana na orodha iliyobandikwa kwenye ubao wa matangazo wa Sao Hill Mufindi. Katika  orodha hiyo Lukuvi ni mtu wa 564.
“Ni kweli niliomba na nikapewa kibali cha kuvuna magogo. Lakini, si kwa nia ya biashara bali kwa ajili ya kupata mbao za ujenzi wa sekonda zilizopo jimboni kwangu, ikiwemo ile iliyoungua moto ya Idodi,” alisema.

Mbunge wa jimbo la Kibakwe, George Simbachawene alipoulizwa kuhusu suala hilo alikiri kuomba mgao wa uvunaji magogo katika msitu huo, lakini akasema lengo lake si kwa ajili ya kufanya biashara bali ni ujenzi wa madarasa.
"Ni kweli niliomba wala sibishi, lakini si kwa ajili ya kufanya biashara. Ilikuwa ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya shule zetu zilizo katika halmasahauri yetu, kwa sababu kununua mbao zikiwa zimeshaandaliwa ni gharama kuliko kuomba kuvuna magogo na kuchana mwenyewe," alisema Simbachawene.

Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni jitihada za kumpata Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyril Chami na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita zilishindikana.

Taarifa zinasema kuwa licha ya kujipatia vibali vinavyotolewa bure na Wizara ya Maliasili na Utalii, wamekuwa hawavitumii kwa uvunaji bali huvikodisha kwa wavunaji wadogo kwa gharama ya Sh5 milioni hadi Sh7 milioni kwa kibali kimoja huku ikielezwa kuwa wapo wanaomiliki vibali zaidi ya 10 na wanavitumia kwa majina tofauti.
Hali hiyo imefanya wavunaji wadogo kupunjwa mgao wa uvunaji magogo tofauti na ilivyokuwa kabla ya watumishi hao wa umma na vigogo kuvamia sekta hiyo.

Hivi sasa wavunaji wadogo zaidi ya 400 wanaambulia mgao kiduchu na wengine kukosa kabisa, hivyo wengi wamelazimika kufunga viwanda vyao kutokana na kukosa malighafi.
“Kama watoa vibali ndio wahusika katika biashara hii je, haki itatendeka kwa wavunaji wadogo?,” kilihoji chanzo kimoja.

Thursday, 9 December 2010



JAMAA mmoja ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Joseph, leo asubuhi alikutwa na kamera yetu akiwa ameanguka katika Barabara ya Forest mjini Morogoro, pembezoni mwa uzio wa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Morogoro, akidai kwamba alikuwa ametokea katika hospitali hiyo na kwamba hali yake ilikuwa imezidi kuwa mbaya.

Akizungumza na mtandao huu, Joseph alisema: "Nimetoka humu ndani (hospitali) kutibiwa na baada ya kupewa dawa niliruhusiwa kurudi nyumbani, nilipofika hapa nimezidiwa na njaa pamoja na ukali wa dawa hizo na kujikuta nikiishiwa nguvu na kuanguka.

Kama kuna mtu ana shilingi elfu moja anisaidie nikanunue walau uji," alisema Joseph huku akionekana akitetemeka kwa njaa pamoja na ukali wa dawa hizo.



Alipoulizwa anasumbuliwa na ugonjwa gani alidai ni homa ya matumbo (typhoid) iliyoambatana na homa kali.

Mwandishi wetu alimpatia kiasi hicho cha fedha ambapo pia baadhi ya watu waliokuwa eneo hilo walimuunga mkono mpiga picha wetu kwa kumuongezea kiasi cha fedha na baadaye kumwinua hadi kwenye mgahawa uliopo jirani na Shule ya Sekondari ya Morogoro.

Baada ya kupata hudumu hizo, Joseph alizinduka na kauli yake ya kwanza ilikuwa ni kuushukuru mtandao huu na wananchi wengine kwa kumpatia msaada huo.

Picha na Habari kwa Hisani ya Global Publishers



WAKATI HALI IKIWA HIVYO KWA MLALAHOI HUYU,GAZETI LA Mwananchi LILIRIPOTI HABARI IFUATAYO.ISOME KISHA ULINGANISHE NA HABARI HIYO YA KUSIKITISHA HAPO JUU,KISHA TAFAKARI KUHUSU MIAKA 49 YA UHURU WETU

Mashangingi ya mawaziri yazua utata 
Sunday, 28 November 2010 21:05

Sadick Mtulya

WAKATI mawaziri na manaibu wawaziri wakikabidhiwa magari mapya, baada ya kuapishwa Jumamosi iliyopita, serikali imeibuka na kusema sio mapya ni ya zamani.Kauli hiyo inaibua utata kutokana na kuwa baada ya kuapishwa viwanja vya Ikulu na Rais Jakaya Kikwete, kila waziri alikabidhiwa dereva mpya na gari jipya aina ya Toyota GX V8, badala ya gari aina ya Toyota VX V8 iliyokuwa ikitumiwa na mawaziri waliopita.

Ununuzi wa Toyota GX V8 mpya, unashiria serikali bado haijawa tayari kuunga mkono msimamo wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambaye amekuwa akisikika akitaka kusitishwa ununuzi wa magari ya kifahari ili kupunguza matumizi ndani ya serikali.

Toyota GX V8 moja huuzwa kati ya Sh210 milioni hadi Sh240 milioni, hukuToyota VX V8 moja inauzwa sio chini ya Sh180 milioni.Akizungumza na Mwananchi jana, Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara ya Miundombinu, Omari Chambo, alisema magari hayo sio mapya na kwamba, yaliyotumiwa na mawaziri waliopita.Rais Jakaya Kikwete ameigawanya iliyokuwa Wizara ya Miundombinu na kuwa wizara mbili; Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Uchukuzi.

“Yale magari sio mapya, yalikuwepo. Kwanza uliyaona au unasema tu, hamjayachunguza vizuri jamani, fanyeni uchunguzi,’’ alisema Chambo na kukata simu.
Mawaziri wote na baadhi ya manaibu walikabidhiwa magari hayo (GX V8), huku manaibu wengine wakikabidhiwa VX V8.Sababu ya baadhi ya manaibu mawaziri kukabidhiwa VX V8 badala ya GX V8, ni kutokana na kutokamilishwa kwa taratibu za kutokamilika.

Mmoja wa manaibu mawaziri (jina tunalo), alikabidhiwa VX V8 iliyokuwa ikitumiwa na aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifungo na Uvuvi, John Magufuli, ambaye sasa ni Waziri wa Ujenzi.Gazeti moja la kila siku (si Mwananchi) limeeleza kuwa ununuzi wa magari hayo, umegharimu serikali Sh9.3 bilioni na kwamba, takwimu za iliyokuwa Wizara ya Miundombinu zinaonyesha kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka wa fedha wa 2005/06 magari makubwa ya kifahari yapatayo 6,000 yalikuwa yamenunuliwa na serikali kwa gharama inayokadiriwa kufikia Sh160 bilioni.

Miongoni mwa magari hayo ni Toyota Land Cruiser (VX/ GX V8, Prado) yapatayo 1,655, Nissan Patrol na Land Cruiser 885, Mitsubishi Pajero 400 na mengineyo.

Tangu kipindi cha serikali ya awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, kumekuwepo na mjadala kuhusu matumizi makubwa ya serikali hasa katika ununuzi wa magari ya kifahari kutokana na kuendeshwa kwa gharama kubwa.Wadau wengi wanataka viongozi watumie magari ya kawaida kama ilivyo kwa nchi ya Kenya na Rwanda


Wednesday, 8 December 2010



Leo ni siku yangu ya kuzaliwa.Kwanza sina budi kumshukuru Muumba kwa kunileta duniani tarehe 9 Desemba miaka thelathini na kitu iliyopita (30 plus yrs ago).Pili,nawashukuru wazazi wangu wapendwa,Baba Mzee Philemon Chahali na Mama mpendwa Marehemu Adelina Mapango (Mungu Akulaze Mahali Pema Peponi Amen).Tatu,nawashukuru wanafamilia wenzangu katika familia yetu-kaka na dada na wadogo zangu.Na nne nawashukuru wale woote nilio/ninaofahamiana nao katika muda wote huo.

Makala hii sio kwa ajili ya kuzungumzia birthday yangu.Kwa bahati nzuri (au mbaya?) tarehe ya siku yangu ya kuzaliwa inarandana na tarehe ya Uhuru wa Tanzania.Inapendeza kusherehekea siku ya kuzaliwa inayoambatana na tukio jingine muhimu la kihistoria.Lakini historia pekee sio muhimu kama haina manufaa stahili kwa jamii husika.

Wakati tunaadhimisha miaka 49 ya uhuru wa Tanzania tunalazimika kujiuliza mara mbili mbili umuhimu wa uhuru huo.Je uhuru wetu uliishia tu kwenye kumwondoa mkoloni au ulipaswa kutuweka huru katika nyanja zote?Naamini hilo la pili ndilo dhamini na maana halisi ya uhuru: uhuru wa kupata huduma tunazostahili (elimu,afya,maji,barabara,umeme,maji,nk),uhuru wa kuchagua na kukataa viongozi kwa njia halali (sio uchakachuaji),uhuru wa habari pamoja na uhuru wa kutoa maoni hata kama habari na maoni hayo hayawapendezi watawala),uhuru wa kuabudu pasipo kuwa kikwazo kwa waumini wa imani tofauti,uhuru wa kuishi ikiwa ni pamoja na kuepusha vifo vinavyoepukika (ajali zinazochangiwa na ufisadi wa polisi trafiki,ukosefu wa madawa unaochangiwa na ufisadi kwenye misaada/manunuzi kwenye sekta ya afya),uhuru wa kuishi bila kubaguliwa (mafisadi vs walalahoi,vigogo vs makabwela,watawala vs watawaliwa,nk),na KILA UHURU ambao ni HAKI ya msingi kwa mwanadamu.

Japo haipendezi kuzungumizia,ukweli mchungu ni kwamba miaka 49 ya uhuru wetu inatuacha na maswali mengi kuliko majibu.Na kama mzaha mbaya,siku chache kabla ya kusherehekea umri huu tumeshuhudia namna uchaguzi mkuu uliojaa kasoro lukuki na uchakachuaji ukitupatia "serikali mpya" (denti yuleyule lakini katika yuniformu mpya...ni dhahiri kuwa kama denti huyo ni "kichwa panzi" yunifomu hizo mpya hazitomsaidia lolote kimasomo).Na siku chache zilizopita tumeshindiliwa msumari wenye kutu katika kidonda kibichi pale kampuni ya Dowans "iliposhinda" kesi dhidi ya Tanesco (serikali) na sasa inastahili kulipwa mabilioni ya shilingi.Hiyo ndio salamu ya happy birthday kutoka kwa mafisadi.Tukio hilo halina tofauti na vitendo vya vibaka (hususan mitaa ya Mwananyamala karibu na hospitali kama unatokea Mwananyamala Kwa Kopa) ambapo vibaka wanakupiga roba ya mbao kisha wanakupigia ukelele wa "mwiz,mwizi".Kuporwa uporwe,na kipigo ukipate.Naam,ndivyo Dowans na wamiliki wake mafisadi wanavyotutenda.Huu ni ubakaji wa hadharani tena mchana kweupe.

Anyway,mie nasherehekea birthday yangu kibinafsi.Kama kuna mafanikio au mapungufu yaliyojiri katika miaka thelatini na kitu tangu nizaliwe yanabaki kuwa masuala binafsi.Lakini kwa vile Tanzania ni yetu sote,hatuna budi kusherehekea birthday yake kwa kufanya tafakuri kuhusu mantiki nzima ya "kuzaliwa" na kuwepo kwake.Ni kwa namna hiyo tu ndipo tutaweza kuendelea kusherehekea siku kama ya leo kwa "amani na utulivu" (tukumbuke mwenye njaa hana amani kama ilivyo kwa mgonjwa asiyeweza kupewa tiba stahili,au msafiri asiyeweza kufika aendako kwa vile barabara hazipitiki,au mlipakodi anayekwamishwa kimaisha na mgao usioisha wa maji na umeme,au mlalahoi asiye na haki mbele ya matakwa ya vigogo na mafisadi).

Happy birthday to me.Happy birthday Tanzania

Friday, 3 December 2010



The founder of WikiLeaks, Julian Assange, answers The Guardian readers' questions about the release of more than 250,000 US diplomatic cables

Fwoggie
I'll start the ball rolling with a question. You're an Australian passport holder - would you want return to your own country or is this now out of the question due to potentially being arrested on arrival for releasing cables relating to Australian diplomats and polices?

Julian Assange:
I am an Australian citizen and I miss my country a great deal. However, during the last weeks the Australian prime minister, Julia Gillard, and the attorney general, Robert McClelland, have made it clear that not only is my return is impossible but that they are actively working to assist the United States government in its attacks on myself and our people. This brings into question what does it mean to be an Australian citizen - does that mean anything at all? Or are we all to be treated like David Hicks at the first possible opportunity merely so that Australian politicians and diplomats can be invited to the best US embassy cocktail parties.

girish89
How do you think you have changed world affairs?
And if you call all the attention you've been given-credit ... shouldn't the mole or source receive a word of praise from you?

Julian Assange:
For the past four years one of our goals has been to lionise the source who take the real risks in nearly every journalistic disclosure and without whose efforts, journalists would be nothing. If indeed it is the case, as alleged by the Pentagon, that the young soldier - Bradley Manning - is behind some of our recent disclosures, then he is without doubt an unparalleled hero.

Daithi
Have you released, or will you release, cables (either in the last few days or with the Afghan and Iraq war logs) with the names of Afghan informants or anything else like so?
Are you willing to censor (sorry for using the term) any names that you feel might land people in danger from reprisals??
By the way, I think history will absolve you. Well done!!!
Julian Assange:
WikiLeaks has a four-year publishing history. During that time there has been no credible allegation, even by organisations like the Pentagon that even a single person has come to harm as a result of our activities. This is despite much-attempted manipulation and spin trying to lead people to a counter-factual conclusion. We do not expect any change in this regard.

distrot
The State Dept is mulling over the issue of whether you are a journalist or not. Are you a journalist? As far as delivering information that someone [anyone] does not want seen is concerned, does it matter if you are a 'journalist' or not?
Julian Assange:
I coauthored my first nonfiction book by the time I was 25. I have been involved in nonfiction documentaries, newspapers, TV and internet since that time. However, it is not necessary to debate whether I am a journalist, or how our people mysteriously are alleged to cease to be journalists when they start writing for our organisaiton. Although I still write, research and investigate my role is primarily that of a publisher and editor-in-chief who organises and directs other journalists.

achanth
Mr Assange,
have there ever been documents forwarded to you which deal with the topic of UFOs or extraterrestrials?
Julian Assange:
Many weirdos email us about UFOs or how they discovered that they were the anti-christ whilst talking with their ex-wife at a garden party over a pot-plant. However, as yet they have not satisfied two of our publishing rules.
1) that the documents not be self-authored;
2) that they be original.
However, it is worth noting that in yet-to-be-published parts of the cablegate archive there are indeed references to UFOs.

gnosticheresy
What happened to all the other documents that were on Wikileaks prior to these series of "megaleaks"? Will you put them back online at some stage ("technical difficulties" permitting)?
Julian Assange:
Many of these are still available at mirror.wikileaks.info and the rest will be returning as soon as we can find a moment to do address the engineering complexities. Since April of this year our timetable has not been our own, rather it has been one that has centred on the moves of abusive elements of the United States government against us. But rest assured I am deeply unhappy that the three-and-a-half years of my work and others is not easily available or searchable by the general public.

CrisShutlar
Have you expected this level of impact all over the world? Do you fear for your security?
Julian Assange:
I always believed that WikiLeaks as a concept would perform a global role and to some degree it was clear that is was doing that as far back as 2007 when it changed the result of the Kenyan general election. I thought it would take two years instead of four to be recognised by others as having this important role, so we are still a little behind schedule and have much more work to do. The threats against our lives are a matter of public record, however, we are taking the appropriate precautions to the degree that we are able when dealing with a super power.

JAnthony
Julian.
I am a former British diplomat. In the course of my former duties I helped to coordinate multilateral action against a brutal regime in the Balkans, impose sanctions on a renegade state threatening ethnic cleansing, and negotiate a debt relief programme for an impoverished nation. None of this would have been possible without the security and secrecy of diplomatic correspondence, and the protection of that correspondence from publication under the laws of the UK and many other liberal and democratic states. An embassy which cannot securely offer advice or pass messages back to London is an embassy which cannot operate. Diplomacy cannot operate without discretion and the
protection of sources. This applies to the UK and the UN as much as the US.
In publishing this massive volume of correspondence, Wikileaks is not highlighting specific cases of wrongdoing but undermining the entire process of diplomacy. If you can publish US cables then you can publish UK telegrams and UN emails.
My question to you is: why should we not hold you personally responsible when next an international crisis goes unresolved because diplomats cannot function.
Julian Assange:
If you trim the vast editorial letter to the singular question actually asked, I would be happy to give it my attention.

cargun
Mr Assange,
Can you explain the censorship of identities as XXXXX's in the revealed cables? Some critical identities are left as is, whereas some are XXXXX'd. Some cables are partially revealed. Who can make such critical decisons, but the US gov't? As far as we know your request for such help was rejected by the State department. Also is there an order in the release of cable or are they randomly selected?
Thank you.
Julian Assange:
The cables we have release correspond to stories released by our main stream media partners and ourselves. They have been redacted by the journalists working on the stories, as these people must know the material well in order to write about it. The redactions are then reviewed by at least one other journalist or editor, and we review samples supplied by the other organisations to make sure the process is working.

rszopa
Annoying as it may be, the DDoS seems to be good publicity (if anything, it adds to your credibility). So is getting kicked out of AWS. Do you agree with this statement? Were you planning for it?
Thank you for doing what you are doing.
Julian Assange:
Since 2007 we have been deliberately placing some of our servers in jurisdictions that we suspected suffered a free speech deficit inorder to separate rhetoric from reality. Amazon was one of these cases.

abbeherrera
You started something that nobody can stop. The Beginning of a New World. Remember, that community is behind you and support you (from Slovakia).
Do you have leaks on ACTA?
Julian Assange:
Yes, we have leaks on the Anti-Counterfeiting Trade Agreement, a trojan horse trade agreement designed from the very beginning to satisfy big players in the US copyright and patent industries. In fact, it was WikiLeaks that first drew ACTA to the public's attention - with a leak.

people1st
Tom Flanagan, a [former] senior adviser to Canadian Prime Minister recently stated "I think Assange should be assassinated ... I think Obama should put out a contract ... I wouldn't feel unhappy if Assange does disappear."
How do you feel about this?

Julian Assange:
It is correct that Mr. Flanagan and the others seriously making these statements should be charged with incitement to commit murder.

Isopod
Julian, why do you think it was necessary to "give Wikileaks a face"? Don't you think it would be better if the organization was anonymous?
This whole debate has become very personal and reduced on you - "Julian Assange leaked documents", "Julian Assange is a terrorist", "Julian Assange alledgedly raped a woman", "Julian Assange should be assassinated", "Live Q&A with Julian Assange" etc. Nobody talks about Wikileaks as an organization anymore. Many people don't even realize that there are other people behind Wikileaks, too.
And this, in my opinion, makes Wikileaks vulnerable because this enables your opponents to argue ad hominem. If they convince the public that you're an evil, woman-raping terrorist, then Wikileaks' credibility will be gone. Also, with due respect for all that you've done, I think it's unfair to all the other brave, hard working people behind Wikileaks, that you get so much credit.
Julian Assange:
This is an interesting question. I originally tried hard for the organisation to have no face, because I wanted egos to play no part in our activities. This followed the tradition of the French anonymous pure mathematians, who wrote under the collective allonym, "The Bourbaki". However this quickly led to tremendous distracting curiosity about who and random individuals claiming to represent us. In the end, someone must be responsible to the public and only a leadership that is willing to be publicly courageous can genuinely suggest that sources take risks for the greater good. In that process, I have become the lightening rod. I get undue attacks on every aspect of my life, but then I also get undue credit as some kind of balancing force.

tburgi
Western governments lay claim to moral authority in part from having legal guarantees for a free press.
Threats of legal sanction against Wikileaks and yourself seem to weaken this claim.
(What press needs to be protected except that which is unpopular to the State? If being state-sanctioned is the test for being a media organization, and therefore able to claim rights to press freedom, the situation appears to be the same in authoritarian regimes and the west.)
Do you agree that western governments risk losing moral authority by
attacking Wikileaks?
Do you believe western goverments have any moral authority to begin with?
Thanks,
Tim Burgi
Vancouver, Canada
Julian Assange:
The west has fiscalised its basic power relationships through a web of contracts, loans, shareholdings, bank holdings and so on. In such an environment it is easy for speech to be "free" because a change in political will rarely leads to any change in these basic instruments. Western speech, as something that rarely has any effect on power, is, like badgers and birds, free. In states like China, there is pervasive censorship, because speech still has power and power is scared of it. We should always look at censorship as an economic signal that reveals the potential power of speech in that jurisdiction. The attacks against us by the US point to a great hope, speech powerful enough to break the fiscal blockade.

rajiv1857
Hi,
Is the game that you are caught up in winnable? Technically, can you keep playing hide and seek with the powers that be when services and service providers are directly or indirectly under government control or vulnerable to pressure - like Amazon?
Also, if you get "taken out" - and that could be technical, not necessarily physical - what are the alternatives for your cache of material?
Is there a 'second line' of activists in place that would continue the campaign?
Is your material 'dispersed' so that taking out one cache would not necessarily mean the end of the game?
Julian Assange:
The Cable Gate archive has been spread, along with significant material from the US and other countries to over 100,000 people in encrypted form. If something happens to us, the key parts will be released automatically. Further, the Cable Gate archives is in the hands of multiple news organisations. History will win. The world will be elevated to a better place. Will we survive? That depends on you.
That's it every one, thanks for all your questions and comments. Julian Assange is sorry that he can't answer every question but he has tried to cover as much territory as possible. Thanks for your patience with our earlier technical difficulties

SOURCE: The Guardian

Thursday, 2 December 2010














Utawala wa URBAN PULSE CREATIVE MEDIA Unapenda kuwashukuru wale wote ambao walijitolea kufika, kushiriki na kutoa support ya namna moja au nyingine wakati wa URBAN TOUR ili kusaidia kuchangia fedha za kupambana na vita dhidi ya Malaria Tanzania. Tour hii ilifanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kuweza kupata publicity duniani kote na kuhamasisha watu mbalimbali ili kutambua umuhimu na namna ya kufanya ili kutokomeza ugonjwa huu kama ambapo kila mtu ataamua kuchukua majukumu na kufanya sehemu yake.

Itakuwa ni vigumu kutoa shukrani kwa kila mtu ila URBAN PULSE ingependa kutoa shukrani za dhati kwanza kabisa kwa Mwenyezi MUNGU ambaye alisaidia kufanikisha tour hii, Ubalozi wa Tanzania hapa UK Pamoja na staff wake,ASET(ASHA BARAKA; BARAKA MSILWA) Bloggers Wote waliosadia kutangaza show yetu ukianzia na MICHUZI,JIACHIE,MISS JESTINA,DJ CHOKA,TZ UK, HAKI NGOWI,GLOBAL PUBLISHERS, ABDALLAH MRISHO,KULIKONI UGHAIBUNI,HUNGA,MASHUGULI,KANUMBA,VINCENT KIGOSI,JENGATZ,MASHUGHULI,TA READING,LADY JAYDEE,MJENGWA,MTAA KWA MTAA,BONGO WIKEND na wengine wote.TV ; RADIO STATION zikiwepo BBC, BEN TV, BET,MTVBASE,AILTV, PRESENTERS: SPORAH, AYOUB MZEE, FRED MTOI, FRED MACHA, SAFINA,IDD SAFE, CHRIS GOLDFINGER NA JJ. MA DJZ; CHAMBI,ASH,ANDREW,10 TONNES,JCOM,MOJA PAMOJA NA CHRIS GOLD FINGER

Hiyo basi Imeandaa party ya kutoa shukrani na kusherekea anniversary ya kwanza ya URBAN PULSE kwa wote jumamosi hii kuanzia 10pm- 4am. DJZ on the deck DJ CHAMBI ;ANDREW


4th November 2010
CLUB AMBASSADOR
20 LONDON ROAD
BARKING, 1G11 8AJ


WOTE MNAKARIBISHWA
ASANTENI
URBAN PULSE CREATIVE



Nimetumiwa na mdau,nami nawasilisha

Nadhani kwa wakaazi wa Arusha na vitongoji vyake watakuwa wameshaona kwenye mabango mbalimbali barabarani ama kupitia redio ama magazeti ya kuwa iliyokuwa inaitwa Novotel Mount Meru Hotel inafunguliwa tena upya ikijulikana kama New Mount Meru Hotel.

Kikubwa nachotaka kuwafikishia watanzania wenzangu ni kuwa nimestaajabika sana ile maana kamili ya uwekezaji kuendelea kutupwa kapuni. Huwezi amini moderator na watanzania kwa ujumla, Hotel hii hadi maua na mchanga vyote vimetoka South Africa ambapo ndipo ilipo kampuni iliyopewa jukumu la kuindesha hotel hii ijulikanayo kama Zabulan.

Nachokiona hapa ni kuwa wasauzi afrika wao wanathamini vyao hata kama wako nje ya kwao, itakumbukwa watu walishapiga kelele kuhusu bidhaa zipatikanazo shoprite ya kuwa hadi nyanya na vitunguu hata mchicha vinatoka hukohuko SA, sasa ambacho watu watajionea hapa ni kuwa mchanga, maua, mbolea, signboards, tisheti, viatu, sabuni, vitambaa, computer, curtains na vyooote vinatoka sauzi afrika, hivi ina maana hapa hatuna hivyo vitu; vingine itasemekana labda viwango na jee hata mbolea na mchanga??

Kali zaidi ni kuwa Senior staffs woote ni ndani ya sauzi afrika ama asia au kwa watani wa jadi, ina maana hapa hatuna mameneja wazuri wakuendesha hotel? hatuna mashefu wazuri hapa tz?

Ikumbukwe walisema katika ajira wataweka mbele wazawa...hii imefia wapi??

Kama uwekezaji ndo hivi jamani bora tufie na tai shingoni.

Kali nyingine ni kuwa Raisi wetu yuleyule aliyeifunguaga Snow Crest Hotel then kesho yake ikaja kuvunjwa ukuta ndio anakuja tarehe 17 Dec kuifungua hii ambayo ilikuwa mali ya watanzania then Mkapa na Magufuli wakaiuza na sasa watanzania hawana hata percent moja hapa, hilo moja pili ni kuwa wafanyakazi woote ni wametoka kenya ama sauzi afrika ma bara asia na pia waliopewa tenda za ku-supply vyakula ni wakenya tupu na vyote vinatoka hukuhuko kenya kuanzia kuku, maharage hadi matunda, jamani rais hana washauri wakamfungua kwenye hili na jee watanzania tutakuwa wapole hadi lini watu wanakuja kupora malighafi zetu na kukimbia??


Ama ndio kichwa cha mwendawazimu??


TUAMKE WATANZANIA NA TULIANGALIE HILI SWALA LA MOUNT MERU KWA JICHO LATATU.


NGUVU YA UMAA IFANYE KAZI JAMANI............

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget