Tuesday, 5 July 2011

Imetumwa na FRANK EYEMBE wa Urban Pulse




ADAM GOLDMAN and MATT APUZZO   07/ 5/11 12:09 AM ET   AP
React
WASHINGTON -- After Navy SEALs killed Osama bin Laden, the White House released a photo of President Barack Obama and his Cabinet inside the Situation Room, watching the daring raid unfold.
Hidden from view, standing just outside the frame of that now-famous photograph was a career CIA analyst. In the hunt for the world's most-wanted terrorist, there may have been no one more important. His job for nearly a decade was finding the al-Qaida leader.
The analyst was the first to put in writing last summer that the CIA might have a legitimate lead on finding bin Laden. He oversaw the collection of clues that led the agency to a fortified compound in Abbottabad, Pakistan. His was among the most confident voices telling Obama that bin Laden was probably behind those walls.
The CIA will not permit him to speak with reporters. But interviews with former and current U.S. intelligence officials reveal a story of quiet persistence and continuity that led to the greatest counterterrorism success in the history of the CIA. Nearly all the officials insisted on anonymity because they were not authorized to speak to reporters or because they did not want their names linked to the bin Laden operation.
The Associated Press has agreed to the CIA's request not to publish his full name and withhold certain biographical details so that he would not become a target for retribution.
Call him John, his middle name.
John was among the hundreds of people who poured into the CIA's Counterterrorism Center after the Sept. 11 attacks, bringing fresh eyes and energy to the fight.
He had been a standout in the agency's Russian and Balkan departments. When Vladimir Putin was coming to power in Russia, for instance, John pulled together details overlooked by others and wrote what some colleagues considered the definitive profile of Putin. He challenged some of the agency's conventional wisdom about Putin's KGB background and painted a much fuller portrait of the man who would come to dominate Russian politics.
That ability to spot the importance of seemingly insignificant details, to weave disparate strands of information into a meaningful story, gave him a particular knack for hunting terrorists.
"He could always give you the broader implications of all these details we were amassing," said John McLaughlin, who as CIA deputy director was briefed regularly by John in the mornings after the 2001 attacks.
From 2003, when he joined the counterterrorism center, through 2005, John was one of the driving forces behind the most successful string of counterterrorism captures in the fight against terrorism: Abu Zubaydah, Abd al-Nashiri, Khalid Sheik Mohammed, Ramzi bin Alshib, Hambali and Faraj al-Libi.
But there was no greater prize than finding bin Laden.
Bin Laden had slipped away from U.S. forces in the Afghan mountains of Tora Bora in 2001, and the CIA believed he had taken shelter in the lawless tribal areas of Pakistan. In 2006, the agency mounted Operation Cannonball, an effort to establish bases in the tribal regions and find bin Laden. Even with all its money and resources, the CIA could not locate its prime target.
By then, the agency was on its third director since Sept. 11, 2001. John had outlasted many of his direct supervisors who retired or went on to other jobs. The CIA doesn't like to keep its people in one spot for too long. They become jaded. They start missing things.
John didn't want to leave. He'd always been persistent. In college, he walked on to a Division I basketball team and hustled his way into a rotation full of scholarship players.
The CIA offered to promote him and move him somewhere else. John wanted to keep the bin Laden file.
He examined and re-examined every aspect of bin Laden's life. How did he live while hiding in Sudan? With whom did he surround himself while living in Kandahar, Afghanistan? What would a bin Laden hideout look like today?
The CIA had a list of potential leads, associates and family members who might have access to bin Laden.
"Just keep working that list bit by bit," one senior intelligence official recalls John telling his team. "He's there somewhere. We'll get there."
John rose through the ranks of the counterterrorism center, but because of his nearly unrivaled experience, he always had influence beyond his title. One former boss confessed that he didn't know exactly what John's position was.
"I knew he was the guy in the room I always listened to," the official said.
While he was shepherding the hunt for bin Laden, John also was pushing to expand the Predator program, the agency's use of unmanned airplanes to launch missiles at terrorists. The CIA largely confined those strikes to targets along Pakistan's border with Afghanistan. But in late 2007 and early 2008, John said the CIA needed to carry out those attacks deeper inside Pakistan.
It was a risky move. Pakistan was an important but shaky ally. John's analysts saw an increase in the number of Westerners training in Pakistani terrorist camps. John worried that those men would soon start showing up on U.S. soil.
"We've got to act," John said, a former senior intelligence official recalls. "There's no explaining inaction."
John took the analysis to then CIA Director Michael Hayden, who agreed and took the recommendation to President George W. Bush. In the last months of the Bush administration, the CIA began striking deeper inside Pakistan. Obama immediately adopted the same strategy and stepped up the pace. Recent attacks have killed al-Qaida's No. 3 official, Mustafa Abu al-Yazid, and Pakistani Taliban leader Baitullah Mehsud.
All the while, John's team was working the list of bin Laden leads. In 2007, a female colleague whom the AP has also agreed not to identify decided to zero in on a man known as Abu Ahmed al-Kuwaiti, a nom de guerre. Other terrorists had identified al-Kuwaiti as an important courier for al-Qaida's upper echelon, and she believed that finding him might help lead to bin Laden.
"They had their teeth clenched on this and they weren't going to let go," McLaughlin said of John and his team. "This was an obsession."
It took three years, but in August 2010, al-Kuwaiti turned up on a National Security Agency wiretap. The female analyst, who had studied journalism at a Big Ten university, tapped out a memo for John, "Closing in on Bin Laden Courier," saying her team believed al-Kuwaiti was somewhere on the outskirts of Islamabad.
As the CIA homed in on al-Kuwaiti, John's team continually updated the memo with fresh information. Everyone knew that anything with bin Laden's name on it would shoot right to the director's desk and invite scrutiny, so the early drafts played down hopes that the courier would lead to bin Laden. But John saw the bigger picture. The hunt for al-Kuwaiti was effectively the hunt for bin Laden, and he was not afraid to say so.
The revised memo was finished in September 2010. John, by then deputy chief of the Pakistan-Afghanistan Department, emailed it to those who needed to know. The title was "Anatomy of a Lead."
As expected, the memo immediately became a hot topic inside CIA headquarters and Director Leon Panetta wanted to know more. John never overpromised, colleagues recall, but he was unafraid to say there was a good chance this might be the break the agency was looking for.
The CIA tracked al-Kuwaiti to a walled compound in Abbottabad. If bin Laden was hiding there, in a busy suburb not far from Pakistan's military academy, it challenged much of what the agency had assumed about his hideout.
But John said it wasn't that far-fetched. Drawing on what he knew about bin Laden's earlier hideouts, he said it made sense that bin Laden had surrounded himself only with his couriers and family and did not use phones or the Internet. The CIA knew that top al-Qaida operatives had lived in urban areas before.
A cautious Panetta took the information to Obama, but there was much more work to be done.
The government tried everything to figure out who was in that compound.
In a small house nearby, the CIA put people who would fit in and not draw any attention. They watched and waited but turned up nothing definitive. Satellites captured images of a tall man walking the grounds of the compound, but never got a look at his face.
Again and again, John and his team asked themselves who else might be living in that compound. They came up with five or six alternatives; bin Laden was always the best explanation.
This went on for months. By about February, John told his bosses, including Panetta, that the CIA could keep trying, but the information was unlikely to get any better. He told Panetta this might be their best chance to find bin Laden and it would not last forever. Panetta made that same point to the president
Panetta held regular meetings on the hunt, often concluding with an around-the-table poll: How sure are you that this is bin Laden?
John was always bullish, rating his confidence as high as 80 percent.
Others weren't so sure, especially those who had been in the room for operations that went bad. Not two years earlier, the CIA thought it had an informant who could lead him to bin Laden's deputy. That man blew himself up at a base in Khost, Afghanistan, killing seven CIA employees and injuring six others.
That didn't come up in the meetings with Panetta, a senior intelligence official said. But everyone knew the risk the CIA was taking if it told the president that bin Laden was in Abbottabad and was wrong.
"We all knew that if he wasn't there and this was a disaster, certainly there would be consequences," the official recalled.
John was among several CIA officials who repeatedly briefed Obama and others at the White House. Current and former officials involved in the discussions said John had a coolness and a reassuring confidence.
By April, the president had decided to send the Navy SEALs to assault the compound.
Though the plan was in motion, John went back to his team, a senior intelligence official said.
"Right up to the last hour," he told them, "if we get any piece of information that suggests it's not him, somebody has to raise their hand before we risk American lives."
Nobody did. Inside the Situation Room, the analyst who was barely known outside the close-knit intelligence world took his place alongside the nation's top security officials, the household names and well-known faces of Washington.
An agonizing 40 minutes after Navy SEALs stormed the compound, the report came back: Bin Laden was dead.
John and his team had guessed correctly, taking an intellectual risk based on incomplete information. It was a gamble that ended a decade of disappointment. Later, Champagne was uncorked back at the CIA, where those in the Counterterrorism Center who had targeted bin Laden for so long celebrated. John's team reveled in the moment.
Two days after bin Laden's death, John accompanied Panetta to Capitol Hill. The Senate Intelligence Committee wanted a full briefing on the successful mission. At one point in the private session, Panetta turned to the man whose counterterrorism resume spanned four CIA directors.
He began to speak, about the operation and about the years of intelligence it was based on. And as he spoke about the mission that had become his career, the calm, collected analyst paused, and he choked up.



Nimekutana nayo huko Jamii Forums.For the time being,taarifa hii inabaki kuwa tuhuma tu hadi hapo itakapothibitishwa.

Wana Jf Mm nimefikia hapa hoteli inayoitwa AFRICA TULIP hapa Arusha mbunge wa CCM Viti maalum kutoka mbeya,Mary Mwanjelwa amekamatwa akiwa ameiba Mataulo,Vikapu vidogo ambavyo huwekwa maua chooni wafanyakazi wa hapa wanadai tukio hili ni la pili baada ya mwezi uliopita kufanya tukio la aina hiyo aliondoka salama wafanyakazi wakakatwa mshahara leo wakati ana check out wafanyakazi waliamua kumsachi na kweli wakakuta ameiba.Hili ni tukio la aibu ameaibisha nchi, bunge na chama chake. Wafanyakazi wa hapa leo wanadai kwamba mabinti wawili mwezi Jana walikatwa kiasi cha shilingi laki 2 nilikua na wazungu wamesikitika sana baada ya kufahamu kuwa huyu ni mbunge.Wanajf nimesikitika nikasema nanyi muipate taarifa hii ni aibu kwa Taifa,Fatilieni ni tukiop la Leo hapa Hotelini ni AIBU NI AIBU NI AIBU DUH Wana Jf nimefatilia Mara ya kwanza alifikia chumba namba 14 akafanya wizi wa soup dish,wizi wa mara ya pili ni room namba 20 miongoni mwa vitu alivoiba ni Pambo la Kitanda,Marekebisho ni kwamba aliiba siku ya Jpili si leo.Naomba kuwasilisha.


DAR PLUS ni Jarida jipya ambalo liko njiani kuingia mtaani mda si mrefu. Jarida hili ni maalum kwa ajili kutoa matangazo na kutangaza biashara ya aina yoyote ikiwepo mitindo, burudani, michezo na matukio mbali mbali kutoka kwenye pande zote za dunia. Vile vile litakuwa likiwaletea habari motomoto pamoja mahojiano ya watu mashuhuri wanaotoa mchango katika jamii yetu.

Kwa maelezo zaidi na gharama za matangazo piga simu namba +255 657 975 747 au +255 655 454 162

Asanteni
DAR PLUS GROUP

Monday, 4 July 2011


Nimekuwa nikipokea shutuma na lawama nyingi kwamba ninaichukia CCM na uongozi wake (sana sana nikituhumiwa kuwa na "chuki binafsi").Kadhalika,nimekuwa nikilaumiwa kuwa ninamchukia Rais Jakaya Kikwete,huku wengine wakidai mimi nia Chadema damu damu.

Kawaida yangu ni kutojihusisha na malumbano na wasomaji wa blogu hii.Hata hivyo,ninapotupiwa shutuma kwa lugha ya kistaarabu huwa najaribu kutoa ufafanuzi kuhusu mtizamo na msimamo wangu.Naomba nirejee position yangu.Kwanza,mimi ni Mtanzania,na japo nimekuwa nje ya nchi yangu kwa takriban muongo (decade) moja sasa,haijanipunguzia japo kwa asilimia 0.0001 utanzania wangu.Baba yangu,kaka na dada zangu,wadogo zangu,marafiki,ndugu na jamaa wengi (zaidi ya asilimia 99.9) bado wapo Tanzania.Kwahiyo uwepo wangu hapa Uingereza haunipunguzii utanzania wangu.Kwa mantiki hiyo,kila kinachowagusa Watanzania wenzangu kinanigusa pia,regardless Watanzania hao wapo huko nyumbani au nje ya nchi.

Pili,mimi ni mwanafunzi wa stadi za siasa (political studies).Japo siwezi kujiita mtaalamu wa siasa au kujimilikisha uelewa wa hali ya juu wa siasa,ukweli ni kwamba angalau ninaielewa siasa at an advanced stage.Sasa kuna faida gani ya kuelimika pasipo kuitumikia jamii?Kwa wasiofahamu definition ya elimu,neno hilo linamaanisha jitihada za binadamu katika kukabiliana na mazingira yake.Sasa kama nimeelimika kwenye fani ya siasa,kisha nikaacha kutumia elimu hiyo kuisaidia jamii yangu kwa namna moja au nyingine,basi sintokuwa na tofauti na mafisadi.Ufisadi wa kitaaluma sio tu kufoji vyeti au kutelekeza taaluma na kukimbilia fedha bali pia kutoitumia taaluma ipasavyo.

Tatu,uwepo wangu nje ya nchi umenisaidia kulinganisha na kutofautisha baadhi ya mambo yanayotokea huko nyumbani.Actually,wakati naanzisha blogu hii niliweka bayana approach yangu katika mambo mbalimbali nitakayokuwa nayaongelea humu.Nilibainisha kuwa napendelea kujadili mambo katika namna ya kukosoa.Natambua kuwa sie waswahili hatupendi kukosolewa (at least wengi wetu).Lakini tatizo sio kukosoa bali kukosoa fyongo,kwa mfano kumkosoa mtu kwa vile tu humpendi.Mara kadhaa nimejaribu kuwaeleza wasomaji wangu kuwa,kwa mfano,sina tatizo na Mtanzania mwenzangu aitwaye Jakaya Kikwete bali nina matatizo na kiongozi wa nchi yetu,Rasi Jakaya Kikwete.Na sina matatizo na naye kwa vile yeye ni Mkwere na mie ni Mndamba (by the way wote ni Watanzania) bali tatizo langu kubwa lipo kwenye udhaifu wa uongozi wake.

Kuhusishwa kwangu na Chadema kunatokana na kushabihiana kimtizamo.Chama hicho kimejidhihirisha kuwa  mahiri katika mapambano dhidi ya ufisadi na maovu mengine katika jamii yetu.Nami pia hilo ndilo jukumu langu kubwa.Kwangu,faida pekee ya elimu yangu ni pale itakapotumika ipasavyo kuitumikia nchi yangu.Kwa kugusia tu,hata kabla ya kuanza uandishi nilikuwa naitumikia nchi yangu katika namna mbayo Watanzania wengi hawajapata fursa kama hiyo.Nisingependa kufafanua kwa sababu za kimaadili na kisheria lakini tu ieleweke kuwa nami ni miongoni mwa Watanzania wachache kabisa waliokuwa wakikesha macho for several nights a week kuifanya Tanzania yetu kuwa nchi stahili ya kuishi.You could feel the blanks by yourself,if you wish to.

Sasa,pamoja na mabaya mengi ya CCM,kuna baadhi ya viongozi wa chama hicho ambao kwa hakika kuna nyakati wanastahili pongezi.Na makala hii inamhusu January Makamba.Najua madhara ya kumsifia kiongozi; watu hawakawii kuhitimisha kuwa "aah anajikomba huyu".Well,let anybody make such a silly conclusion lakini penye ukweli sharti tuseme au tuandike.

Gazeti la Mwananchi toleo la leo lina habari kuwa Wizara ya Nishati na Madini imeingia kwenye kashfa ya kuhonga wajumbe wa kamati ya bunge ya nishati na madini ili "bajeti ya wizara hiyo ipite kiulaini huko bungeni".And guess what,aliyefanikisha kufahamika kwa taarifa hizo za kushtua si mwingine bali mwenyekiti wa kamati hiyo,yaani January.Huu ni uzalendo wa kupigiwa mstari.Ukiweka kanda political rhetorics and sentiments ambazo zimezoeleka kwenye competitive politics,January ana mitizamo inayoshairia kuweka mbele maslahi ya nchi badala ya maslahi ya chama chake.Of course,kama kiongozi wa CCM analazimika kuisifia na kuwarushia madongo wanasiasa wa upinzani,lakini hatuwezi kumhukumu kwa yale tusiyayapenda tu.Ndio maana hata katika makala niliyoandika kwenye jarida la Raia Mwema kumkosoa baba wa taifa Julius Nyerere nilibainisha wazi kuwa wengi tunafahamu mazuri ya Nyerere lakini "mabaya" yake yamebaki kuwa muted au taboo kuyaongelea.Kama kuongelea "mabaya" ya Nyerere hakumaanishi kumchukia,kumsifia January Makamba hakumaanishi kuipenda CCM (at least kwa madudu yake na ulezi wake kwa mafisadi).It simply means giving credit where it's due...au kwa kiswahili ni mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Kwahiyo Mheshimiwa January,natumaini hutoishia tu kwenye kufichua uovu ndani ya kamati yako bali pia utajaribu kusambaza jitihada zako za kizalendo na kwenye maeneo mengine pia.CCM inahitaji viongozi watakaotanguliza maslahi ya nchi mbele ya maslahi ya chama.Haimaanishi msiwe mashabiki wa chama chenu bali nchi yetu ni muhimu zaidi ya chama cha siasa.

Anyway,habari husika ni hii hapa chini

Kashfa nzito Wizara ya Ngeleja  
Monday, 04 July 2011 08:44
MAOFISA WA JUU WATUHUMIWA KUIHONGA KAMATI YA MAKAMBA
Mwandishi Wetu
WIZARA ya Nishati na Madini imeingia katika kashfa nzito ambapo baadhi ya maofisa wa wizara hiyo wanatuhumiwa kuwahonga baadhi ya wabunge katika Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kwa kile kinachodaiwa kutaka bajeti ya wizara hiyo kupita kwa urahisi, Mwananchi limebaini.
Habari zilizopatikana kutoka Dodoma na Dar es Salaam zimedokeza kuwa taarifa za uovu huo tayari zimefikishwa mezani kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amesema atalishughulikia baada ya kuwa amewasiliana na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja.
Kwa mujibu wa habari hizo suala hilo pia tayari limefikishwa kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda na kwamba kamati ya uongozi ya bunge anayoiongoza pia imearifiwa kuhusu suala hilo.
Kashfa hiyo imeikumba wizara hiyo katika kipindi kigumu ambacho nchi iko gizani huku wizara hiyo ikilaumiwa kutokana na uhaba wa nishati ya umeme kiasi cha Waziri Ngeleja kutangaza mgawo wa saa 10 wakati wa mchana na saa sita wakati wa usiku "ni janga la kitaifa".
Habari zaidi zinasema miongoni mwa mambo muhimu ambayo kamati hiyo ilikuwa ikitaka maelezo ni mapendekezo ya wizara hiyo kutaka kujenga jeno la makao yake makuu jijini Dar es Salaam kinyume cha ilani ya CCM ambayo inaweka wazi kwamba hakutakuwa na ujenzi wa makao makuu ya wizara jijini humo katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Habari zilizolifikia Mwananchi zilidai kwamba, Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini ya Bunge, January Makamba ndiye aliyewasilisha malalamiko kwa Pinda na Makinda baada ya kubaini 'ulegevu' miongoni mwa wajumbe wa kamati yake wakati wa mchakato wa kujadili mapendekezo ya bajeti ya Wizara hiyo na kwamba mapema alikuwa ameishapokea taarifa kuhusu baadhi ya wajumbe wake kuhongwa.
"Mwenyekiti (January) alipewa taarifa za wajumbe wawili wa kamati yake ambao walikataa hongo hiyo, na baada ya kufanya uchunguzi alibaini kwamba kuna kila dalili kwamba baadhi ya wabunge katika kamati yake walikuwa wamebadili msimamo katika baadhi ya mambo," kilieleza chanzo chetu mjini Dodoma.
Habari zaidi zilidai kuwa kufuatia hali hiyo, January aliitisha kikao cha wabunge ambao ni wajumbe wa kamati yake na kugeuka mbogo, huku akiweka bayana kuchukizwa kwake na taarifa za wajumbe wake kuhongwa na kwamba alikwenda mbali zaidi akitishia kujiuzulu nafasi ya uenyekiti ili kutoa nafasi kwa wabunge hao kuchagua mwenyekiti mwingine ambaye atakuwa tayari kuvumilia uovu huo.
"Yule kijana (January) alikasirika sana, alichukizwa kweli kweli na hali hiyo kwa sababu ni kama wajumbe waliopokea hizo bahasha walikuwa wakimzunguka kwani tayari walikuwa wanajua nini wanachopaswa kufanya ili kuziokoa sekta za nishati na madini,"kilieleza chanzo hicho.
Kadhalika suala hilo la hongo lilijadiliwa katika kikao cha pamoja baina ya wajumbe wa kamati hiyo na viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini, ambapo Waziri Ngeleja na Naibu wake, Adam Malima waliomba radhi kutokana na tukio hilo, hivyo kamati hiyo kuagiza maofisa wa wizara waliohusika wachukuliwe hatua.
"Ni kama Ngeleja na Malima walimalizana na kamati, si unajua maana ni kama January alikuwa peke yake, kama kulikuwa na wanaomsapoti (wanaomuunga mkono) walikuwa ni wachache, hivyo kama waziri na naibu wake waliomba radhi hakukuwa jinsi zaidi ya kumalizana nao," zilidai taarifa hizo na kuongeza:
"Hata hivyo Mwenyekiti na baadhi ya wajumbe walimwagiza Ngeleja na Malima kuwachukulia hatua maofisa waliohusika na ugawaji wa fedha hizo kwa baadhi ya wabunge".
Kauli za viongozi
Mwananchi liliwasiliana na January ili kufahamu undani wa suala hilo, lakini mbunge huyo wa Bumbuli hakukanusha wala kukubali kuhusu baadhi ya wajumbe wake kupokea rushwa.
"Nani kakwambia bwana, mimi siwezi kuzungumza lolote, mambo ya kamati jamani si yote tunayoweza kuweka wazi, lakini siku hizi hatufanyi vikao bila kuwaruhusu waandishi wa habari, kama hayo yangetokea si yangeonekana wakati huo?,"alihoji January.
Waziri Ngeleja kama ilivyo kwa January naye hakukubali wala kukanusha kuwepo kwa tuhuma hizo na badala yake alisisitiza kwamba anayeweza kuzizungumzia ni mwenyekiti wa kamati akimaanisha January.
"Unasikia, kama jambo limetokea kwenye kamati mimi sina mamlaka ya kulizungumzia hata kidogo maana nitakuwa navunja kanuni, kama wengine nilivyowaambia maana naona leo wengi wananitafuta kwa habari hii, mpigieni mwenyekiti wa kamati yeye ana mamlaka, mimi kwangu no comment (siwezi kusema chochote),"alisema Ngeleja kwa simu.
Spika wa Bunge, Makinda kwa upande wake pia alikanusha kupokea taarifa hizo. "Mimi ndiyo nazisikia kutoka kwako, pengine kama zimeletwa kwa barua sijaiona, lakini sifahamu kitu kama hicho," alisema Makinda alipozungumza kwa simu na Mwananchi.
Kwa upande wake Naibu Spika Job Ndugai alisema kuwa hana taarifa hizo kwa kuwa yeye alikuwa nje ya nchi kikazi. "Ndugu yangu, pengine ukimpata Spika anaweza kukusaidia, mimi nimerudi jioni hii (jana jioni) ndio naingia hapa Dodoma najiandaa kwa ajili ya kesho,"alisema Ndugai.

Nihitimishe makala hii kwa kutoa wito kuwa it's high time Ngeleja has to go.Sijui afanye madudu yepi ili Rais Kikwete agunude kuwa Waziri huyu hafai kuendelea kuongoza Wizara hiyo nyeti lakini ni matarajio yetu kuwa skandali hili jipya ni kitanzi cha mwisho kwa Ngeleja.He has to go..NOW!

Kadhalika,Spika Anne Makinda sasa anapaswa kuhamishia udikteta wake kwa wabunge wa upinzani  to wajumbe wa kamati waliopokea mlungula.Na jeshi la polisi ambalo ni mahiri kwa kuwabana wapinzani linapaswa kuanza uchunguzi wa mara moja kuhusu suala hili,sambamba na TAKUKURU.

Sunday, 3 July 2011


DCI Manumba katika kashfa; Adaiwa kumkingia kifua mbunge asikamatwe
Sunday, July 3, 2011, 12:03
Habari, Mtanzania
*Adaiwa kumkingia kifua mbunge asikamatwe

Na Kulwa Karedia

MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, amedaiwa kumkingia kifua Mbunge wa Busega, Dk. Titus Kamani (CCM) asikamatwe.
Uamuzi wa kukamatwa umekuja baada ya mbunge huyo kuhusishwa na njama za kutaka kumuua aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Dk. Raphael Chegeni.

Habari zinadai kuwa, DCI Manumba amekuwa akimkingia kifua mbunge huyo, licha ya Jeshi la Polisi kutangaza azma ya kumkamata kwa nguvu kutokana na ukaidi wa kutotii amri ya jeshi hilo.

Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari, DCI Manumba amekuwa akimkingia kifua mbunge huyo kwa kuwa wanatoka wilaya moja ya Magu, mkoani Mwanza.

Taarifa hizo ziliendelea kudai kuwa, tayari Dk. Kamani alikwisha jisalimisha polisi mkoani Mwanza mwishoni mwa wiki kwa mahojiano zaidi.

Akizungumza na MTANZANIA Jumapili, Manumba alikanusha shutuma hizo na kueleza kuwa tangu mbunge huyo ahusishwe na sakata hilo, hajawahi kumkingia kifua kwa namna yoyote.

“Kwanza nikwambie ukweli, suala hilo ndilo kwanza nalisikia kwako, sielewi kinachoendelea… kama kuna mambo Dk. Kamani amefanya taratibu zote za kisheria zitafuatwa.

“Sijawahi hata siku moja kumkingia kifua, kesi yao naamini inashughulikiwa kwa mujibu wa sheria za nchi, sasa iweje mimi nijiingize kwenye kitu ambacho sihusiki?” alihoji DCI Manumba.

DCI Manumba alisema yeye hapaswi kuzungumzia kwa undani suala hilo kwa kuwa si msemaji wa polisi na kwamba anayefaa kuhojiwa ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Saimon Sirro.

“Sasa hayo mengine unayosema mimi si msemaji, nakuomba umtafute RPC Sirro yeye ndiye anayeweza kuzungumzia zaidi suala hilo kwa kuwa limetokea kwake,” alisema.

DCI Manumba alikiri kutoka eneo moja na mbunge huyo, ingawa alisema hiyo si sababu ya kumkingia kifua. “Ni kweli huyu ni mbunge wangu na mimi ni mpiga kura wake, lakini hii si sababu ya kufanya nizuie polisi wasifanye kazi yao, hakuna mtu aliye juu ya sheria, hatutoki kijiji kimoja…narudia mimi ni mpiga kura wake, …nawashauri wale wote wanaohusishwa na tukio hili, waendelee na mambo yao, mimi sihusiki hata chembe katika hili,” alisema DCI Manumba.
Alisema upelelezi ndiyo njia pekee itakayomkomboa mbunge huyo kama ana hatia au la.

“Unajua hatufanyi kazi kwa kukurupuka, upelelezi unaoendelea ndiyo njia pekee itakayoamua kama nani ana kesi ya kujibu, tungoje tuone,” alisema.

Mapema wiki hii, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Simon Sirro, aliwaambia waandishi wa habari kuwa mbunge huyo alijisalimisha na kutoa maelezo yake kuhusiana na tuhuma zinazomkabili.

Alisema mbunge huyo alifika na kuhojiwa mwishoni mwa wiki na baada ya hapo aliachiwa, huku polisi wakiendelea na upepelezi zaidi kabla ya kumpandisha kizimbani.

Habari zinasema mbunge huyo, alijisalimisha kituo cha polisi Juni 25, mwaka huu na kuhojiwa usiku kabla ya kuondoka kuelekea Dodoma kuendelea na vikao vya Bunge. Akiwa mkoani Shinyanga, gari lake liligonga mtu na kuua papo hapo.

Mei 31, mwaka huu, inaelezwa kuwa Jeshi la Polisi mkoani Mwanza, liliandika barua Ofisi ya Bunge kutaka Dk. Kamani aende Mwanza kwa ajili ya mahojiano dhidi ya tuhuma zinazomkabili.

Barua hiyo yenye namba MZR/CID/SCR/105/2011/4 ilitumwa kwa Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila ikimtaka Dk. Kamani kwenda kujibu kesi yenye namba ya usajili MW/IR/2607/2011-MR-CC.28/2011.

Dk. Kamani atakuwa mshitakiwa wa tano iwapo atafikishwa mahakamani, baada ya watu wanne ambao ni Dismas Zacharia Ndaki, Erasto Kazimili Kombe, Queen Joseph Bogohe na Ellen Joseph Bogohe, ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Mwanza.

CHANZO: Mtanzania



Na Nova Kambota,

Binafsi nimeshtushwa sana na kauli za baadhi ya wana CCM kuwa chama chao kimeshajivua gamba , wanatumia mabadiliko ya safu ya uongozi ndani ya chama hiko yaliyofanyika hivi karibuni huko Dodoma, wakiwa na furaha kubwa wanadai kuwa hatua ya sekretarieti ya chama chao kujiuzulu huku ikimtupa nje katibu mkuu Yusuph Makamba na kumwingiza katibu mkuu mpya Willison Mkama na pia hatua ya kamati kuu ya chama hiko kuvunjika kwa maana nyingine imewatupa nje wajumbe mbalimbali lakini kati ya hao wapo wanasiasa wawili waliotawala vichwa vya magazeti hawa ni Andrew Chenge na Rostam Aziz lakini kujipa matumaini wanaccm wanadai kuwa kuingia kwa sura mpya tena za vijana kama Nappe Nauye na January Makamba ni ushahidi kuwa chama chao kimejivua gamba na sasa kipo safi .

Hata hivyo miezi michache tu baada ya safu mpya ndani ya chama hiko kutangazwa dalili za wazi kabisa zimeonekana kuwa CCM ilikuwa imeshiba sana kiasi kwamba ilikuwa vigumu kwake kupenya kwenye tundu jembamba sana hivyo ilipaswa kujivua gamba ili ipite lakini kwavile gamba la CCM limeshikamana na ngozi basi kikao cha Dodoma kimehofia maumivu ya kuvua gamba na badala yake CCM imejidanganya yenyewe kama sio kufanya mchezo wa kitoto wa kutapika ikidhani kuwa kwa kupunguza ukubwa wa tumbo itaweza kupenya hapo lakini sivyo inapaswa kujivua gamba! Lakini kwanini nasema CCM imetapika tu na sio kujivua gamba kama wengi wadhaniavyo?

Kwanza kabisa wanabiolojia au wataalamu wa elimu ya viumbe wanafahamu kuwa nyoka hajivui gamba kwa lazima la hasha! Bali gamba lenyewe huelegea na kujivua au hulegea sana na wakati nyoka akipita kwenye upenyo Fulani basi gamba huvuka hata pasipo nyoka mwenyewe kufahamu huu ni ukweli wa kisayansi kabisa lakini cha ajabu sana ni kile kinachoitwa kujivua gamba kwa ccm ni kwa kujilazimisha ,hakika nyoka hawezi kujivua gamba kwa kujilazimisha hivyo hata CCM haiwezi kujivua gamba kwa kujilazimisha badala yake inaweza kutapika kwa kujilazimisha labda kwa kuingiza vidole kwenye koromeo au kula kitu Fulani kitakachopelekea tumbo kuvurugika kisha kutapika hivyo kwa mantiki hii ni dhahiri kabisa ilichofanya CCM ni kutapika tu lakini sio kujivua gamba kama wanavyotaka kuuaminisha umma wa watanzania.

Pili ni jinsi CCM ilivyoshindwa kufanya mabadiliko ya kimchakato ndan ya mioyo ya makada wake nasema hivi kwasababu naona kabisa kile kinachoitwa migawanyiko au minyukano ndani ya CCM itaendelea kwa maana mpaka sasa CCM haijafanikiwa kujipambanua kiitikadi na kiimani iwapo ipo pamoja na wafanyabiashara ambao ni wafadhili wa chama hiko huku wengi wao wakihusishwa na tuhuma za ufisadi au wapo pamoja na wakulima na wafanyakazi ambao ndio wenye chama chao lakini sasa wameporwa kiasi kwamba sasa wenye fedha ndio wenye nguvu na ndio wenye uwezo wa kugombea na kushinda ndani ya chama hiko kiasi kwamba katibu mkuu wa zamani wa chama hiko Philip Mangula aliwahi kutamka kuwa CCM itangaze tenda kwenye kuwania uongozi! Hivyo ni wazi kuwa CCM haijaweza kuwaleta meza moja Harrison Mwakyembe na Edward Lowassa, pia haijafaulu kuwakutanisha kimtazamo Samwel Sitta na Rostam Aziz au kuwaimbisha wimbo mmoja Andrew Chenge na Anne Kilango Malecela wala mabadiliko haya hayawezi kuwasemesha lugha moja Yusuph Makamba na Shy-Rose Bhanji, CCM ingejivua gamba haya yasingekuwepo lakini kwavile imejidanganya kwa kutapika tu siiombei mabaya ila nasema isubiri ione nini kitafuata.

Tatu CCM ingejia gamba kweli isingejitosa kwenye maji ya moto tena yanayochemka nasema hivi kwasababu mpaka sasa dalili za wazi zinaonyesha kuwa CCM haiamini kuwa ipo ndani ya mfumo wa vyama vingi chukulia mfano wa hoja ya katiba mpya , naona kabisa ukimtoa Prince Bagenda nadhani wanaccm wengine wote licha ya kutamka kuwa katiba ni hoja ya wananchi ila mioyoni mwao wanaamini katiba ni hoja ya CHADEMA, CUF, NCCR na baadhi ya wanaharakati tu kwasababu iwapo kweli CCM inaamini kuwa ipo kwenye ushindani wa kisiasa kwenye mfumo wa vyama vingi basi kujijenga kwake kungetegemea katika kuipenda na kuikuza demokrasia badala yake inategemea nguvu zake , mimi naamini CCM ilipaswa kuwa ya kwanza kuipinga rasimu ya marekebisho ya katiba kwa jinsi ilivyojaa mapungufu badala yake inaunga mkono licha ya mapungufu hayo hii inatafsiri gani? Je CCM inataka kuvikomoa vyama vya upinzani au uhafidhina unaisumbua CCM? Je CCM ingejivua gamba ingeendeleza uhafidhina wa jinsi hii? au na yenyewe ingepinga rasimu hiyo? Jibu rahisi ingejivua gamba isingekuwa na uchafu wa aina hii ila kwavile imetapika tu ndio maana sasa ina njaa ya kuwakomoa wapinzani lakini niwakumbushe kuwa katiba mpya ni hitaji la watanzania sio CHADEMA wala CUF.

Nne CCM walipaswa kufanya mapinduzi ya kimfumo sio watu kama ilivyofanya, kwangu mimi nilitegemea CCM ingekuja na maazimio ya kukomesha mfumo wa wafanyabiashara kukimbilia ndani ya chamma hiko na vilevile kukomesha mfumo wa viongozi wa chama hiko kupendaz kusifia na kusifiwa tu , mimi nilitegemea kuwa sasa CCM inaandaa mkakati rasmi wa kuwa na tabia ya kujikosoa ili kulinda staha, tunu na falsafa ya mapinduzi ya chama hiko lakini sijaliona hili amini nakwambia ndani ya CCM bado ukiwa msemakweli kama Samwel Sitta,Harrison Mwakyembe na John Magufuli utajikuta unaongeza maadui kuliko marafiki, mambo haya hayawezi kubadilishwa kwa kumwondoa Makamba na kumweka Mkama bali kubadili mfumo wa CCM ndio maana nasisitiza kuwa ilichofanya CCM imetapika tu haijajivua gamba kwa kuhofia maumivu kwa maana gamba limeshikamana na ngozi.

Tano nilitegemea CCM ijisafishe kwa dhati kabisa kwenye kila ngazi na jumuiya zake tena kwa kuwapiga chini viongozi wale wanaoonekana ni mzigo lakini siamini kama hili litafanyika , hapa sidhani kama UVCCM , UWT na Jumuiya ya wazazi zitaguswa, labda nitumie wasaa huu kumpa siri Jakaya Kikwete kuwa hayo anayoita makundi na minyukano ya vigogo wa chama hiko kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 chanzo chake haswa ni huko kwenye jumuia hizi na endapo hatazigusa wala kuzitikisa walau kidogo basi hicho kinachoitwa kujivua gamba litakuwa ni jambo la kufikirika tu kuliko uhalisia ndani ya chama chake hiko.

Mwishowe nihitimishe makala haya kwa kuwaasa wanaaccm kuwa bado wana safari ndefu ya kujivua gamba sio kirahisirahisi hivi kama wanavyodhani tena hakuna ubishi kuwa kwa gamba lilliloshikamana na ngozi kazi kubwa inahitajika kulivua, kwa upande wa vijana wa chama hiko wasishangilie kuingia kwa vijana wenzao January Makamba na Nappe Nauye bali wanapaswa wajikite zaidi katika mapambano ya ndani ya chama yatakayowawezesha kukibadili chama hiko kutoka wazee oriented kuwa vijana oriented kisha wapindue mfumo wa wafanyabiashara na wakirudishe chama mikononi mwa wakulima na wafanyakazi vinginevyo hiko wanachoita kujivua gamba si lolote bali ni kutapika tu na hivyo CCM yao haiwezi kupenya kwenye mioyo miyembamba ya watanzania masikini kwa kujitapisha tu bali inapaswa ijivue gamba hata kama itapata maumivu makali…Tafakari!


Nova Kambota,
+255717 709618
novakambota@gmail.com
www.novakambota.com
Tanzania, East Africa
Jumamosi, 2 julai 2011

Naomba kura yako kwenye tuzo za blog Tanzania kwenye vipengele vya best collaboration/group blog, best informative political blog na best political blog kunipigia kura nenda www.tanzanianblogawards.com

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget