Monday, 5 September 2011
05:45
Unknown
Igunga, Mjengwa
No comments
Kuna wagombea watatu wenye kuchuana vikali Igunga; Dr Peter Kafumu ( CCM), Leopard Mahona ( CUF) na Joseph Kashindye ( CHADEMA). Blogu yako ya Jamii Shirikishwa, Mjengwablog, imekuandalia Pima- Maji ili utoe maoni yako kwa kupiga kura. Zimebaki siku sita za kupiga kura. Swali ni hili; Je, ni nani ataibuka kidedea Igunga? Piga kura juu kulia kwenye http://mjengwa.blogspot.com
Saturday, 3 September 2011
17:19
Unknown
Gaddafi, JAKAYA KIKWETE, WIKILEAKS
5 comments
Kwa sasa nitaiwasilisha kama ilivyo lakini naahidi kuifanyia tafsiri ya Kiswahili baadaye leo.
Viewing cable 06DARESSALAAM277, KIKWETE CORRUPTION TIDBIT
If you are new to these pages, please read an introduction on the structure of a cable as well as how to discuss them with others. See also the FAQs
This record is a partial extract of the original cable. The full text of the original cable is not available.
C O N F I D E N T I A L DAR ES SALAAM 000277 SIPDIS DEPT FOR INR, R.EHRENREICH E.O. 12958: DECL: 02/13/2016 TAGS:
PGOVPRELTZSUBJECT: KIKWETE CORRUPTION TIDBIT Classified By: Ambassador Michael Retzer, Reason 1.5 (d) ¶1. (C) President Kikwete has accepted gifts (bribes) from the owner of the Kempinski Hotel chain,s Tanzanian properties, a citizen of the United Arab Emirates. ¶2.
(C) In a conversation with the manager and the publicity director of Dar Es Salaam,s Kilimanjaro-Kempinski Hotel hours after accompanying A/S Frazer to her October 18, 2005 meeting with then-Foreign Minister Kikwete, I commented on Kikwete's flashy attire, asking "Who dresses him?" "We do," they responded. Initially thinking this meant Kikwete frequented a men,s shop in the hotel, I learned later in the evening from hotel publicity director Lisa Pile (protect) that the hotel owner*UAE citizen Ali Albwardy*had recently flown Kikwete to London for a subsidized shopping expedition.Among other things, on that trip Ali Albwardy bought Kikwete five Saville Row suits. He had also recently made a $1 million cash contribution to the CCM (which is a legal contribution under current Tanzanian law). ¶3.
(C) Pile told me the Kempinski Hotel chain is greatly expanding its presence in Tanzania. She said that in December it would open "the best hotel in Zanzibar." Her prediction was a little off; the new Kempinski hotel, located on the beach on Zanzibar,s east coast, opened January 5. I attended the opening ceremony along with Zanzibari President Karume, who was asked publicly by Ali Albwardy for a site in Stone Town to build a new hotel. Later that day, Pile revealed that the Zanzibar government had already earmarked for Ali Albwardy a hotel site in Stone Town. ¶4.
(C) Pile also said in the October 18 conversation that Ali Abwardy was about to receive the rights to construct two new hotels on the mainland: one on the edge of Ngorongoro Crater and another on the Serengeti plain overlooking the main animal migration routes. Stringent conservation rules currently ban the construction of permanent structures inside national parks*including in the crater and on the Serengeti plain*but Pile said that in November legislation would be introduced to parliament to authorize the new hotels.
(Comment: We have received no reports on new legislation, but the Dar Es Salaam Daily News on January 15 reported that the Tanzania National Parks Authority had approved construction of a five star hotel on the Serengeti plain.) ¶4.
(C) Later on October 18, over dinner, an Indian/South Asian man described as a business associate of Ali Albwardy briefly took Pile from the table for a conversation in Kiswahili. I am not sure what was said, but Kikwete's name came up several times and he passed her an envelope. Pile told me the envelope was stuffed with 1 million shillings ( $1,000) and was to pay for a Kikwete meeting at the Kilmanjaro-Kempinski later that month. Apparently Kikwete is a regular customer, but no name ever appears on the hotel registry when a government bigshot has an "event" in one of the guest rooms. ¶5.
(C) Bio Note: Lisa Pile, an Australian citizen, has lived in Dar working for Kempinski Hotels since early 2004. Before that she had served in a similar capacity with the Kempinski chain in China. Her family in Australia is prominent in Australia's Liberal Party (the center-right party of Prime Minister John Howard). ¶6.
(C) Comment: What does it all mean? I don,t know, but my guess is that the investor Ali Albwardy has access to oil money out of the UAE. I suspect giving free clothes and the campaign donation is just the way these people do business. ¶7.
(C) For his part, Kikwete probably thinks having all these five star hotels around is a good idea for the country,and I agree with him. His new minister of Natural Resources and Tourism, Anthony Diallo, says he wants to double tourism,s contribution to the national economy in ten year,s time. Kikwete probably believes there is no harm in taking these "little gifts" to do what he would have been inclined to do anyway. That said, they are what they are: bribes.
Thursday, 1 September 2011
Mawaziri wa kiume nchini Zimbabwe wapo mbioni kutahiriwa kama sehemu ya mkakati wa serikali ya nchi hiyo kuhamasisha njia hiyo inayoaminika kupunguza maambukizi ya Ukimwi.
Tafiti zinaonyesha kuwa tohara kwa wanaume inasaidia kupunguza uwezekano wa maambukizi ya Ukimwi (wakati wa tendo la ndoa) kwa takriban asilimia 60.Hata hivyo,wataalamu wa tiba wanaonya kuwa tohara hiyo sio njia mbadala ya hatua nyingine za kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.
Zimbabwe ilianzisha kampeni kubwa mwaka juzi ikiwalenga angalau wanaume milioni 1.2 katika jitihada za kupambana na maambukizi mapya ya ugonjwa huo.
Vituo vinavyoendesha zoezi hilo vimeeleza kuwa watu wengi wamekuwa wakijitokeza na wanaonyesha kukubaliana na hatua hiyo.
Lakini sasa kuna mpango wa kuwalenga wanasiasa wa ngazi za juu ikiwamo mawaziri,wabunge na madiwani ili nao watahiriwe.
Naibu Waziri Mkuu Thokozani Khupe ameeleza kuwa hatua hiyo inaendana na mkakati wa serikali kupambana na Ukimwi.
"Utafiti umeonyesha kuwa wanaume waliotahiriwa wana nafuu ya maambukizi ya Ukimwi pungufu kwa mara nane,na kama viongozi serikalini tunapaswa kuongoza kwa kuonyesha mfano ili tunaowaongoza watambua umuhimu na faida ya tohara," Khupe alilieleza gazeti la Sunday News la Bulawayo.
"Lengo letu ni kuwa na vifo sifuri kutokana na Ukimwi.Tunaweza tu kufanikiwa iwapo viongozi wataonyesha mfano.Watu wanapaswa kuelewa kuwa Ukimwi upo na haipaswi kudhani kwamba kuzungumzia tohara ni mwiko."
Zimbabwe ni moja ya nchi zilizoathiriwa vibaya sana na janga la Ukimwi huku kiwango cha maambukizi kikiwa miongoni mwa vikubwa zaidi duniani.
Hata hivyo,kiwango cha maambukizi kimepungua kwa kasi,takriban kwa nusu kutoka asilimia 29 ya Wazimbabwe wote mwaka 1997 hadi kufikia asilimia 16 mwaka 2007.
Watafiti wanaeleza kuwa wananchi wameanza kukubali kubadili tabia za ngono kutokana na kukua kwa uelewa kuhusu vifo vinavyotokana na Ukimwi na hofu ya kuambukizwa virusi vya ugonjwa huo.
"Nchi chache sana duniani zimeshuhudia kupungua kwa maambukizi,na katika Afrika,Zimbabwe ilionekana kama sio rahisi kumudu kupunguza maambukizi," Simon Grason wa chuo cha Imperial jijini London alieleza katika ripoti ya hivi karibuni.
CHANZO: Nimetafsiri habari hii kutoka gazeti la New Zimbabwean (bonyeza kiungo kuisoma katika lugha ya Kiingereza)
20:18
Unknown
Ndondi, Super D
No comments
Kocha wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila (Super D) kushoto akitangazwa mshindi zida ya bondia Safari Berdard kipindi hicho |
Super D Boxing Coach kushoto Akipambana na Rashidi Ali |
Super D Boxing Coach kulia akipambana na Ajibu Salumu |
Salam alykum kaka kwenye maktaba yangu ya picha nimekutana na picha hizo kaka si vibaya ukawakumbusha bondia machachari aliekuwa anasimamisha mashabiki vitini awapo ulingoni asante kwa ushirkiano wako tupo pamoja
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
Mob;+255787 406930
Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania
--
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
Mob;+255787 406930
+255774406938
Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania
- superd vs ajibu.JPG
- super d vs rashid ali.JPG
- super d ushindi.JPG
Na Nova Kambota,
Namkumbuka mwanamuziki wa kizazi kipya Seleman Msindi maarufu kama Afande sele na kile kibao chake cha “Darubini kali” anapohoji “kama unapenda pepo kwanini uogope kifo?”
Tungo hii kwa namna ya pekee inamgusa waziri mkuu wa Tanzania Mh Mizengo Pinda maarufu kama “mtoto wa mkulima” ndiyo namuuliza Pinda ataonaje pepo pasipo kufa kwanza?
Tangu kuteuliwa kwake mara baada ya Edward Lowassa kujiuzulu, Kwa wale wanaomjua Pinda walishasema kuwa “Pinda atapwaya sana”, sasa ikiwa ni takribani miaka mitatu na nusu tayari mambo hadharani kuwa Pinda “kashindwa kazi”
Kwa wasiomjua Mizengo Pinda tafuteni ukweli mtamjua tu, ni Mizengo Pinda huyu amebaki kuwa mshauri wa Kikwete badala ya waziri mkuu kufikia hatua ya kutamka bungeni kuwa hana mamlaka, ni Pinda huyu asiye na makundi lakini anakubali kumezwa na mitandao na makundi ya CCM na bosi wake Kikwete na sasa nimeanza kusikia watu wakimwita ni “mtoto wa mkulima anayeishi kibilionea”
Hakuna ubishi kuwa hata watetezi wachache wa Pinda waliobaki sasa wamefadhaishwa na udhaifu wake kama sio uwoga wa kupindukia, “jeuri” ya Luhanjo na sakata la Jairo limemwaka njia panda Mizengo Pinda, amebaki kujiumauma na kutapatapa tu, kadhalilishwa lakini hataki kuchukua hatua, katukanwa lakini anachekelea! Huyu ndiye Mizengo Pinda.
Waziri mkuu Pinda akiongelea sakata la Jairo akajiapiza kuwa angekuwa na mamlaka angemfukuza kazi Jairo kwa maana nyingine Pinda amekiri kuwa Jairo anastahili adhabu na serikali haikutaka kumwangusha waziri mkuu “ikamtwanga likizo ya malipo” Bw Jairo lakini ghafla katibu mkuu kiongozi anaibuka na kumdhalilisha waziri mkuu eti Jairo hana kosa arudi kazini, wakati Pinda akisita kuchukua hatua wabunge kwa umoja wao wameamua kumtetea waziri mkuu kwa kudhalilishwa sasa Bunge limeunda kamati.
Hivi katika mduara huu wa “kudhalilishana na kushushiana heshima” ipi nafasi ya Pinda? Yapi maamuzi ya Pinda? Kichekesho ni kuwa Pinda “yupoyupo tu” hajachukua uamuzi na dalili zinaonyesha kuwa kwa mara nyingine tena Pinda amekubali kupiga magoti na kujishusha sehemu aliyotakiwa apigiwe magoti yeye huyu ndiye Pinda ambaye bilashaka hata “ukimpiga ngumi” yeye wakati wa kukurudishia lazima atavaa gloves ili asikuumize.
Pinda anataka pepo? Anataka watanzania tumkumbuke kuwa ni kiongozi jasiri? Basi hana budi kufa ili aione hiyo pepo! Naam amedhalilishwa sana, ameshushiwa hadhi yake, na sasa ni wakati wayeye kufikiria kujiuzulu.
Haiwezekani Luhanjo na Pinda waendelee kuitumikia serikali moja, hiki kitakuwa ni kiinimacho , ni lazima mmoja wao atoke, na kwa vile wote tunakubaliana Pinda anaitamani pepo, anataka kukumbukwa mioyoni mwa watanzania, lazima aachane na serikali hii ya akina Luhanjo na Jairo, hana budi kumwachia Kikwete ateue waziri mkuu mwingine ambaye atakubali kuvunjiwa heshima, Naam! Pepo haiji hivihivi, ni lazima Pinda afe leo ili aione pepo kesho!
Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
Tanzania, East Africa,
Alhamisi, September 1, 2011.
Subscribe to:
Posts (Atom)