Monday, 17 November 2008

Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara mkoani Kilimanjaro (MUCCoBS) kimewatimua wanafunzi 595 wa mwaka wa kwanza kutokana na kuanzisha mgomo chuoni hapo. 

Aidha wanafunzi hao pamoja na mgomo huo,wametuhumiwa pia kuhatarisha maisha ya baadhi ya wanafunzi wenzao wa mwaka wa pili na wa tatu sambamba na wahadhiri chuoni hapo baada ya kuwamwagia mchanga na kuwarushia mawe wakiwa darasani. 

Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Suleiman Chambo alisema jana kuwa kutokana na mgomo huo, menejimenti iliamua kuwasimamisha masomo wanafunzi hao kwa muda usiojulikana na umewataka wawe wameondoka chuoni hapo hadi kufikia jana saa 10 jioni. 

"Wanafunzi wa mwaka wa kwanza walipoona wenzao wa mwaka wa pili na tatu hawawaungi mkono waliamua kuwafuata madarasani na kuwamwagia mchanga na kuwarushia mawe huku mhadhiri mmoja akiwa darasani, Profesa Temba, ambaye alinusurika kipigo na ilimbidi kuingia chini ya meza ili kujinusuru," alisema. 

Aliongeza kudai kuwa wanafunzi hao hawana madai ya msingi na kwamba moja ya madai yao ni kuishinikiza Serikali kuwalipia mikopo kwa asilimia 100 huku madai mengine ni kuwaunga mkono wanafunzi wenzao katika vyuo vikuu vilivyofungwa. 

"Tumeamua kuwarudisha nyumbani kwa muda usiojulikana, na wakirudi waandike barua wathibitishe kulipa ada kwa asilimia 100, waombe kurudi chuoni na kufuata taratibu za chuo na walete vyeti vya kuonesha kwamba wana sifa za kurudia shahada wanayosomea," alisema. 

Alidai kuwa wanafunzi hao pia walitishia maisha ya Rais wa Serikali ya wanafunzi chuoni hapo, Zamu Mlimila ambaye alilazimika kuokolewa na polisi baada ya wanafunzi kumzonga kwa lengo la kumshinikiza atangaze mgomo chuoni hapo.

CHANZO: Majira

Picha (ni kielelezo tu,haihusiani na habari) kwa hisani ya MJENGWA

WALIMU wanaofundisha katika shule zilizopo wilayani Monduli mkoani Arusha ambao waliajiriwa toka Julai mwaka huu, wapo katika hali mbaya kimaisha kiasi cha kufikia hatua ya kufanya kazi za kugonga kokoto ili kujikimu kimaisha.

Hali hiyo imetokana na walimu hao kutolipwa mishahara yao ya miezi zaidi ya minne toka waajiriwe, licha ya kusaini mkataba wa miaka mitano.

Uchunguzi wa kina uliofanywa na Tanzania Daima, umebaini kuwa walimu walioathirika kwa kiasi na hali hiyo ni waliopo katika maeneo ya Loolkisare, Moita, Meserani Juu, Mto wa Mbu, Losomingo na Lepulko ambapo inadaiwa walimu hawana hata nauli ya kuwafikisha katika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli.

Akizungumza na Tanzania Daima, mmoja wa walimu hao, Goodluck Namoyo, alisema hali zao ni mbaya kifedha na wanajiandaa kukutana leo ili kujadili hatma yao.

Katika maeneo mengine ya Loolkisare na shule zilizopo vijiji vya mbali walimu wanaingia darasani kwa muda mfupi na muda mwingi wanatumia kufanya kazi za vibarua kwa kugonga kokoto ili kuwawezesha kupata angalau fedha za kujikimu.

Kaimu Afisa Elimu wa wilaya ya Monduli Emanueli Maundi, alikiri kuwepo kwa hali hiyo na kuongeza kuwa walimu 40 hawajalipwa mishahara yao mpaka sasa na wao kama idara ya elimu, wamefanya jitihada kunusuru hali hiyo.

''Ndugu yangu mwandishi hivi tunavyoongea licha ya mweka hazina kuwasilisha majina ya walimu hao wizarani kwa muda mrefu sasa, hali bado ni tete na imemlazimu afisa elimu hiyo kwenda jijini Dar- es- salaam kushughulikia mishahara ya walimu hao kwani wana hali mbaya sana hivi sasa,'' alisema Maundi.

Naye katibu wa chama cha walimu wilaya za Monduli na Longido Godwin Mushi, alisema hali ya walimu hao inadhihirisha ni jinsi gani walimu hawathaminiwi kwani toka waajiriwe, hawajalipwa.

''Sidhani kama mwalimu huyo anaweza kumshauri ndugu yake yoyote apende kuwa mwalimu kutokana na hali aliyokumbana nayo yeye hivi sasa na hali hiyo ni hatari zaidi kwa siku za baadaye juu ya mustakabali wa elimu nchini, ''alisema Mushi.

Akizungumzia hali hiyo Mkaguzi wa Elimu wa Wilaya ya Monduli, Ernest Mwende, alisema kazi ya walimu kwa sasa ni ngumu kutokana na kupungua kwa thamani ya mwalimu.
CHANZO: Tanzania Daima

CLICK HERE to read the story.


Universities are being asked to set up surveillance units to monitor the movements of international students in a government-led crackdown on bogus student immigration scams, academics say. New rules to force universities to report overseas students who miss too many lectures to immigration officers will harm the academic-student relationship because lecturers are being asked to act in a "police-like" manner, according to a group of 200 academics and activists opposing the moves.

A letter to the Guardian, organised by Ian Grigg-Spall, academic chair of the National Critical Lawyers Group and signed by leading academic lawyers, the head of the lecturers' union and Tony Benn, claims that the rules could breach the European convention on human rights, which guarantees the individual's right to privacy. "This police-like surveillance is not the function of universities and alters the educational relationship between students and their teachers in a very harmful manner," it says. "University staff are there to help the students develop intellectually and not to be a means of sanctioning these students."

The rules will require all universities to obtain a licence to admit students from outside the EU. They will then have to sponsor students, who will be required to have their fingerprints taken and be issued with ID cards. Lecturers will have to report any student who misses 10 or more lectures or seminars. Students will also have to prove they have funds to cover fees plus £800 a month for the duration of their courses. Universities have separately raised concerns that the system of registering overseas students, which is planned to take place at six centres around the country, will struggle to cope.

About 350,000 overseas students attend British universities every year. Universities are heavily dependent on the £2.5bn a year they pay in fees.

Almost 300 bogus colleges have been uncovered in the past three years, many involved in immigration scams.

Sally Hunt, general secretary of the University and College Union, said: "We have grave concerns that new rules on monitoring foreign students have been pulled together without any consultation with the people who would implement them. We do not believe it is appropriate or effective to task colleges and universities with the policing of immigration."

A Home Office spokesman said: "Those who come to Britain must play by the rules and benefit the country. This new route for students will ensure we know exactly who is coming here to study and stamp out bogus colleges who facilitate the lawbreakers.

"International students contribute £2.5bn to the UK economy in tuition fees alone. The student tier of the points system means Britain can continue to recruit good students from outside Europe."

SOURCE: The Guardian

Sunday, 16 November 2008


*Wajipanga kuanika siri zote hadharani
*Vocha za malipo kwa CCM kuanikwa
*Kapt. Chiligati awakana, naye awatisha
*Asisitiza hakuna kikao kilichowatuma

Na Mwandishi Wetu 

BAADHI ya watuhumiwa wa ufisadi kwenye Akaunti ya EPA iliyokuwa Benki Kuu (BoT) sasa wameamua kuitisha Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, uchunguzi wa Majira umebaini. 

Kitisho hicho kimekuja kufuatia baadhi yao kukamwatwa na kufunguliwa kesi mbalimbali za jinai huku ikionekana kuwa wao walikuwa mawakala tu katika kupitisha fedha hizo na vigogo husika wakiwa nje. 

Chanzo chetu kilicho karibu na baadhi ya watuhumiwa hao kilieleza kuwa kukamatwa, kufunguliwa mashitaka kumewadhalilisha sana baadhi yao huku wakiumia zaidi kwa kusota rumande, kwenye gereza la Keko na wale wanawake wakiweka Gereza la Wanawake Segerea. 

"Jamaa ameumia sana rohoni, hata kuhangaikia dhamana alisita mwanzo baada ya kuona kwa nini ahangaike kutoa mali zake, wakati alikuwa wakala tu," kilisema chanzo chetu kilicho karibu ni mmoja wa watuhumiwa waliokwisha funguliwa kesi na akasota sana kwenye gereza la Keko. 

Ingawa Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kikikana mara kadhaa kuhusika kunufaika na fedha hizo katika chaguzi mbalimbali, duru za uchunguzi, zinawakariri baadhi ya watuhumiwa hao wakilalamika 'kutolewa kafara.' 

Ndugu mwingine wa mtuhumiwa ambaye ameshafanikiwa kwa kiasi kikubwa kulikwepa sakata la EPA, ingawa taarifa za kiuchunguzi bado zinaamini huenda akaburutwa naye kortini, aligusia kuwa kwa sababu yeye alitumiwa tu, ameandaa faili la utetezi ambalo pamoja na nyaraka nyingine, limeheheni kile alichokitaja kuwa vocha za malipo kwenda kwa baadhi ya vigogo wa CCM. 

"Hapa ndipo Serikali itakapoumbuka. Kila kitu kipo. Hajakamatwa bado, ameshahojiwa na kubanwa katika shughuli zake, anasubiri tu afikishwe kortini atoe vielelezo vyake, yeye si fisadi, aliombwa asaidie shughuli halali akafanya hivyo, kwa namna anavyojiheshimu, asingeweza kusaidia akakubali wizi," kilisema chanzo chetu kilicholiona faili hilo la utetezi. 

Wakati watuhumiwa hao wa EPA wakijipa 'kujiondoa katika ukafara,' Mwandishi Wetu Eckland Mwaffisi anaripoti kuwa uongozi wa juu wa CCM, umeendelea kusisitiza kuwa hawahusiki na ufisadi wa EPA. 

Akitoa tamko kwa niaba ya Chama chake Dar es Salaam jana, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, Bw. John Chilligati, alisema CCM haikuhusika na wizi huo kama ilivyodhibitishwa na ripoti ya kamati ya wanasheria. 

Alisema pamoja na madai yanayotolewa na viongozi wa vyama vya upinzani, pasipo kuthibitisha madai hayo, CCM haikuchukua fedha hizo wala haikumtuma mwanachama wake au mkereketwa yoyote kwenda kuchukua fedha hizo katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT). 

Bw. Chilligati alisema pamoja na orodha ya watuhumiwa wa EPA kuhusisha majina ya wanachama wa CCM ama Wakereketwa, Chama hakijahusika kumtuma bali ni kitendo cha mtu binafsi. 

Hadi sasa miongoni mwa waliokamatwa kwa tuhuma za wizi wa fedha za EPA wanaohusishwa na ukaribu na vigogo wa CCM au kuwa makada ni Bw. Rajabu Maranda na mfanyabiashara, Bw. Jeetu Patel. 

"Kwenye ukweli, uongo hujitenga, madai yote ya kuihusisha CCM na ufisadi wa EPA ni uongo wenye nia ya kukivunjia heshima chama chetu machoni mwa jamii pamoja na hila za kuchafua jina la chama zinazofanywa na wapinzani ambazo kamwe, hazitafanikiwa," alisema Bw. Chilligati. 

Kutokana na hali hiyo, Bw. Chilligati aliongeza kuwa, baadhi ya wanachama wanaokiuka maadili hayo, isichukuliwe kwamba wanatumwa na vikao vya chama bali ni vitendo vyao binafsi na watachukuliwa hatua za kisheria na vyombo vya dola kama ilivyo kwa wahalifu wengine. 

Alisema CCM, inapongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hatua alizozichukua katika kushughulikia sakata hilo. 

Hadi wiki inayoanza leo, ambapo zipo tetesi za watuhumiwa zaidi kuanza kufikishwa kortini huku Mkurugenzi wa Mashitaka ya Umma (DPP), Bw. Eliezer Feleshi akikiri kuwa bado kuna mafaili yanapitiwa, idadi ya watuhumiwa waliokwishafikishwa kortini ni 20. 

Baadhi ya makampuni ambayo yameshafikishwa mahakamani ni pamoja na Money Planners, Kiloloma & Brothers, Njake Hotel, Rashhas, Mibare Farm, Changanyikeni, Bencon International, Kernel, Malta Mining, Navy Cut Tobacco na BC Grassel & Company. 

Makampuni yanayosubiriwa kwa hamu na wananchi katika Mahakama ya Kisutu ni pamoja na kampuni ya Kagoda ambayo inadaiwa kuchota fedha nyingi kulikoni kampuni nyingine.

CHANZO: Majira

T.I ft Rihana-Live Your Life

Eminem-Stan

CAUTION:Explicit lyrics.50 Cent-If I Cant

CAUTION: Explicit Lyrics.The Street-Blinded by the Lights

Skinnyman-Council of Estate Minds

2 Pac ft Danny Boy-I Aint Mad At Cha

Luniz-I Got 5 On It

The Fugees- Fu-Gee-La

Jay Z-Hard Knock Life

Nas-I Can

Photo courtesy of MICHUZI

From the outside, the highly protected Maximum Prison, located in the southern part of Dar es Salaam, could easily be mistaken for a Toyota showroom on weekend days. 

But the compound is not a showroom. It is the current home of 13 EPA suspects who have so far spent about ten days in the tiny prison's cells, since they were arrested last week. 

Behind these highly fenced and protected walls are men who were busy men who negotiated lucrative business deals over their sophisticated mobile phones, in fabulously furnished offices or in the restaurants of the city`s expensive hotels. 

Their arrests and prosecution last week changed their lifestyles suddenly and dramatically. 

One close family member of the prominent tycoon Jeetu Patel hinted to our reporter in the prison compound: ``Boss doesn`t believe what is happening,he feels he has been betrayed by his allies in the government.`` 

The person, who spoke on condition of anonymity last Sunday, explained further: ``He was extremely shocked on the day he entered prison, but he says he has surrendered his fate to the almighty God.`` 

For some, it has been a dream shattered by their sudden arrest, but for others it has been a time for short vacation after spending months on the streets of Dar es Salaam, trying to make ends meet. 

Their life hasn't changed much, though their freedom to move and mix with their buddies and families have been terminated, as they spend their nights and days at the Prison, pending the fate of their bail applications. 

According to a week-long survey conducted by The Guardian on Sunday, despite being locked behind bars, some suspects are still managing their businesses from the prison. 

``Each passing day the businessman signs several cheques amounting to millions of shillings. 

It is business as usual, the only difference being that it is being conducted in a prison cell instead of an office,`` one senior prison official who declined to have his identity disclosed, revealed. 

In what shows the smugness of money on Sunday, the Prison`s parking yards is full of posh cars as relatives and friends gathers here to see the EPA suspects. 

Inside prison however, some of them are enjoying a relatively good lifestyle compared to their fellow inmates, one of the aspects of which is the allowance for accessing food from outside, while ordinary inmates scramble for the little, unpalatable official variety. 

And to make life easier, some of the suspects reportedly spend much time in sickbays reserved for ailing inmates. 

It is being speculated, also, that confining the suspects to the sickbays is a deliberate security measure intended to protect them from attacks by ordinary remandees who may be infuriated by the EPA scum. 

``The way they are being treated is quite different from other prisoners,`` the official said. 
One of two brothers charged in the case remarked openly to prison warders: `It is a relief for me to stay away for sometime from the taxing business engagements. Two weeks here will do me some good.`` 

Sunday is a hectic day for prison warders, as they have to cope with hundreds of well-wishers of the EPA suspects. 

``I have never experienced such a situation since I became a warder ten years ago,`` one of them remarked. According to the Prisons regulations, visitors are allowed to see their relatives on Sundays. 

Security 

Alarmed by the prominence of the EPA suspects- considering that most of them are powerful financially who can even buy their way out-on Tuesday this week, strategic measures to improve security were taken by the government. 

Assistant Commissioner of Prisons Mtiga Omari, fearing a recurrence of the early 1980s when some treason trial suspects escaped from the prison, said effective from this mid-week all visitors of the EPA suspects must secure special permission from the Prisons Department Headquarters. 

``These suspects hold financial power which can easily corrupt some of our `weak` people. 

To play it safe, anyone seeking an audience with the suspects must get a permit from us,`` said Mtiga who incidentally overheard a group of people at Kisutu Court area joking that ``the police have taken theirs, it is now the turn of the judiciary to take theirs.`` 

The relatives or friends must give in writing their identities, the EPA suspects they want to visit and the reasons behind such visits to satisfy the Commissioner for Legal Affairs and Administration. 

This will also help in keeping track of them, he explained. 

``We are careful. Some of these persons are top executives in local and international businesses, others in high positions in the Bank of Tanzania, while some are decision-makers in companies involved in the scandal,`` Mtiga said. 

``Their offices may need them for some reasons or other.`` 

ACP Mtiga said the issue of segregating EPA suspects from other remanded prisoners at Keko or Segerea is the discretion of the Principal Commissioner of Prisons, although he dismissed any favouritism.



Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget