Watawala wetu waache magari yao ya kifahari wachekwe?Nchi tajiri lakini viongozi wanaishi kawaida,lakini sie masikini na ombaomba wa kutembeza bakuli viongozi wetu wanaishi kifahari kama wafanyabiashara matajiri.
Tuesday, 18 May 2010
13:45
Unknown
DAVID CAMERON
2 comments
Watawala wetu waache magari yao ya kifahari wachekwe?Nchi tajiri lakini viongozi wanaishi kawaida,lakini sie masikini na ombaomba wa kutembeza bakuli viongozi wetu wanaishi kifahari kama wafanyabiashara matajiri.
Ofkoz,Mtukufu Rais Jakaya Kikwete alikuwa anatania alipotetea rushwa hadharani kwa kudai takrima haikwepeki.Ndio,Rais alikuwa anatania,na ndo maana,Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa amekaririwa na magazeti kadhaa akimtetea JK kuwa "kauli yake (JK) kuhusu takrima (rushwa) ilikuwa utani tu".Pengine neno 'utani' kwa mujibu Tendwa linaweza kuwa na maana kubwa zaidi tukilitafsiri katika informal English.Kwenye kamusi,'joke' (informal) inamaanisha An object of amusement or laughter; a laughingstock.Kwa Kiswahili,ni 'kituko', 'kioja' au 'kitu cha kuchekwa'.
Lakini kwa namna siasa zetu zilizvyojaa vituko (jokes) si ajabu Tendwa alikuwa serious kumtetea bosi wake JK.Na inawezekana kabisa Msajili huyo wa Vyma vya Siasa anayepaswa kufanya kazi bila upendeleo anaamini kwa dhati kuwa rais wetu alikuwa anataniana tu na viongozi wa dini.Kama ni hivyo,basi nae ni kituko pia.Haiingii akilini kwa kiongozi wa nchi kukutana na watu muhimu katika jamii yetu (viongozi wa dini) na kufanya 'utani mbaya' kama huo.Kulikuwa na umuhimu gani basi wa rais kuhudhuria mkutano huo kama lengo lilikuwa kutoa utani tu?Si angeweza kuwapigia simu kwa wakati wake kisha akawarushia utani huo!
Kwa bahati mbaya,au makusudi,'utani huo mbaya' ushaanza kusahaulika miongoni mwa Watanzania wengi.Siwezi kuwalaumu walalahoi ambao wako bize na kuhakikisha mkono unaenda kinywani,lakini nashindwa kujizuia kuwashangaa Watanzania wenzetu walio katika 'tabaka la kati' (middle class) kwa kuweka umuhimu zaidi kwenye ishu kama tuzo za Kili,ujio wa Sean Kingston,'kujirusha',nk ilhali tabaka la chini linalohitaji sapoti yao likizidi kuangamia.Wengi wa walio katika tabaka la kati wako bize zaidi 'kuishi kama tabaka tawala' (hata kama hiyo itamaanisha wakope kwa ndugu na marafiki au wajihusishe na ufisadi) kuliko kupambana na 'tabaka tawala' (tabaka la juu) 'kusawazisha uwanja' (to level the ground) kwa minajili ya kujenga jamii yenye kukaribia usawa.
Sijui tunaelekea wapi,lakini lililo bayana ni kwamba hatma ya taifa letu iko mashakani.Ukiona mkuu wa nchi anaongea pasi hofu (na kicheko juu,kama kawaida yake) kuwa takrima (ambayo ni jina la kistaarab la rushwa) haikwepeki.Tafsiri pana ya kauli hiyo ya 'Chaguo la Mungu' ni mithili ya kuhalalisha uhalifu kwa vile rushwa ni kosa la jinai.Lakini binafsi sishangazwi sana na kauli hiyo ya 'mwenye nchi' kwa vile alishawahi kutamka bayana kuwa 'anajali haki za binadamu za mafisadi' alipohutubia Bunge Agosti mwaka 2008
Kusoma habari kamili kuhusu utetezi wa Tendwa kwa Kikwete BONYEZA HAPA na HAPA.
Sunday, 16 May 2010
Saturday, 15 May 2010
18:52
Unknown
None
2 comments

It's been quite a while since our Dear leader Jakaya Mrisho Kikwete last visited the United Kingdom.As a seasoned world traveller,and in the spirit of the Anglo-Tanzania friendship,I suspect JK will be here sooner than later.And in an effort to maintain his record as the first African president to meet Barack Obama,he certainly could be here in a matter of weeks if not days.
Just because you poor souls can't afford to visit other areas in Tanzania either because the fares are too dear,or your intended destinations are inaccesible due to TRL taking a long break from serving walalahoi,or simply because you're scared of dying after looking closely at the growing figures of road accidents (and subsequent deaths) doesn't mean our Dear leader,God's choice,JK should not continue to 'accumulate his international air miles'.
Yes,as Basil Pesambili Mramba once said,a president cannot travel on top of a camel.Of course,he was not really defending that infamous decision to buy a rarely used Presidential jet but rather the dough on its way to his own bank account.
Satiric or not,truth remains that our leaders are so distant from the led that they hardly understand why people keep on complaining about one thing or another.It goes without saying that if Dr Shukuru Kawambwa were to be stranded at a train station for just a couple of hours due to the TRL bullshit,he surely would understand how it affects walalahoi.And if JK trips were to rely on ATC,he certainly would have thought the importance of having a 'living' national carrier (ATC is long dead except for the name and the likes of Mustafa Nyang'anyi who make most of what's left of the corporation).
It's down to such distance that,for instance,our God-sent president came to the decision to order DCs to carry out house house-to-house searches to 'catch' kids who didn't up to schools despite having been selected to join secondary education.Assuming the searches pay dividents,would the militias acting on powers invested to them by the DCs be turning up at the 'truant' kids' homes day in day out to force them to go to schools?Did His Excellency Jakaya do any brainstorming as to why these kids chose to abscond school in the first place?They certainly are not allergic to education,or are they?Would it still chasing these kids deemed necessary had the much-hyped 'secondary school in every ward' corresponded with number of desks for students,housing and salary on time for teachers,and such logistical considerations?Although I truly understand the importance of education,I think this misguided directive should rather target owners of Kagoda and their fellow mafisadi than our innocent kids.
I know the privileged fews whose hands are superglued to the national cake would regard this article as being seditious.Whatever!That's all I can tell them.
Kwa hakika baadhi ya kauli za Rais wetu Jakaya Kikwete zinachanganya kupita kiasi.Juzijuzi tu alisaini kwa mbwembwe sheria tuliyoambiwa imelenga kudhibiti rushwa katika chaguzi.Tukiweka kando suala la wasaidizi wake kumwingiza mkenge kwa kuchomekea vipengele kinyemela,sambamba na mapungufu lukuki katika utekelezaji wa sheria hiyo (kubwa likiwa uswahiba kati ya CCM ya Kikwete huyohuyo na mafisadi),uamuzi wa kuwa na sheria hiyo ulileta faraja kidogo kwamba angalau mkuu wa nchi sasa anaanza kuikabili rushwa kwa vitendo badala ya maneno na ahadi tupu.
Sasa kabla hata sheria hiyo haijapata nafasi ya kutumika ipasavyo,JK kaja na hadithi mpya.Kwa mujibu wa vyombo vya habari,Rais amewaeleza viongozi wa dini kuwa suala la takrima kwenye chaguzi ni gumu kulidhibiti.Kama huelewi vizuri maana ya takrima basi naomba nikugamishe kuwa hiyo ni jina la kistaarabu (polite name) la rushwa au hongo wanayotoa wagombea kwa kisingizio cha 'ukarimu'.
Kinachonifanya nishindwe kumuelewa JK ni hiki: ina maana wakati anaipigia chapio sheria anayoamini itadhibiti rushwa kwenye chaguzi alikuwa hafahamu kuwa takrima (ambayo ni rushwa) ni ngumu kudhibitiwa? Au tuseme JK haamini kuwa takrima ni rushwa na ndio maana iliharamishwa?Na je kama takrima ni ngumu kudhibitiwa kwahiyo inakuwa halali?Je kiongozi wetu huyu haoni kuwa mkanganyiko anaozua unaweza kupelekea mvurugano baada ya uchaguzi ambapo wagombea watakaoshindwa kutokana na uwezo wao duni kumudu kutoa takrima wakikimbilia mahakamani,watoa rushwa (takrima) watatumia kauli ya JK kuhalalisha kuwa walichofanya ni sehemu ya utamaduni wetu wa ukarimu ("kama alivyobainisha Rais tarehe 14/05/2010)?
Habari kamili kuhusu kauli hiyo ya JK soma HAPA na HAPA.
Subscribe to:
Posts (Atom)