Wednesday, 2 June 2010

Kwa mujibu wa imani zetu za Kiswahili,aliyekuroga akifariki basi uwezekano wa kupona nao unakuwa kama umefariki.Na msemo huu unaonekana kurandana na hali halisi ya baadhi ya matendo yetu viumbe tunaojulikana kama Watanzania.Nafahamu kuwa si wote "tuliorogwa" lakini hiyo si sababu ya "kutowatolea macho" wenzetu "waliorogwa kisha aliyewaroga akafariki".

Mwishoni mwa wiki hii,timu yetu ya taifa inakabiliwa na mpambano muhimu dhidi ya timu ya taifa ya Rwanda katika kusaka nafasi ya kushiriki kwenye michuano ya CHAN.Taifa Stars inatarajiwa kucheza siku ya Jumapili kisha Jumatatu wanatarajiwa kuingia tena uwanjani kupambana na timu ya Taifa ya Brazil katika pambano lililonunuliwa kwa mamilioni ya dola na chama chetu cha soka.

Na kwa takriban wiki nzima sasa,uongozi wa FA umekuwa bize zaidi na maandalizi ya pambano hilo walilonunua kuliko kuelekeza akili zao kwa mpambano dhidi ya Rwanda.Japo natambua kuwa kila mpenzi wa soka duniani angependa kuiona Brazil ikicheza uwanjani lakini sio kwa kununua mechi ya mamilioni ya fedha ambazo hakuna uhakika kama zitarudi.FA hawajaweka bayana gharama za kununua mechi hiyo lakini taarifa zinasema wamelipa dola za kimarekani milioni mbili unusu  (zaidi ya shilingi bilioni 3 unusu).Na hiyo ni ada (fee) tu lakini kuna uwezekano wa kiwango hicho kuwa kikubwa zaidi tukichanganya na gharama za kumudu ziara hiyo.

Kuna hoja kuwa ziara hiyo itasaidia kutangaza utalii.Well,lakini tuwe wakweli,yaani kutangaza utalii kwa dakika tisini kwa gharama ya shilingi bilioni tatu!?Na kama tujuavyo tatizo sugu la wizi wa mapato kuanzia TRA hadi kwa watendaji ngazi ya kata,si ajabu muda huu mafisadi wameshapiga mahesabu ya pasenti ngapi watakwiba kwenye chochote kitakachpatikana kwenye mechi hiyo.

Na kuna hoja ya rankings za FIFA.Hivi mechi moja ya kununua kwa mabilioni itatupandisha kwa kiwango gani ukilinganisha na menchi dhidi ya Rwanda ambayo kama "tukikaza misuli" na kufanikiwa kucheza CHAN tutapata nafasi kubwa zaidi ya kupandisha ranking yetu huko FIFA?

Ukitaka kufahamu namna ubabaishaji na ufisadi unavyozidi kutafuna mfumo wa jamii yetu subiri mechi iishe kisha vianze visingizio vya namna FA walivyoshindwa kufikia lengo la mapato.Binafsi nisingekuwa na tatizo laiti FA wangeafikiana na wenzao wa Brazil kisha kuuza tiketi kabla ya mechi na hivyo kufahamu faida au hasara itakayopatikana.Lakini kwa hali yasasa ni sawa na kucheza bahati nasibu.Na si ajabu visingizio vimeshaandaliwa as to kwanini "mechi hiyo haikuweza kurejesha faida iliyotarajiwa".

Ndio maana nashawishika kusema kuwa inawezekana ALIYETUROGA KESHAFARIKI.

Tuesday, 1 June 2010

Crew ya £OVELY GAMBLE
BARAKA BARAKA, Managing Director wa Urban Pulse,akitoa hotuba
 BARAKA, DAISY,TIM, RENNY na FRANK
FRANK EYEMBE na BARAKA BARAKA
MC wa Show,Miss TINA GEORGE wa AILTV
MECKY,RAHMA CLASSIC,TINA,BARAKA,HALIMA,FRANCIA na FRANK
Msanii ANN-LYNN,AMOS MASANJILA na TINA
Producer wa £ovely Gamble,FRANK EYEMBE,akitoa hotuba
Urban Pulse CEO akiwa na MECKY
£OVELY GAMBLE

Sunday, 30 May 2010


Nafahamu unaweza usinielewe kwenye post hii lakini naomba niweke bayana kuwa niko radhi kutofautiana nawe msomaji wangu mpendwa.Kwa tutakaoafikiana,all I can say is POA.Nimeguswa na habari kuwa jana Makamu wa Rais,Dkt Shein, amezindua mbio za mwenge.Lengo la makala hii ni kuibua mjadala kuhusu suala hili la MWENGE WA UHURU.

Zamani hizo,mwenge ulikuwa na maana kubwa kwa kila mahali ulipopita.Lakini ni dhahiri kwamba mbio za mwenge kwa sasa hazina tofauti na ngonjera kuwa "Tanzania ni nchi ya Kijamaa" au kaulimbiu kwamba "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania Yanawezekana".

Hili dude linalokula mamilioni ya shilingi katika gharama za kununua mafuta ili liendelee kuwaka,sambamba na posho kwa wanaolizungusha nchi nzima lina umuhimu gani kwa sasa?Maana zamani hizo mwenge ulikuwa na madhumuni ya KUMULIKA lakini sote tunafahamu kuwa kwa muda mrefu sasa mwanga wa mwenge huo unamulika vichochoroni tu huku ukishindwa kuwaangazia macho mafisadi wanaotafuna nchi yetu kama mchwa.Natambua kuwa kuna miradi mbalimbali inayozinduliwa wakati wa mbio za mwenge lakini hilo linafanyika hata wakati mwenge umezimika.Kwa maana nyingine,mwenge uwake usiwake bado wananchi wataendelea kujikusanya (pamoja na uchovu wao) kujitafutia maendeleo yao wenyewe.

Tatizo kubwa la sie Waafrika ni kuendeleza "mila na desturi" hata pale zilipopitwa na wakati.Hivi fedha zinazotumika kuzungusha mwenge nchi nzima zinaweza kujenga zahanati,shule na barabara ngapi?Kwa hakika ni nyingi tu.

To cut the story short,mie nina mtizamo kuwa mbio za mwenge zimepitwa na wakati.Naamini kuwa gharama zinazotumika katika mbio za mwenge zinaweza kutumika vizuri zaidi kwenye maeneo mengine ya msingi.Mwenge unakimbizwa kila mwaka lakini umasikini wa Watanzania unazidi kuongezeka (puuza kauli za Mkulo kuwa uchumi unazidi kukua kwani analipwa mshahara kusema 'lolote'),ujambazi ndio usiseme,na mafisadi wanazidi kulindwa na chama tawala.Sasa hili dude linalokula mafuta kama halina akili nzuri bado lina umuhimu kweli kwa mazingira ya Tanzania ya sasa?

Karibu uchangie


Ukisoma habari zifuatazo unaweza kukubaliana nami kuwa AKUTUKANAE HAKUCHAGULII TUSI.Katika habari ya kwanza tunashuhudia Waziri wetu wa Fedha akiongea vitu ambavyo vinaleta maana tu vikiangaliwa kwa maadnishi lakini sio mtaani.Na katika habari ya pili,tunashuhudia uzembe uliozoeleka wa kitokee kwanza kisha tufanye kitu flani.Yaani siku zote hizi mtu aliyekabidhiwa dhamana ya kuongoza Jeshi la Polisi alikuwa hafahamu kuwa kituo cha polisi kisicho na silaha hakina tofauti simba wa karatasi!
Hebu soma habari husika hapa chini
Mkulo: Uchumi unazidi kukua 

Saturday, 29 May 2010 09:22

Exuper Kachenje

SERIKALI imesema kuwa ukuaji wa pato la taifa katika unakadiriwa kuongezeka na kwamba pato halisi litakua kwa asilimia 7 katika mwaka 2010.

Akiwasilisha taarifa ya mwelekeo wa uchumi kwa mwaka 2009 na mwelekeo katika kipindi cha kuanzia 2010 hadi 2013 mbele ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo alisema kuna matarajio makubwa uchumi kuendelea kukua.

Huku akiwaomba radhi wabunge kwa kuchelewa kuwapa nakala ya taarifa hiyo, Mkulo alisema maelezo hayo yalipitishwa juzi asubuhi na Baraza la Mawaziri.

"Naomba radhi waheshimiwa kwa kuchelewa kuwapatia nakala ya taarifa hii kwa kuwa imepitishwa jana asubuhi (juzi) na Baraza la Mawaziri hivyo imechelewa kuchapwa," Mkulo alisema.

Mkulo alisema kuwa katika mwaka 2011, pato halisi la uchumi litakuwa kwa asilimia 7.1, mwaka 2012 asilimia 7.4 na hadi kufikia mwaka 2013 pato halisi la taifa litafikia asilimia 7.8.

“Kama ilivyotarajiwa athari za msukosuko wa uchumi zilikuwa za mpito, hivyo ukuaji wa pato la taifa unakadiriwa kuanza kuongezeka. Pato halisi litakua kwa asilimia 7.0 mwaka 2010, asilimia 7.1 mwaka 2011, asilimia 7.4 mwaka 2012 na kuendelea kuongezeka hadi asilimia 7.8 mwaka 2013,” alisema Mkulo.

Alifafanua kuwa malengo hayo yanatarajiwa kufikiwa kwa kutekeleza sera na misingi ya uchumi kwa kuzingatia mambo mbalimbali, ikiwemo mwenendo wa uchumi wa dunia na hitaji la kujenga uwezo kukabiliana na athari za msukosuko wa uchumi wa dunia.

Alitaja misingi mingine kuwa ni kuendelea kutengemaza vigezo muhimu vya uchumi jumla na maendeleo ya jamii hasa mfumuko wa bei, kuweka msukumo katika utekelezaji Dira ya Maendeleo ya Taifa, Mkukuta awamu ya pili, Kilimo Kwanza na kuelekeza rasilimali kwenye maeneo chochezi ya uchumi kwa haraka zaidi.

Kwa mujibu wa Mkulo katika kipindi hicho miradi inayopewa kipaumbele katika mwongozo huo wa bajeti itakuwa ni pamoja na miundombinu, uendelezaji ardhi na makazi pamoja na vitambulisho vya taifa.

Vingine ni nishati, viwanda, sekta ya fedha na pia kutaja uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba mwaka huu kuwa ni kipaumbele cha kipekee kwa serikali katika mwaka huu kwa lengo la kuhakikisha unafanyika kama ilivyopangwa.
Waziri huyo alisema katika muda huo kasi ya upandaji wa bei inakisiwa kupungua hadi asilimia 8.0 kufikia mwezi Juni mwaka huu na kupungua zaidi hadi asilimia tano ifikapo Juni 2011.

Aidha, alisema katika kipindi hicho mapato ya ndani ya taifa yatafikia uwiano wa asilimia 17.3 kwa mwaka 2010/11; asilimia 17.4 mwaka 2011/2012 na asilimia 17.6 ifikapo mwaka 2012/2013.

Alisema serikali pia inalenga kuwa na akiba ya fedha za kigeni itakayokidhi uagizaji bidhaa kutoka nje na huduma kwa kipindi kisichopungua miezi mitano; kuwa na viwango imara vya ubadilishaji wa fedha; kuboresha mazingira ya uwekezaji na kufanya biashara na kuedeleza kilimo na kupunguza viwango vya riba.
Kuhusu biashara, Mkulo alisema Tanzania imeshuka katika vigezo vya urahisi wa kufanya biashara kutoka nafasi ya 126 kati ya nchi 183 na kuwa ya 131 mwaka 2009.

Kuhusu mapato ya ndani, Waziri Mkulo alisema yaliongezeka kwa asilimia 18.1 kufikia Sh4,293.1 bilioni mwaka 2008/09; kutoka Sh3,634.6 bilioni mwaka 2007/08 na kwamba kiasi hicho ni pungufu ya asilimia 10 kwa mwaka 2008/09.

Kwa kipindi cha Julai 2009 hadi Machi 2010, mapato ya ndani yalifikia Sh3,490.3 bilioni ikiwa chini ya asilimia 8.7 ya makisio ya Sh3,924.9 kwa kipindi hicho akieleza kuwa hali hiyo ilitokana na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia.

Mkulo alisema kwa kipindi cha Julai 2009 hadi Machi mwaka huu matumizi ya serikali yamefikia Sh6,143.9 bilioni kati ya makisio ya Sh6,718.7 kwa kipindi hicho, ikiwa ni upungufu wa asilimia tisa uliotokana na upungufu wa mapato.

Wakichangia maelezo hayo wabunge walitaka serikali ieleze itafanya nini kuwezesha wananchi kumiliki uchumi badala ya kumiliki asilimia 10 pekee kama ilivyo sasa.

CHANZO: Mwananchi

IGP Mwema afuta vituo

na Sitta Tumma na Ali Lityawi
SIKU tatu baada ya wananchi wa Kata ya Mbarika, wilayani Misungwi, mkoani Mwanza kuvamia kituo cha polisi na kuua majambazi watatu, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema ameanza kulikarabati upya jeshi hilo.
Tanzania Daima imethibitishiwa hilo; ukarabati wa jeshi hilo umelenga kuvipunguza kwa kuvifutilia mbali baadhi ya vituo vidogo visivyokuwa na silaha wala askari wa kutosha.

Wakati IGP Mwema akipanga kuvifumua vituo hivyo, jeshi la polisi mkoani Mwanza halijamkamata mtu hata mmoja kuhusiana na tukio la kuvamia na kuvunja kituo cha polisi Mbalika na kuua watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi.

Akithibitisha yote hayo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanmza, Simon Sirro (RPC), alisema IGP Mwema yupo katika mikakati ya kupunguza utitiri wa vituo vidogo vidogo vya polisi, kwani vimeonekana havina faida kwa wananchi.

“Unajua vituo hivi vidogo visivyokuwa na silaha havina faida kwa maana hiyo mkuu wa polisi kwa sasa yuko katika mpango wa kuvipunguza.

“Mkakati huu madhumuni yake ni kuwa na kituo kimoja kila kata chenye silaha na askari wa kutosha,” alisema Kamanda Sirro.

Mei 27 mwaka huu majira ya saa 1:30 jioni, wananchi wa Mbalika, wilayani Misungwi mkoani hapa, walivamia na kuvunja kituo cha Mbalika kisha kuua watuhumiwa.

Moja ya sababu za wananchi hao kuvamia na kufanya mauaji katika kituo hicho, inaonekana ni kutokuwa na silaha pamoja na askari wa kutosha kituoni hapo na kumshtua IGP Mwema.

Kamanda Sirro, alipoulizwa mikakati ya kupunguza vituo hivyo, alisema hana jibu anayepaswa kulizungumzia ni IGP Mwema pekee.

Tanzania Daima, ilipomtafuta IGP Mwema kwa ajili ya kupata ufafanuzi zaidi, simu yake ilipokelewa na msaidizi ambaye alidai yuko mkutanoni.

“Afande IGP yupo kikaoni huku Kilolo mkoani Iringa; atakuwa Dar es Salaam kesho (leo),” alisema msaidizi huyo.



Tawala,viongozi na wafanyakazi wa African Star,Afro Euro Events Management, Buzzie Production, Manamba Studio na Urban Pulse. Wanatoa shukurani zao za dhati kwa Watanzania wote waliojitokeza usiku wa jana 29/05/2010 kwenye onyesho maalum la ‘£OVELY GAMBLE’ kuchangia watoto wanaoishi na vijirusi vya UKIMWI nyumbani Tanzania. Watoto hawa wanaangaliwa na TANZANIA MITINDO HOUSE. Hakika ya kweli mmeoonyesha umoja ambao tunauthamini na hatutousahau.

Vilevile tungependa kuwatambua watu wafuatao, ambao kwa njia moja ama ingine    wmesaidia sana kufanikisha Onyesho hili maalum

UBALOZI WA TANZANIA  (mama Balozi na Maafisa wote wa Ubalozi)
TANZANIA ASSOCIATIONS zote Kitaifa na matawi  ya Reading, Birmingham na Soctland
BONGO FLAVOUR (Dixon na Flora)
TMH (Khadija Mwanamboka)
SWIFT FREIGHT (Abu Faraji)
SWAHILI TRAVEL AGENCY (Tino)
VINCENT BAR (Kalinga na Gado)
MAMA MAYOR (Mariam Nice)
NOCHA SEBE
MISS YVONNE
WITENGERE KITOJO 
TEGEME CHAMPANDA
FRANCIA CHENGULA
FREDDY MACHA
AYOUB MZEE
RASHIDI KAWAWA
ALLY MUHIDINI
GLOBAL PUBLISHER (Abdalah Mrisho)
BONGOSTARLINK (Dj Choka)
JIACHIE (Ahmad Michuzi)
KULIKONI UGHAIBUNI ( Evarist Chahali)
MISS JESTINA GEORGE (Tina George)
FASHION 8020 (Shamim Mwasha)
NURU THE LIGHT (Nuru)

Vyombo hivi na Watanzania hawa wamekuwa mstari wa mbele katika kufanikisha Onyesho hili maaaluma la mchango wa kihiyari. Mungu awaongezee na tuendeleze umoja  huu.


            MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU WABARIKI WATANZANIA

Saturday, 29 May 2010

Mama Mpendwa,

Ilikuwa saa 4.30 usiku,tarehe 29 Mei 2008 ulipotutoka.Nakumbuka nilipopigiwa simu kufahamishwa kuwa Bwana Amekutwaa,nilidhani ni ndoto tu.Japo ulikuwa umepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitatu kabla ya kukumbwa na mauti sote tuliamini kuwa siku moja ungeamka ukiwa mzima.Mama,japo leo ni miaka miwili tangu ututoke,bado nahisi niko ndotoni na nimeshindwa kabisa kukubaliana na ukweli kwamba haupo nasi.Mara kwa mara nakuona ndotoni,lakini napoamka nagundua ni ndoto tu,na hiyo inazidisha uchungu na majonzi.

Baba Mzee Chahali,uliyeishi nae katika ndoa kwa miaka 50,anaendelea kukukumbuka mno.Ni vigumu zaidi kwake kukabiliana na kututoka kwako kwa vile ulikuwa ni rafiki yake mkuu,mtu wake wa karibu kabisa na kila kitu kwake kama ilivyo kwetu.Mapacha, Kulwa (Peter) na Doto (Paul) nao wameendelea kuwa na wakati mgumu kwa vile wewe ulikuwa zaidi ya mama yao.Walikutania,walicheka nawe,walikusaidia kazi za nyumbani,walikwambia furaha na majonzi yao,na waliringa kuwa na mzazi mwenye upendo kama wewe.

Japosiku zote  tangu ututoke tumekuwa na wakati mgumu sana,siku hii ya leo tunapoadhimisha miaka miwili ya kifo chako ni ngumu zaidi kwetu.Inaleta kumbukumbu zisizoelezeka na zisizostahimilika.

Kazi ya Mungu haina makosa.Tukijiuliza sana kwanini alikuchukua wakati bado tunakuhitaji sana tutakuwa tunakufuru.Tunajaribu kujifariji kwa kuamini kuwa alikuchukua kwa vile alikupenda zaidi yetu.Na tunajitahidi pia kujiridhisha kuwa huko ulipo unapata pumziko la amani na unaangaziwa mwanga wa milele ukistarehe kwa amani.Japo haupo nasi kimwili lakini siku zote tupo nawe kiroho.

Pumziko la Milele Akupe Ee Bwana na Mwanga wa Milele Akuangazie Ustarehe Kwa Amani,Amen.


ONYESHO MAALUM LA FILAMU £OVELY GAMBLE 
TAREHE 29TH OF MAY 2010. 
 KARIBUNI KUCHANGIA YATIMA WALIOATHIRIKA NA UKIMWI TANZANIA NA JUMUIA YETU YA TANZANIA

VILEVILE KUTAKUWA NA CHAKULA, VINYWAJI, BURUDANI YA MIZIKI NA VICHEKESHO.
NYOTE MNAKARIBISHWA NA KUFIKA KWENU NDIO KUFANIKISHA SHUGHULI HII. TUNAWAOMBA MJE KUSAIDIA WATOTO HAWA NA JUMUIYA YETUWETU.

DRESS CODE: LADIES: DRESS GLAMOROUS AND ELEGANT  GENTS: SMART

MUSIC: LIVE MUSIC, AFRO BEAT, BONGO FLAVOR, HIP HOP, MDUARA AND RNB

WYCLIFFE VENUE 233 KINGS ROAD READING RG1 4LS. 6.30pm-11.30pm

TCKT IN ADVCE £10 FOR VIP’s SEATS AND £5 FOR STANDARD SEATS. (*VIP TCK HOLDERS GETS FREE AFTER PARTY PASS*)

TCKT ZA PAUNDI 5 ZINAMALIZIKA WAHI MAPEMA

‘£OVELY GAMBLE DVD AND SOUNDTRACK OUT NOW’

DVD MAALUM “DIRECTORS CUT” WITH BONUS MATERIAL
*FILMMAKERS
*HATAKAMA
*SEXY MAMA

WOTE MNAKARIBISHWA
---------------------------------------------------------------
BARAKA BARAKA

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget