Wednesday, 23 April 2008

Naamini wengi wenu mnakikumbuka kibao cha "Ingekuwa Vipi" cha wasanii Jay-Mo na Mwanafalsafa.Nakipenda,sio kwa beats zake pekee,bali pia kimebeba ujumbe mzito wenye maswali mazito.Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la Raia Mwema imeanza kwa kunukuu verse moja ya wimbo huo,lengo likiwa sio uchambuzi...

Tuesday, 22 April 2008

NINA LUNDO LA PICHA LAKINI LEO INTERNET IKO SLOW SANA.KEEP ON VISITING THE BLOG FOR MORE PICS.PICHA TATU ZA CHINI NI KUTOKA HOSPITALI YA MTAKATIFU FRANCIS IFAKARA (KUNA SANAMU YA MTAKATIFU HUYO KATIKA PICHA YA TATU).PICHA YA NNE NI MAHINDI YALIYOANIKWA KWENYE LAMI.SIJUI NDIO TEKNOLOJIA AU VIPI LAKINI...

Monday, 21 April 2008

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inaelezea kwa kirefu nightmare niliyokumbana nayo baada ya kuingia mkenge wa kusafiri "first class" ya Tazara.Hiyo ilikuwa wakati naelekea nyumbani Ifakara mkoani Morogoro.Baada ya mateso ya hiari huko Tazara,nikaamua usafiri wa kurudi Dar...

Bilionea mwenye vijisenti,Andrew Chenge amejiuzulu,na Braza Ditto amefariki.Hizo ndizo habari zinazovuma hapa Dar tangu asubuhi.Hii ya kifo cha Ditto niliisikia jana.Na kama ilivyo kawaida,kila mmoja anasema lake ila kwa vile blogu hii si ya udaku,naomba nisiorodheshe conspirancy theories lukuki zinazovuma...

Friday, 18 April 2008

Katika picha hapo chini,treni ikikatiza kwenye railway crossing hapo jana.Almanusura itokee ajali mbaya laitimzalendo mmoja asingemshtua dreva kwamba anaona moshi wa treni kwa mbali.Yaani hakuna namna kwa mwenye gari kufahamu awapo kwenye railway crossing iwapo garimoshi linakuja au la.Picha ya chini...

Wednesday, 16 April 2008

Katika makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema,nazungumzia suala zima la huduma bora.Makala inaanza kwa kuondoa fikra za "u-tambarare" wa maisha ya ughaibuni,zinazochochewa na taswira za runinga na magazeti ya kimataifa.Ni rahisi baadhi ya wenzetu walioko nyumbani kuhisi kwamba...

Tuesday, 15 April 2008

Nani kasema Breaking News lazima iwe ya CNN,BBC,AL-Jazeera,etc pekee?Hii ni live and direct from Ifakara:maji katika mto Lumemo yamevunja kingo za mto huo dakika chache zilizopita na hivi sasa yanakuja kwa kasi huku mjini-kati.Wazoefu wananiambia nikisubiri ili nipate picha za kuweka hapa bloguni basi si ajabu huko Scotland likarudi jina tu na hii blog ikaishia kufa kifo cha asili (bloga akisombwa na mafuriko si inamaanisha blogu nayo imekufa,au...

MASHABIKI WA SOKA WA IFAKARA WAKIFUATILIA MECHI KATI YA TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS YA KENYAHUYU NYAU ANAJARIBU KU-GOOGLE NENO "UFISADI"HIKI NI CHOO NDANI YA BEHEWA LA DARAJA LA KWANZA LA TAZARA.EVER HEARD OF A TRAIN FROM/TO HELL?UFISADI KUTOKA CHINA: HII NI PIRACY YA DARAJA LA KWANZA (ZAIDI YA LILE...

Thursday, 10 April 2008

Huduma za afya hapa nyumbani ni duni na hazileti matumaini ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania (by the way,tangu nifike hapa sijaona ile hamasa niliyoikuta 2005 kuhusiana na kauli-mbiu hiyo.Sijui imekufa kifo cha asili au imepotea kama Gavana Daudi Ballali!).Hospitali za umma zinaweza kujitetea kuhusu...

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget