
Friday, 27 June 2008

Thursday, 19 June 2008

Pia makala yangu inazungumzia suala zima la ushirikina hapa nyumbani ambapo nimejaribu kulitazama kwa upande mmoja kama mwanafunzi wa zamani wa sosholojia ya dini (sociology of religion) na kwa upande mwingine kama mwanajamii ninayeelewa nini kinanizunguka,hata kama tunaona aibu kukiongelea.Sio siri kwamba mambo ya ushirikina yameshika hatamu sana katika jamii mbalimbali za Kiafrika,lakini hii ya Fisadi Mzee wa Vijisenti kumwaga ndumba ndani ya Bunge inaonyesha jinsi gani mambo yanakwenda mrama sana katika nchi hii tuliyoahidiwa kuwa maisha bora kwa kila aliyezaliwa hapa yanawezekana.Nisikunyime uhodno,bingirika na makala hiyo pamoja na nyingine zilizokwenda shule ya kutosha KWA KUBONYEZA HAPA
Saturday, 14 June 2008

Naomba kuwapatia makala chache ambazo kutokana na matatizo niliyokuwa nayo sikuweza kuzitundika hapa.Katika makala yangu ndani ya gazeti la Raia Mwema la tarehe 28/05 nilizungumzia suala la wagombea binafsi na kutabiri kwamba huo unaweza kuwa ndio kifo cha mafisadi.Makalahiyo ilikwenda kwa kichwa WAGOMBEA BINAFSI:KIFO CHA MAFISADI CHAJA. Katika toleo lililofuatia,yaani la tarehe 04/06,nilizunguzmia kuhusu utendaji kazi wa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu,Bwana Salva Rweyemamu.Zaidi,soma makala hiyo yenye kichwa KAULI ZA MKURUGENZI IKULU KUHUSU BALLALI MKANGANYIKO MTUPU.Makala ya wiki hii,yaani iliyotoka Jumatano ya tarehe 11/06 inazungumzia Mkutano wa Sullivan uliomalizika huko Arusha hivi karibuni.Katika makala hiyo nimejaribu kuhoji iwapo Mkutano huo umekuwa/utakuwa na faida yoyote kwa Watanzania.Makala hiyo imebeba kichwa kisemacho MKUTANO WA SULLIVAN:WAZAWA WAMENUFAIKA VIPI?
Tuesday, 3 June 2008
07:39
Unknown
MSIBA
6 comments
NINASIKITIKA KUWATANGAZIA KIFO CHA MAMA YANGU MZAZI ADELINA MAPANGO KILICHOTOKEA IFAKARA MOROGORO TAREHE 29/05/2008 NA MAZISHI YALIKUWA JANA TAREHE 02/06/2008 KATIKA MAKABURI YA UKOO WA CHAHALI HAPA IFAKARA.NAWASHUKURU NYOTE AMBAO KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE MLIUNGANA NAMI KATIKA KUMUOMBEA MAMA APONE LAKINI BWANA AMEMPENDA ZAIDI NA HATIMAYE KUMREJESHA KWAKE.UKOO WA CHAHALI NA MAPANGO UNAWASHUKURU SANA KWA USHIRIKIANO WENU.BWANA AMETOA BWANA AMETWAA,JINA LA BWANA LIHIMIDIWE MILELE.
Subscribe to:
Posts (Atom)