Wednesday, 5 March 2014

 
Mshindi wa kura za maoni za kugombea ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani Kikwete amesema siasa anazofanya sasa hazina uhusiano wala ubia na baba yake.
Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kura za maoni za chama hicho katika jimbo hilo kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Msata alisema anafanya siasa kwa maisha yake na si kwa mgongo wa baba yake kwani aliingia katika siasa akiwa na umri wa miaka mitano na hakuwahi kufanya hivyo kwa sababu ya baba yake.
“Siasa ninayofanya haina uhusiano na baba yangu, nafanya siasa kwa maisha yangu na sina ubia na baba yangu katika hili” alisema mtoto huyo wa Rais Jakaya Kikwete.
Akijibu swali la kwa nini amejiingiza katika siasa tofauti na maneno yake aliyowahi kutamka mwaka 2010 kuwa hawezi kushiriki katika kinyang’anyiro cha ubunge katika jimbo hilo, Ridhiwani alisema wakati huo hakuwa tayari.
“Kwenye siasa usiwe muwazi katika kila kitu, ukiwa hivyo unawapa nafasi maadui kukushambulia, mimi hapa Chalinze ni kwetu, kwa wazazi wangu na kule Bagamoyo tunakwenda tu kikazi na ndiyo maana nikaamua kurudi nyumbani kuomba ridhaa. Nashukuru kuongoza katika kura za maoni ninaona ni kiasi gani ninaungwa mkono,” alisema.
Katika kura hizo za maoni Ridhiwani alibuka mshindi kwa kura 758, akifuatiwa na Imani Madega aliyepata kura 335, Ramadhan Maneno (206) na Mkwazu Changwa (17).
Kamati Kuu ya CCM (CC), inatarajiwa kukutana Machi 8, mwaka huu kupitisha jina mgombea wake wa ubunge katika jimbo hilo nafasi ambayo iliachwa wazi na Said Bwanamdogo aliyefariki dunia Januari 22, mwaka huu.

Related Posts:

  • The Week In Bullshit: From Russia With LoveYea,I know,it's none of my business but,man,this story left me quite perplexed.Lots of stuff's already been said about what you might call 'the foreign arms of our ruling party CCM.And much of it isn't funny to read,but I per… Read More
  • Has the Opposition Endorsed JK?It's nearly less than seven months before Tanzanians go to poll to elect,among others, the 5th phase president,should all go well.However,none of the major opposition parties have so far come up with any names of their potent… Read More
  • CCJ Wana Mpya Gani?Mwaka 1996 nikiwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza pale Mlimani nilipata 'somo' moja muhimu kuhusu wanasiasa wa Tanzania.Ilikuwa ni kwenye mhadhara (lecture) ya Dr (Profesa kwa sasa) Max Mmuya katika somo Siasa na Serikali Tanz… Read More
  • Laiti Busara za Waziri Kiongozi Zingesambaa CCM....Shamsi Vuai Nahodha.Huyu ni Waziri Kiongozi huko Zanzibar.Naomba kukiri hadharani kuwa kwa muda mrefu nimekuwa nikimuona mwanasiasa huyu kama 'yupo yupo' tu.Unajua kuwa mwanasiasa au kiongozi kunapaswa kuendana na mchango wa … Read More
  • Utafiti UDSM/TAKUKURU: CCM Kinara wa Rushwa.CCM kinara wa rushwaYahya CharahaniWAKATI vita dhidi ya ufisadi ikionekana kupoteza mwelekeo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho kinachoongoza kwa rushwa nchini, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam … Read More

0 comments:

Post a Comment

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget