KULIKONI UGHAIBUNI-37Asalam aleykum,Miongoni mwa mambo ambayo taasisi nyingi za huku ughaibuni zinajitahidi sana kuwa nayo ni hadhi na imani za wananchi kwa taasisi hizo.Na sehemu nzuri ya kuangalia hilo nalozungumzia ni kwenye taasisi za fedha.Kwa hapa Uingereza na nchi nyingine za Magharibi,wateja wa taasisi flani huwa ni kama wameweka “mikataba” na taasisi hizo. Usishangae ukisikia kuwa katika familia flani,tangu enzi za mababu wao wamekuwa wateja...
Thursday, 16 November 2006
Monday, 13 November 2006
13:51
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI:Asalam aleykum,Kwanza nitoe salamu zangu za rambirambi kwa familia ya dereva wa daladala aliyeuawa kwa kupigwa risasi na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Braza Dito.Ni matarajio yetu wengi kuwa sheria itachukua mkondo wake na haki itatendeka,na kwa wakati huu inatupasa tuiachie mahakama ifanye kazi yake bila kuingiliwa.Wakati naandaa makala hii wananchi wa Marekani wanapiga kura katika uchaguzi wa kati ya muhula (mid-term) ambao unaotazamiwa...
13:49
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-35:Asalam aleykum,Waziri Mkuu Tony Blair anatarajiwa kung’atuka mwakani.Ataondoka huku Waingereza wengi wakimwona kama kiongozi ambaye anapaswa kuingia katika vitabu vya historia kwa mambo mbalimbali,mazuri na mabaya.Pengine baya zaidi ni jinsi ambavyo wengi wanamwona kama kibaraka wa George W. Bush.Hata hivyo,wapinzani wa Blair wanakubali bila ubishi kwamba huyu Bwana akipewa fursa ya kujieleza huwa hafanyi makosa.Ukubaliane nae...
13:47
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-34Idd Mubarak (japo nimechelewa kutoa salamu hiyo,nategemea kusikia “minal faidhina” kutoka kwako msomaji mpendwa wa safu hii).Katika mojawapo ya makala zangu za nyuma niliwahi kuahidi kuwazungumzia jamaa flani ambao ndio kama uti wa mgongo wa uongozi wa Rais George W Bush.Hawa jamaa wanafahamika kama “neoconservatives” au kwa kifupi “neocons.”Msamiati huu uliibuka kwenye miaka ya 60 na 70 na ukapata umaarufu zaidi wakati wa utawala...
13:46
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-33Asalam aleykum,Majuzi nilipata barua pepe kutoka Uholanzi ikinieleza kwamba jina langu limepitishwa katika bahati nasibu ya Jumuiya ya Ulaya na “nimebahatika” kuwa mshindi wa Euro milioni moja!Wahusika waliniomba kuwapatia taarifa za akaunti yangu ya benki ili waweze kuingiza kitita hicho.Unaweza kudhani kwamba labda nilipiga kigelegele cha furaha kwamba hatimaye Mndamba mie nimekuwa milionea.Umekosea.Kabla hata ya kumaliza kuiosma...
13:44
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-32Asalam aleykum,Kwanza napenda kutoa pole kwa familia za marehemu Walter Mazula na mchumba wake Vonatha Nkya.Kwa namna mazingira ya huku ughaibuni yalivyo,Mtanzania mwenzako popote alipo ni kama sehemu ya familia.Mauaji hayo ya kikatili yamewagusa watu wengi hata kwa sie ambao hatukubahatika kukutana nao wakati wa uhai wao.Kwa mujibu wa wenzetu walio Marekani,kulikuwa na ushirkiano mkubwa na familia ya wafiwa kwa kuwafariji na...
13:43
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-31Asalam aleykum,Moja ya mambo ambayo yalikuwa magumu kwangu baada ya kuwasili hapa nilipo ni namna ya kuendana na aina ya chakula kilichozoeleka hapa.Mie ni Mndamba,na kule kwetu Ifakara hadithi ni wali,wali na wali sana.Asubuhi ni chai na kiporo cha wali,mchana ni wali,na usiku hadithi ni hiyohiyo ya wali.Nilipokuwa nawakaribisha rafiki zangu pale Ifakara mama alihakikisha kuwa lazima wapate wali,na japo ugali pia ni mlo lakini...
13:42
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-30:Asalam aleykum,Mwaka jana wanamuziki mbalimbali maarufu duniani walifanya matamasha makubwa nchini Uingereza,Marekani,Japan,Italia,Ufaransa,Canada na Afrika Kusini kwa lengo la kukusanya fedha za kupambana na umasikini barani Afrika.Miaka 10 kabla ya hapo kulifanyika matamasha kama hayo kwa lengo hilohilo.Matamasha hayo yalizua mjadala mmoja mkubwa kuhusu iwapo kweli nia nzuri ya kupambana na umasikini barani Afrika inaweza...
13:40
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-29Asalam aleykum,Kuna dalili za kutosha kwamba pindi Waziri Mkuu wa hapa Tony Blair atapong’atuka madarakani atarithiwa na Kansela Gordon Brown.Tayari baadhi ya viongozi wa chama cha Conservative kimeonyesha wasiwasi wa namna flani kuhusu Brown ambaye anatoka Scotland kushika nafasi hiyo ambayo ni ya uongozi wa juu kabisa wa serikali ya Uingereza.Pia kuna kipindi flani kulikuwa na mjadala kuhusu wabunge wanaotoka Scotland kuchangia...
13:39
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-28Asalam aleykum.Mwaka 2003 Mmarekani mmoja aitwaye Dan Brown alichapisha kitabu kiitwacho The Da Vinci Code ambacho baadaye kilipelekea kutengenezwa kwa filamu iliyobeba jina hilohilo.Hadi mwezi Mei mwaka huu zaidi ya nakala milioni 60 za kitabu hicho zimeshauzwa sehemu mbalimbali duniani.Idadi hiyo ni sawa na nakala moja kwa kila Mtanzania na bado nyingine kibao zitasalia.Nayo filamu ya Da Vinci Code iliyotolewa mwaka huu hadi...
13:38
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-27Asalam aleykum,Hivi karibuni,serikali ya hapa ilitoa idadi ya raia wa kigeni walioingia nchini humu kutoa nchi za Ulaya za Mashariki ambazo ziliingizwa kwenye Jumuiya ya Ulaya mwaka juzi.Wengi wa wageni hao ni kutoka Poland na serikali imekiri kuwa idadi ya walioingia imekuwa zaidi ya matarajio ya awali.Tayari kumeanza mijadala kuhusu athari za kuruhusu wageni hao kuja kwa wingi namna hiyo.Hofu imeongezeka zaidi kutokana na ukweli...
13:35
Unknown
No comments
KULIKONI UGHAIBUNI-26Asalam aleykum,Hapa ni shwari japokuwa usafiri wa anga umekuwa ni kama adhabu vile tangu zipatikane taarifa kwamba kuna kundi la watu lililokuwa linapanga kulipua ndege kadhaa.Huwezi kuzilaumu taasisi zinazohusika na usafiri na usalama kwa kuchukua hatua ambazo kwa namna flani ni kama bughudha kwa wasafiri kwa vile pindi wakizembea kidogo tu basi kuna hatari ya watu kupoteza maisha yao.Wachambuzi wa mambo wanasema wakati magaidi...
Subscribe to:
Posts (Atom)