Saturday, 15 June 2013




Mara nyingi nimekuwa mtetezi wa mabloga wenzangu hasa katika dhana iliyotapakaa miongoni mwa Watanzania wenzetu kuwa mabloga wengi ni watu wa kukopi na kupesti, hawajibidiishi kupata ukweli wa wanachoandika...na kimsingi ni wadaku tu. Moja ya sababu zinazoifanya jamii iwaangalie mabloga wa Kitanzania kwa jicho baya ni huu UGONJWA WA BREAKING NEWS. Looks like, mabloga wengi wanahangaika sana kupata breaking news, na wengi wakidhani kuwa wao kuwa wa kwanza 'kuvunja' habari kutasaidia kuwapandisha chati.

Lakini Breaking News ni kitu kinachohitaji umakini mkubwa.Unaweza kuskia 'flani kafa' kumbe si kweli, na keshoyake ukaletewa mashtaka ya 'kumzushia mtu kifo.' Tmaa ya kuwa wa kwanza 'kuvunja habari' sharti iendane na umakini wa kuhakikisha kuwa habari husika ni sahihi.Ni muhimu kujihangaisha huko mtandaoni, kutafuta kwenye Google-kama ni habari ya kimataifa- au kumpigia simu mhusika au watu wanaomfahamu, kabla ya kukurupuka na 'BREAKING NEWS' kwa herufi kuubwa.

Nimekerwa sana na uzushi unaosambazwa na baadhi ya mabloga wa Kitanzania kuwa ziara ya Rais Barack Obama nchini Tanzania imefutwa. Chanzo cha uzushi huu ni kwa mabloga husika kutofahamu maana ya neno SAFARI.Akilini mwa mabloga hao, neno la Kiingereza SAFARI ni sawa kabisa na neno la Kiswahili safari.Wasicheoelewa ni kuwa SAFARI ya Kiingereza inamaanisha "kutembelea mbugani hasa kwa madhumuni ya uwindaji au kuangalia wanyama" Na hicho ndio kilichokuwa -cancelled katika ziara ya Obama.

Kwamba Rais Obama alipanga kutumia siku mbili nchini Tanzania katika SAFARI (kuzuru mbuga za wanyama) lakini inadaiwa kuwa gharama za kilojistiki zimepelekea wazo hilo kufutwa.Kilichofutwa ni WAZO LA KUFANYA SAFARI MBUGANI na sio WAZO LA ZIARA YA KUJA TANZANIA.

Na kimsingi habari hii (ya Obama kuahirisha SAFARI MBUGANI) ambayo chanzo chake ni gazeti la Washington Post (soma HAPA) BADO HAIJATHIBITISHWA,na kilichoandikwa na gazeti hilo ni taarifa tu ya kichunguzi

Sasa angalia mabloga wetu walivyokurupuka na BREAKING NEWS zao



Ndugu zangu mabloga, lugha ya Kiingereza ni tatizo la Kitaifa kwa Watanzania wengi japo kuna wanaojifanya 'kichwa ngumu' licha ya kutoimudu lugha hiyo. Sasa mnapokutana na habari iliyoandikwa kimombo, na hamna hakika nayo, basi ni vema kuomba msaada kwa wanaoimudu lugha hiyo badala ya kutuharibia sifa ambayo tayari ishaanza kuharibika.

TUTAKAO-MANTAIN HESHIMA YA KUBLOGU NI MABLOGA WENYEWE, NA TUNAKAOISHUSHA HADHI YA KUBLOGU NI MABLOGA WENYEWE PIA.

NATARAJI MABLOGA NILIOWATAJA HAPO JUU WATATUMIA UUNGWANA KWA KUHARIRI HABARI HIYO YA OBAMA, NA PENGINE WATATUMIA USTAARABU WA KUOMBA RADHI WASOMAJI WAO, BADALA YA KUENDELEA KUPOTOSHA UMMA.

PIA NATUMAINI HAWATOCHUKIZWA NA MIE KUWATAJA KATIKA POST HII KAMA MIFANO YA UBABAISHAJI KATIKA FANI YA KUBLOGU.

Related Posts:

  • Sarah,the Brains Behind Angalia BongoWiki hii tumeadimisha siku ya wanawake duniani.Na kesho ni siku ya mama zetu.Ni kipindi mwafaka cha kungalia mchango wa jinsia ya kike katika ngazi ya familia hadi taifa.Tukubali tusikubali,dunia imeendelea kutawaliwa na mfum… Read More
  • Kutoka kwa Dada Koero Kundi: UJIO WANGUNi matumaini yangu kuwa muwazima na mnaendelea na majukumu yenu ya kujenga Taifa au ustawi wa familia zenu popote mlipo.Ni kitambo kidogo nilitoweka katika ulimwengu wa Kublog, na hiyo ilitokana na majukumu yangu ambayo yalin… Read More
  • UOGA: UGONJWA UNAOTUKWAZA WATANZANIAHivi karibuni niliandika makala flani kuhusu milipuko ya mabomu huko Mbagala, jijini Dar es Salaam. Kwa kutambua kuwa blogu yangu haina idadi kubwa ya wasomaji (japo nawathamini sana wachache wanaotumia muda wao kuitembelea) … Read More
  • My Honest Reply to the So-called "Meya wa Mzumbe"You posted the following comment on this blog.I have tried to reply on your blog but it doesn't seem to work.I know my reply will offer you a rare chance of publicity,but,well,there's nothing I could do about that.Perhaps tha… Read More
  • Ukiona Mtu Anajikuna Basi Ujue AnawashwaUandishi wa blogu si jambo rahisi kama inavyodhaniwa na wengi.Na ni jambo gumu zaidi kwa akina sie tunaoelemea zaidi katika kuandisha mambo yanayogusa maslahi ya mafisadi na vibaraka wao.Kwa mfano mara kadhaa nimekuwa nikipat… Read More

0 comments:

Post a Comment

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget