Tuesday, 2 February 2010


Hivi karibuni Tume ya Uchaguzi ilieleza kwamba inaangalia uwezekano wa kuongeza idadi ya majimbo ya uchaguzi.Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu: ni rahisi kwa Tume hiyo kuwa na wazo kama hilo kwa vile halina athari zozote kwenye mishahara au posho zao.Kinyume chake,tunaambiwa zoezi la tathmini linatarajiwa kugharimu mabilioni ya shilingi.Unadhani zinakwenda wapi hizo kama si kwa haohao wanaokuja na wazo la kuongeza majimbo?

Mzazi mwenye busara hawezi katu kufikiri kuongeza idadi ya watoto wakati hao alionao sasa "wanampelekesha" linapokuja suala la kumudu gharama za matundo/malezi.Ni katika mantiki hiyohiyo,Tume ya Uchaguzi,ilipaswa kutambua kuwa uwezo wetu kiuchumi hauwezi kumudu majimbo zaidi ya hayo tuliyonayo sasa.

Lakini jingine lililo muhimu zaidi ni kuangalia ufanisi wa wawakilishi tulionao sasa.Naamini wengi tutaafikiana kwamba idadi kubwa ya wabunge hadi sasa haijasaidia kumkomboa Mtanzania kutka kwenye lindi la umasikini wa kutupwa.Tunashuhudia jinsi Bunge na Serikali wanavyotunishiana misuli kuhusu mazingaombwe ya Richmond,Kiwira,nk.Je kuongeza idadi ya wabunge kutaongeza "misuli zaidi" kwa Bunge.Jibu la haraka ni HAPANA.

Wengi wa wabunge wetu ni wabinafsi wanaoangalia maslahi yao binafsi.Umuhimu wa wapiga kura wao na majimbo wanayowakilisha unakuja pale tu kunapojiri uchaguzi.Wabunge,hususan wa CCM,wameweka mbele maslahi ya Chama kuliko wananchi wanaowawakilisha.Hilo lisingekuwa tatizo kama CCM ingekuwa chama kinachowajali wananchi badala ya mafisadi.

Na kwanini wazo la majimbo mapya lije mwaka huu tunapotarajia uchaguzi mkuu?Kwanini sio mwaka jana,juzi au 2007?Jibu jepesi ni kwamba wazo la majimbo mapya halina uhusiano na kukuza demokrasia au kuongeza uwakilishi bali ni kuwatafutia ulaji vigogo wanaonyemelea ubunge au wale ambao ubunge wao uko hatarini kutokana na upinzani kwa wanaotaka nafasi hiyo.

Nihitimishe kwa kueleza kuwa kuongeza idadi ya majimbo si moja ya vipaumbele vyetu kwa sasa.Pengine badala ya wazo hilo la kuwatengenezea watu ulaji,Tume ingetafakari ni namna gani wapiga kura watawezeshwa kuwabana wawakilishi wasiotekeleza wajibu wao majimboni.Tume pia inapaswa kuelewa kwamba wabunge watakaoongezwa pindi wazo la majimbo mapya likikamilika watapaswa kuongoza watu "hai",na ili "uhai" wa watu hao uwe na uhakika wa kuwepo ni muhimu kuhakikisha hatua za haraka zinachukuliwa kurekebisha hali ya uchumi wetu,sambamba na kuwabana mchwa (mafisadi) wanaotafuna kila kidogo tulichonacho.

Related Posts:

  • KUNDI LA MAFISADI LAZIDI KUIMARIKA NDANI YA CCMLowassa Tishio Ndani ya CCMNguvu ya kundi lake yatawala ndani ya NECKUNA kila dalili kwa aliyekuwa Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa, kupitishwa na vikao vya juu vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa mgom… Read More
  • KUONGEZA MAJIMBO SI KIPAUMBELEHivi karibuni Tume ya Uchaguzi ilieleza kwamba inaangalia uwezekano wa kuongeza idadi ya majimbo ya uchaguzi.Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu: ni rahisi kwa Tume hiyo kuwa na wazo kama hilo kwa vile halina athari zozote… Read More
  • MASWALI MUHIMU KUTOKA KWA MPAYUKAJI MSEMAOVYOJe mama Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe?na Nkwazi MhangoSiku hizi mke wa rais, Salma Kikwete, anaonekana kwenye kurasa za mbele za magazeti karibu kila siku akiwa mikoani akihamasisha hili na lile. Wengi wanahoji.… Read More
  • BAADA YA AHADI HEWA YA KUANZISHWA MAHAKAMA YA KADHI,MUFTI ATAKA WAISLAM WAIKATAE CCMMufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCMMufti Issa bin Shaaban Simba, amekasilishwa na uamuzi wa serikali kuhusu Mahakama ya Kadhi.Na Ummy MuyaBARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia … Read More
  • KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA 2010Ahadi za urais 2005 zamtesa Kikwete uchaguzi wa mwakaniRais Jakaya Kikwet, mzigo mzito wa ahadi zake za mwaka 2005 unamkabili uchaguzi ujao 2010.Na Mwandishi WetuMIEZI michache ikiwa imebaki kabla ya kuanza kwenda kwa wananch… Read More

0 comments:

Post a Comment

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget