Rafiki yangu mmoja amenitumia barua-pepe muda mfupi uliopita baada ya kusoma makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema.Hakuwa na pongezi wala malalamiko bali alidai kwamba wakati anasoma makala hiyo alijiskia kama anaongea nami uso kwa uso japo tuko umbali wa maili elfu kadhaa.Ni kweli,napoandika makala huwa najitahidi kadri ya uwezo wangu kuiwasilishalisha kwa kutumia staili ya mazungumzo (conversational style).Lakini sio mazungumzo kama ndani ya semina-elekezi,warsha,kongamano au semina bali yale yanayoweza kuwa yanafanyika mahala ambapo "tunaongea kwa kijinafasi" (comfortably).
Tukiachana na hilo,makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inagusia michuano ya soka ya Mataifa ya Afrika huko Ghana,na kuielezea kwamba ni moja ya habari njema chache kutoka bara hilo,hasa kwa vile kwa takriban mwezi sasa habari zinazotawala kutoka huko ni kuhusu vurugu zinazoendelea Kenya zilizotokana na matokeo ya uchaguzi mkuu nchini humo.Kwa kutumia mfano hai,makala hii pia inaelezea ugumu anaoweza kukabiliwa nao Mtanzania pindi akidadisiwa chanzo cha umasikini wa nchi yetu,kabla ya kuwachambua mafisadi wa fedha na wale wa mawazo.Pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule katika jarida hilo la Raia Mwema,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.
Ukimaliza kusoma makala hiyo,unaweza kuangalia clips hizi za versions mbili za Jesus Walks ya Kanye West.Naamini nasi tunahitaji nguvu za kiroho kukomesha ufisadi huko nyumbani.
KILANGO: CCM WANAOGOPA MAFISADIASEMA WACHACHE WALIOTHUBUTU WAACHIWE WAPIGE VITA UFISADISalim SaidMBUNGE wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela amesema viongozi wa chama tawala (CCM) wanaogopa kupambana na ufisadi kwa kuwa wanaopambana nao ni viongozi au …Read More
MOTO ALIOUANZISHA MALECELA WAENDELEA KUSHIKA KASI NDANI YA CCM MIMI SI MWANASIASA JAPO MALENGO YANGU YA BAADAYE NI KUWA MCHAMBUZI WA SIASA (POLITICAL ANALYST).BINAFSI SIICHUKII CCM ILA NAKERWA NA BAADHI YA KASUMBA ZILIZOOTA MIZIZI NDANI YA CHAMA HICHO KIKONGWE.NA KASUMBA KUU INAYONITATI…Read More
KAMATI YA BUNGE YAKATA 15% YA MISHAHARA YA MAFISADI MONDULI NAOMBA USOME HABARI IFUATAYO KISHA TUSHIRIKIANE KUFANYA TAFAKURI KATIKA MASWALI YANAYOJITOKEZA (katika maneno yenye rangi nyekundu).Na Salim SaidKAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa imekikataa kwa mara ya pili kita…Read More
MWANAHALISI: ROSTAM NUSURA AJIUMBUENa Alfred LucasMFANYABIASHARA na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz amesitisha uchapishaji magazetini wa taarifa yake ya kukana tuhuma za ufisadi.Taarifa iliyokuwa inakwenda kwa njia ya tangazo, ilikuwa inakana kuhusika kwake na k…Read More
MBUNGE WA CCM AWAWAKIA MAFISADI WA CCMAlly Sonda, Moshi MBUNGE wa Jimbo la Vunjo(CCM) Aloyce Kimaro,amewataka mafisadi wanaojiandaa kumng'oa madarakani Rais Jakaya Kikwete na kundi la wabunge waliojitoa kafara kupinga ufisadi kuvunja mtandao wao mara moja kwa kuw…Read More
0 comments:
Post a Comment