Monday, 26 September 2011


Wajuzi wa mambo wanadai kuwa moja ya mambo yanayopunguza ufanisi wa Idara yetu ya Usalama wa Taifa ni tabia iliyoota mizizi ambapo kila kigogo anataka kumpatia mwanae,mpwae,mtoto wa rafiki yake,nk katika ajira ya taasisi hiyo nyeti.Haina ubaya kutoa ajira iwapo mwajiriwa mtarajiwa atakuwa na sifa husika.Lakini uzoefu umeonyesha kuwa kanuni na taratibu zinabemendwa makusudi ili ajira hizo ziende kwa watu wa karibu wa vigogo hao.

Kibaya zaidi ni ukweli kwamba wengi wa watoto wa vigogo wanapopata ajira kwenye taasisi kama hii ambayo msingi wake mkubwa ni uzalendo wa mtumishi husika hujiona kama 'untouchables' flani,wanafanya mambo wapendavyo,usumbufu mtaani kwa zile 'unajua mimi ni nani/nafanya kazi wapi' huku bastola zikiachwa zionekane waziwazi kama Aden Rage.Wengi wa hawa vijana hawafahamu jukumu kubwa walilonalo kwenye kila sekunde ya uhai wa Mtanzania.Don't get me wrong kuwa ninajifanya kuelewa sana mambo haya lakini ukweli ni kwamba taaluma ya ushushushu ni uti wa mgongo wa uhai wa taifa lolote lile duniani.Idara ya Usalama ya nchi ikiyumba,nchi nayo inayumba.Watu wengi hawaelewi umuhimu wa chombo hiki kwa vile kimaadili kinapaswa kufanya kazi zake kwa siri,japo watoto wa vigogo wanaona usiri huo kama kero.

Anyway,nimekutana na tangazo la ajira za ushushusu katika 'Idara ya Usalama' (wa ndani-yaani ya kuzuia ujasusi) ya Uingereza-MI5 au kwa kirefu Military Inteligence,Section 5)-ambalo limewekwa kwenye gazeti la bure la kila siku la METRO.Utaratibu huu ambao sitarajii kuuona ukiigwa na taasisi nyingi za usalama duniani,achilia mbali yetu,unaweza kusaidia sana kufanya zoezi zima la kuajiri (recruitment process) kuwa ya huru,wazi na inayowekea mkazo uwezo,ujuzi na sifa za mwombaji kazi (based on merit(s)).

Hii ni mada nyeti kwahiyo naomba niishie hapa.Ukiwa na swali,usisite kuniuliza (majibu yatategemea swali limeulizwaje).

Related Posts:

  • ISRAEL'S SHIN BET WARNS OF FACEBOOK "SPIES"Israel's internal intelligence service urged the public today to exercise caution when using Facebook, saying Arabs are trying to recruit spies on the popular social networking site.The Shin Bet security agency warned Israeli… Read More
  • EX-MI6 CHIEF CONCERNED ABOUT BRITISH BIG BROTHER SURVEILLANCE SOCIETYThe former head of MI6 says he is concerned about the big brother surveillance society and the 'loss of liberties' in Britain. Sir Richard Dearlove said the extensive use of anti-terrorist stop and search powers by the Metrop… Read More
  • THE POWERFUL, SHADOWY MOSSAD CHIEF MEIR DAGANThe brazen assassination of Mahmoud al-Mabhouh has thrown the spotlight on one of Israel’s most powerful but shadowy figures, Meir Dagan, the current Mossad chief, who yesterday faced calls for his resignation.There is a piec… Read More
  • GCHQ DENIES SNOOPING CLAIMThe government's electronic eavesdropping centre has issued a rare response to accusations that it plans to install thousands of black boxes to monitor all internet and telephone use in Britain.In a statement, GCHQ denied its… Read More
  • MI5 TURNS 100MI5: To defend the realmBritain's counter-intelligence agency turns 100 next month. Historian Nigel West looks at the service's success, its secrets and scandals by Nigel West 26 Sep 2009Happy Birthday, MI5. The UK's counter-… Read More

1 comment:

  1. Mr. Evarist: its true kutokana na yote uliyoyasema... lakini kwa Tanzania taifa letu, nahisi hawapo kwaajili ya Usalama wa taifa ama Usalama wa nchi....... labda ni kwa faida zao binafsi. na je kuna vigozo gani unapotaka kuomba nafasi ktk usalama wa taifa.....??? samahani ningeppenda unijibu inbox kwa E-mail zolfiqrashid@rocketmail.com

    ReplyDelete

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget