Wednesday, 30 January 2008

Pamoja na mambo mengine,makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inatoa changamoto kwa vyombo vya habari vya Tanzania kutumia ipasavyo teknolojia ya habari kwa kuwezesha habari zao kupatikana mtandaoni.Pia nimegusia kwa kifupi "tangazo" la Balozi Ali Karume kuhusu dhamira yake...

Tuesday, 29 January 2008

Does a ringtone tell anything about a mobile phone's owner?Well,for more than 2 yrs now I've just stuck by one old song,Toploader's Dancing in the Moonlight .What about you?Here's the song's video (it's the flavour-especially kinanda -organ,accordion or whatever)-that I really like,and not the video actually)Some other clips...for Tuesday.Busta Rhymes ft Mariah Carey-I Know What You WantPharrell ft Snoop-That GirlATL-Calling All GirlsLil' Flip ft...

Thursday, 24 January 2008

Siku chache zilizopita Wamarekani waliadhimisha siku ya Dakta Martin Luther King Jr,mmoja wa wapigania haki za Waamerika Weusi.Historia inamkumbuka Dkt King (aliyezaliwa mwaka 1929 na kuuawa kwa risasi mwaka 1968)kama nguzo muhimu katika kupigania haki za Waamerika Weusi nchini humo.Pengine kilichomfanya...

Wednesday, 23 January 2008

Alfajiri hii nimepata barua-pepe kutoka kwa mtu mmoja anayeelekea kuumia moyo kwa namna navyoshutumu ufisadi na mafisadi.Mzembe huyo ametoa shutuma lukuki kuhusu makala zangu magazetini na humu "bloguni" kuhusiana na suala la ufisadi.Kwa kutompa ujiko aliokuwa anatafuta,nimeamua kupuuza barua-pepe hiyo na sikumjibu.Binafsi,nilikuwa natambua bayana kwamba mafisadi wameshabaini kwamba mtandao una nguvu pengine zaidi ya magazeti yetu huko nyumbani,hasa...

Rafiki yangu mmoja amenitumia barua-pepe muda mfupi uliopita baada ya kusoma makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema.Hakuwa na pongezi wala malalamiko bali alidai kwamba wakati anasoma makala hiyo alijiskia kama anaongea nami uso kwa uso japo tuko umbali wa maili elfu kadhaa.Ni...

Tuesday, 22 January 2008

Usiku huu (kwa saa za hapa Uingereza) msanii wa Bongofleva,T.I.D,alifanya mahojiano mafupi na kituo cha runinga cha BEN cha jijini London,kuhusu ziara ya msanii huyo nchini hapa.Inapendeza kuona msanii kutoka nyumbani akihojiwa,lakini nahisi kulikuwa na tatizo kidogo katika mfumo wa mahojiano hayo ambapo kwa mtizamo wangu,nadhani mtangazaji alitaka interview iwe ya Kiswahili lakini T.I.D alijibu maswali mengi kwa "Lugha ya Mama" (kimombo),japo sina...

Monday, 21 January 2008

Wafuatiliaji wa blog hii watakuwa wameshasoma mara kadhaa niki-confess kwamba mie nina "allergy" na masuala ya namba (hisabati).Sasa hii mada fupi nayoandika inahusu uchumi,na kwa "kilaza" wa namba kama mie,ipo kazi kuiwasilisha vema ieleweke.Ntajitahidi hivyohivyo.Jana,masoko mbalimbali ya fedha (au...

Sunday, 20 January 2008

Siku chache zilizopita,ndege aina ya Boeing 777 ya British Airways ilinusukirka kusababisha maafa makubwa baada ya kupata matatizo wakati linajiaandaa kutua katika uwanja wa ndege wa Heathrow.Marubani na wafanyakazi wengine wa ndege hiyo (iliyokuwa na abiria 152) waliibuka mashujaa kwa namna walivyoweza...

Makala hii ilitoka kwenye gazeti la Mtanzania siku ya Alhamisi 17Jan 2008.Hatimaye ugavana wa Dkt Daudi Ballali katika Benki Kuu ya Tanzania umetenguliwa.Sijui kama utenguzi huo ni sawa na tunachosoma,kuona na kusikia kwenye vyombo mbalimbali vya habari kwamba Balali amefukuzwa kazi.Pengine la muhimu kwa sasa ni kwamba mtu huyo ametolewa katika wadhifa huo japo la muhimu zaidi ni kuweka rekodi vizuri kwa minajili ya kuondoa utata uliojitokeza hasa...

Saturday, 19 January 2008

Miongoni mwa matukio ya mwaka jana yaliyoathiri huduma hapa Uingereza ni pamoja na mgomo wa wafanyakazi wa Royal Mail (kufupisha maelezo,tuliite "shirika la posta la hapa").Pamoja na madai mengine yaliyopelekea mgomo huo,ni upinzani wa wafanyakazi hao dhidi ya mpango wa Royal Mail kuongeza teknolojia ambazo zingepelekea kupunguza wafanyakazi.Teknolojia ina faida na hasara zake,na moja ya "hasara" kubwa ni kupunguza utegemezi wa binadamu katika sehemu...

Friday, 18 January 2008

Siku chache zilizopita nilizungumzia kuhusu "afya" ya muziki wa Bongofleva.Dhamira ya makala hiyo ilikuwa ni kuwaamsha wahusika na kuwakumbusha kwamba japo ni vizuri kula matunda ya jasho lao,wanapaswa kuwa makini wasije kujikuta wanakata kabisa na mimea inayotoa matunda hayo.Leo napenda kuzungumzia nafasi ya muziki huo katika kuleta mabadiliko kwenye jamii.Nilisoma mahala flani kuhusu lawama dhidi ya rapa maarufu huko Marekani,Jay-Z,baada ya kutoa...

Nimekuwa mwandishi wa makala magazetini tangu mwaka 1998,takriban miaka 10 sasa.Mtu aliyenipa changamoto la kufanya hivyo anaitwa Albert Memba,mwandishi wa zamani wa habari za michezo katika gazeti la Nipashe na Guardian.Huyu jamaa anaimudu lugha vilivyo.Nilianzaia kwenye magazeti "ya udaku" kama Sanifu...

Thursday, 17 January 2008

Gavana mpya wa Benki Kuu,Profesa Benno Ndulu,amefanya mabadiliko kadhaa katika uongozi wa benki hiyo.Katika mabadiliko hayo,Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala (DAP) wa B.O.T,AMATUS LIYUMBA (pichani) ameondolewa katika wadhifa huo.Habari kamili soma hapa. (Picha hii ya zamani ya Liyumba ni alipokuwa Mkuu...

Wednesday, 16 January 2008

Wiki iliyopita ilitawaliwa na surprises mbili:huko New Hampshire,Marekani,Hillary Clinton aliibuka mshindi kwenye primaries za chama cha Democrats,kinyume kabisa na utabiri wa awali wa waendesha kura za maoni na wachambuzi wa siasa za nchi hiyo.Na huko nyumbani,ugavana wa Daudi Balali ulitenguliwa.Wakati...

Tuesday, 15 January 2008

Hivi msomaji wangu mpendwa ulishaota ndoto ngapi za "ningependa kuwa flani" kabla hujafika hapo ulipo?Kwangu ni 3,moja naendelea kuhangaika nayo,na kwa Mapenzi yake Mola+jitihada zangu,natarajia kuitimiza miezi michache ijayo.Naomba niihifadhi ndoto hiyo kwa sasa.Ndoto yangu kwanza utotoni ilikuwa kuwa daktari.Sehemu ya elimu yangu ya msingi na O'level ilipatikana katika shule zilizokuwa karibu na hospitali flani yenye CV ya kuridhisha (imezaa madaktari...

Monday, 14 January 2008

Jana niliweka makala fupi kuhusu documentary ya gereza la San Quentin iliyoonyeshwa na BBC2.Baadaye leo nimepata comment kutoka kwa ndugu yangu TAFAKARI kwamba ilishindikana ku-download documentary hiyo kwa sababu teknolojia ya iPlayer ya BBC kwa sasa hairuhusu mkazi wa nje ya Uingereza ku-download chochote kinachokuwa posted huo.Ashakum si matusi,but this is absolutely bulls**t.Kwa vile mtumishi wenu nilikuwa na kiu ya ku-share nanyi kilichojiri...

Sunday, 13 January 2008

Muda mfupi uliopita nilikuwa naangalia documentary moja ya Louis Theroux kuhusu maisha ndani ya San Quentin State Prison,one of the toughest and most dangerous in the U.S. of A.Katika documentary hiyo iliyoonyeshwa BBC2 Louis alipewa access ya wiki mbili ndani ya jela hiyo,na kwa hakika simulizi na...

Saturday, 12 January 2008

Afrika imetoa mastaa kadhaa waliotamba na wanaotikisa nchini Marekani na duniani kwa ujumla."Zaire" ilitupatia Dikembe Mutombo na Senegal imetuzawadia Akon.Tanzania nayo inaelekea kupata kitu zaidi ya umaarufu wa Mlima Kilimanjaro au mbuga ya Selous.Hapa namzungumzia TK...TEDDY KALONGA,Mtanzania anayeleta...

Wednesday, 9 January 2008

Baada ya Barack Obama kuibuka kidedea huko Iowa,kuna wengi walioanza kuamini kwamba sura mpya imefunguliwa katika siasa za Marekani.Mimi sikuwa mmoja wao,na ushahidi unapatikana kwenye makala zangu zilizopita kuhusu ushindi huo wa Obama.Katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema nimejaribu kuangalia...

Tuesday, 8 January 2008

Inatia uchungu,inasikitisha na inakasirisha kuona uhuni anaofanya Mwai Kibaki wa kuamua kutangaza baraza la mawaziri ilhali anafahamu fika kwamba hatua hiyo itakwaza jitihada za kutafuta amani zinazoendelea nchini humo.Nadhani Kibaki anakwepa kwa makusudi jitihada hizo kwa vile anafahamu fika zinaweza...

Sunday, 6 January 2008

Kuna mengi yanasemwa kuhusu mwelekeo mzuri wa Barack Obama katika harakati zake za kuingia Ikulu ya Marekani baadaye mwaka huu.Lakini,je mafanikio ya Obama yanamaanisha kukubalika kwa asilimia 100 kwa mtu mweusi katika jamii ya Waamerika au ni matokeo ya kukwepa kile "weusi wenzie" kama Jesse Jackson...

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget