Wednesday, 07 March 2012 19:31 |
Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa Ramadhan Semtawa UTATA umegubika afya ya Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa baada ya taarifa mbalimbali kueleza kuwa yuko hospitalini nchini Ujerumani kwa matibabu.Takriban juma moja sasa kumekuwa na taarifa mbalimbali zikizungumzia afya ya Lowassa lakini hakukuwa na taarifa rasmi kutoka chanzo chochote kati ya Serikali, familia yake au Bunge kuzungumzia afya ya Mbunge huyo wa Monduli. Jana, Lowassa akizungumza na mwandishi wetu kwa simu alisema kwamba yuko hospitali, bila kufafanua kuwa ni nje au ndani ya nchi, wala kueleza kinachomsibu. Mahojiano hayo kati ya Lowassa na mwandishi wetu yalikuwa kama ifuatavyo: Swali: Asalaam alaykum Mheshimiwa Lowassa. Jibu: Waalaykum Salaam. Swali: Mimi naitwa... (jina la mwandishi) kutoka gazeti la Mwananchi. Kwanza pole kwa matatizo ya kiafya yanayokusumbua. Jibu: Ahsante. Swali: Nimekupigia pamoja na kukupa pole, nilitaka kujua unaendeleaje na matibabu? Jibu: Niko hospitalini kwa sasa naomba niache mambo mengine tutaongea baadaye. Swali: Lakini, ni matibabu gani hasa unayopata? Jibu: ... (akimtaja mwandishi) naomba niache niko hospitalini sasa hivi mambo mengine tuongee baadaye. Lowassa alitoa majibu hayo majira ya saa nane mchana na alipopigiwa tena saa 10.20 jioni, alijibu kama ifuatavyo: Swali: Naam, Mheshimiwa Lowassa nimekupigia tena mimi... (mwandishi akajitambulisha). Jibu: ... Unataka nikuambie nini tena? Nilishakwambia niko hospitalini niache! Swali: Sawa, natambua uko hospitalini, lakini wewe ni kiongozi ambaye umewahi kuwa Waziri Mkuu, hivyo Watanzania wangependa kujua maendeleo ya afya yako kutokana na utata ulioibuka na kama je, umelazwa hapo hospitalini au uko katika matibabu ya kawaida? Jibu Niache, ninachokwambia niko hospitalini sasa unataka nini tena? Nisingependa kuzungumzia afya yangu kwa undani. Bunge Akizungumzia suala hilo juzi, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah alisema ofisi hiyo haijapata maombi rasmi ya mbunge huyo kwenda nje kwa ajili ya matibabu. Dk Kashillilah alisema kwa utaratibu, Ofisi ya Bunge inashirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya kuwapeleka wabunge wanaoumwa nje ya nchi baada ya kupata rufaa ambayo inatokana na ushauri wa kitaalamu wa madaktari wa ndani. Alisema hadi juzi, hakuwa akijua aliko Lowassa na kama ana matatizo ya kiafya kama inavyozungumzwa au la: “Mimi ndiyo Ofisi ya Bunge na ndiyo nakwambia hatujapata maombi ya kutaka mheshimiwa Lowassa apelekwe nje ya nchi.” Mtendaji huyo mkuu wa Bunge alisema wapo baadhi ya wabunge ambao huwa wanakwenda nje kwa vipindi maalumu kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa kawaida wa afya baada ya matibabu lakini, katika orodha hiyo Lowassa hayumo. “Tunao utaratibu wa baadhi ya waheshimiwa wabunge kwenda nje kwa mujibu wa ratiba zao kwa ajili ya kufanyiwa uangalizi wa kawaida wa afya zao. Lakini, hadi sasa (juzi) katika orodha hiyo mheshimiwa Lowassa hayumo,” alisema Dk Kashillilah. Hata hivyo, kwa mujibu wa nafasi yake ya utumishi serikalini aliyokuwa nayo, Lowassa anaweza kupata matibabu nje ya nchi kwa kupitia utaratibu wa Serikali bila ya kuhusisha Bunge. Juhudi za kupata Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda au Naibu wake, Dk Lucy Nkya zilishindikana kutokana na simu zao kufungwa na kutopatikana ofisini. CHANZO: Mwananchi |
Thursday, 8 March 2012
17:03
Unknown
EDWARD LOWASSA
No comments
Related Posts:
Dkt Slaa Apuuza Uropokaji wa Salva.Amtaka Kikwete Ajiuzulu Kuhusu DowansPicha Hii Inatoa Maelezo Alfu Kidogo.Ukiangalia kwa Makini Utamwona Rostam Kama Kalizimishwa Kuinua Mkono,huku Kikwete Akiwa as if Anampigia Debe Bosi Wake...na Tabasamu Juu!Lol,Ama Kweli Rais Tunaye,Si MchezoDk. Slaa: Kikwet… Read More
CCM: Joka Lenya Vichwa Vitatu Linaweza Kusalimika Likikatwa Vichwa Viwili?Habari zilizopatikana kutoka Dodoma kwenye kikao cha CCM chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete zinaeleza kuwa baadhi ya viongozi waadamizi wa chama hicho wamevuliwa madaraka.Kwa mujibu wa vyanzo vya mtandaoni,waliokumbwa … Read More
Tofauti za Lowassa na Rostam kuhusu "Babu": Mpasuko au Wanatuzuga tu?"Tiba ya Babu" imeibua kila aina ya vimbwanga.Nikianza kuviorodhesha vimbwanga hivyo basi tutakesha kwani kila kukicha kuna mapya.Mara tusikie wagonjwa waliotoroka mahospitalini "wamefumaniana" na madaktari waliotorokwa na wa… Read More
Kikwete Tumechoka,No More Drama Chukueni Mabilioni Yenu ya DowansKwa hakika inachosha kila unapoingia mtandanoni na kukutana na episode mpya ya sakata la Dowans.Tangu mwanzo ilishabainika Rais Jakaya Kikwete yuko upande gani katika ishu ya ujambazi wa waziwazi (daylight robberies) uliosham… Read More
Tanzania Daima Wana Siri Gani na Lowassa?Katika siku za hivi karibuni,gazeti la Tanzania Daima limeonekana kama linafanya juhudi za wazi kuiweka profile ya Edward Lowassa machoni na masikioni mwa wasomaji wa gazeti hilo.Ukidhani observation hii ni ya majungu,basi na… Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment