Pinda: SIJUI Waziri Nahodha anaishi hotelinina Martin Malera, DodomaWAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amesema hajui kama Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, anaishi hotelini.Kauli hiyo aliitoa jana bungeni baada ya kuulizwa swali na mbunge wa Chambani, Salim Hemed Khamis (CUF), alihoji dhamira ya serikali kupunguza matumizi.Mbunge huyo alihoji kwa nini Waziri Nahodha anakaa hotelini wakati serikali ina nia ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.“Kuna mawaziri wanaishi hotelini tangu walipoteuliwa hadi sasa, serikali haioni kama hali hiyo ni kikwazo kwa mafanikio ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano tulioupitisha hivi karibuni Bungenin?” alihoji mbunge huyo.Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu Pinda kwanza alionekana kushangazwa na taarifa hiyo na baadaye alimtaka mbunge huyo ataje majina ya mawaziri anaowajua wanaioshi hotelini hadi sasa tangu walipoteuliwa.Mbunge huyo alitaja jina la Waziri Nahodha.Huku akiwa haamini na kumkazia macho Waziri Nahodha, Pinda alijibu kwa kifupi tu: “Basi nimesikia.”Katika hatua nyingine, Spika Anna Makinda, alimzuia Waziri Mkuu Pinda kujibu maswali ya Mbunge wa Singida Vijijini, Tundu Lisu, na Esther Matiku wote CHADEMA, yaliyohusu mauaji ya raia katika mgodi wa kampuni ya Barrick, Tarime mkoani Mara
Saturday, 18 June 2011
15:22
Unknown
MIZENGO PINDA
No comments
Related Posts:
Tafakuri ya Nova Kambota: Pinda Kubali Kufa Ili Uione PepoNa Nova Kambota,Namkumbuka mwanamuziki wa kizazi kipya Seleman Msindi maarufu kama Afande sele na kile kibao chake cha “Darubini kali” anapohoji “kama unapenda pepo kwanini uogope kifo?”Tungo hii kwa namna ya pekee inamgusa w… Read More
EXCLUSIVE TO KULIKONI UGHAIBUNI: Rais Kikwete Azungumzia Kauli ya Pinda Kuhusu Posho za WabungeRais Jakaya Kikwete amekiri kuwepo kwa mkanganyiko uliojitokeza kufuatia kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuwa Rais ameridhiria nyongeza ya posho za Wabunge.Rais alisema hayo katika majadiliano kati yangu na yeye kupitia mt… Read More
Familia ya PINDA Yahamia CHADEMA? (PICHA)A PICTURE COULD TELL A MILLION WORDS: Dogo anaonekana akitoa alama ya V (for victory over mafisadi) huku Mtoto wa Mkulima akionekana kupigwa na bumbuwazi! CHANZO: Jamii Forums… Read More
Kilio Kumwokoa tena Pinda?Anyway,yeye na Mawaziri Wake ni Dalili tu,Chanzo ni KikweteWaziri Mkuu Pinda akifanya usanii wa kulia bungeni katika sakata la maalbino.Je hatorejea tena mbinu hii?Tusiume maneno.Tanzania hivi sasa inayomba kwa vile Rais tuliye nae,Jakaya Kikwete,ni mithili ya mtu asiyejua kwanini Wa… Read More
Pinda Kumfuata Lowassa?Pinda kumfuata Lowassa• HATMA YA MAWAZIRI WATANO MIKONONI MWA JKna Mwandishi wetuWAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, sasa yuko katika hatari ya kuondolewa madarakani kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kufuatia tuhuma nzito … Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment