Monday, 18 July 2011




Kama kuna kosa ambalo Watanzania watalijutia kwa muda mrefu sana ni lile walilofanya mwaka 2005 na kisha kulirudia mwaka jana kumchagua Jakaya Kikwete kuwa Rais wa nne wa Tanzania.Tusiume maneno,mengi ya matatizo yanayoikabili nchi yetu kwa sasa ymesababisha,yanasababishwa au yamechangiwa au yanachangiwa na ubabaishaji wa Kikwete.

Ni nani mwenye akili timamu asiyefahamu kuwa wakati kelele dhidi ya ufisadi zinaelekezwa kwa "mapacha watatu" waliobaki wawili (ie Lowassa na Chenge,na Ristam aliyejiuzulu),Kikwete ni sehemu muhimu kabisa ya tuhuma zinazoelekezwa kwa wanasiasa hao.Hapa simaanishi kuwatetea mafisadi hao bali ninachojaribu kupigia mstari ni ukweli kwamba Kikwete hana tofauti na Lowassa,Chenge au Rostam.Na hilo halihitaji ufafanuzi.Yeye anajua,mapacha watuatu waliobaki wawili wanajua,na kila Mtanzania mwenye akili tiammu anajua.Kwanini hadi leo Kikwete bado ni Rais wetu ni swali gumu kulijibu just like lile la kwanini alichaguliwa mara ya kwanza mwaka 2005 na baadaye 2010 ilhali wanamjua walikuwa wanatambua bayana kuwa hana sifa za kushika wadhifa huo mkubwa kabisa katika nchi yetu.

Anyway,lengo la makala hii sio kujadili ubabaishaji wa Kikwete katika utendaji kazi wake bali lengo ni kukemea kwa nguvu kubwa uhuni uliofanywa na Kikwete wa kufanya harusi ya mdogo wake kwenye Ikulu ndogo ya Bagamoyo.Hivi kwa kuwa Rais,Kikwete anadhani kuwa Watanzania wametoa urais kwa ukoo wake mzima?Kwanini asikodi ukumbi kwa fedha zake kisha akamfanyia sherehe mdogo wake?

Kama huelewi kwanini ninalamika,Ikulu iwe ile ya Magogoni au hizo ndogo za wilayani na mikoani ni mahala patakatifu-kama alivyowahi kusema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.Si mahala ambapo kila Tom,Harry and Dick anaweza kufanya atakalo.Lakini licha ya utakatifu huo wa Ikulu,ifahamike kuwa mahala hapo panaendeshwa kwa fedha za walipakodi.Kwa mantiki hiyo,kufanyia sherehe mahala hapo ni sawa na kuwabebesha gharama Watanzania kwa ajili ya harusi ya ndugu wa Kikwete.Sidhani hata waliompigia kura mwaka jana au 2005 walitamani kuona kura waliyompigia Jakaya inageuzwa kuwa mithili ya kuupigia kura ukoo wake mzima.

Huu ni uhuni unaopaswa kukemewa vikali.Rais anaweza kuzurura nje ya nchi atakavyo (inaelekea kama hakuna namna ya kumwelewesha kuwa safari zake za mara kwa mara nje ya nchi ni mzigo mkubwa kwa Watanzania) lakini kamwe tusiruhusu nafasi ya Urais ikageuzwa kuwa kama cheo cha kifamilia.

Madhara ya kumwacha Kikwete aendelee na madudu yake ni kwamba anaweza kumaliza muda wake hapo 2015 na kuiacha Tanzania ikiwa jina tu-haina maadili,haina raslimali,na kibaya zaidi,nafasi ya urais ikaishia kuwa na heshima ndogo kuliko ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa.

PICHA: Kwa hisani ya Global Publishers

Related Posts:

  • Ah,JK Vipi Mbona Haeleweki?Kwa hakika baadhi ya kauli za Rais wetu Jakaya Kikwete zinachanganya kupita kiasi.Juzijuzi tu alisaini kwa mbwembwe sheria tuliyoambiwa imelenga kudhibiti rushwa katika chaguzi.Tukiweka kando suala la wasaidizi wake kumwingiz… Read More
  • REDET: Pinda Mchapakazi Zaidi Ya Kikwete na SheinMatokeo ya utafiti uliofanywa na Mradi wa Utafiti na Elimu na Demokrasia Tanzania (REDET) yanaonyesha kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ni mchapakazi zaidi ya 'bosi' zake,Rais Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Ali Mohammed Sh… Read More
  • JK Anatania,Tendwa Anatania,Na Siasa Zetu ni Utani MtupuOfkoz,Mtukufu Rais Jakaya Kikwete alikuwa anatania alipotetea rushwa hadharani kwa kudai takrima haikwepeki.Ndio,Rais alikuwa anatania,na ndo maana,Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa amekaririwa na magazeti kadhaa akimtet… Read More
  • Kama Hii Ni Kweli Basi TUMEKWISHAHapa chini kuna habari ambayo kama ni ya kweli basi hatma ya nchi yetu iko mashakani.Lakini kabla hujaisoma,angalia picha ifuatayo na inaweza kukusaidia kukupa uelewa wa namna tulivyofika tulipo.KUMBE Rais Jakaya Kikwete haku… Read More
  • Jini Ndani ya Chupa...Likitoka LimetokaNadhani unamfahamu Christina Aguillera,na kama unamfahamu basi ni dhahiri utakuwa unakumbuka 'singo' yake ya kwanza kabisa Genie in a Bottle (Kama huukumbuki basi cheki video hii hapa).Ushaikumbuka?Well,lengo la makala hii si… Read More

0 comments:

Post a Comment

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget