JK alisaini sheria hiyo kwa mbwembe kama alivyoahidi.Siku chache baadaye,Dkt Wilboard Slaa akaibua hoja kuhusu 'usanii' uliofanyika kuongeza vipengere katika Sheria hiyo.Spika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakatetea 'usanii' huo.Licha ya mlolongo wa matukio hayo kuashiria kuwa sheria hii yenye nia njema itabaki kuwa maandishi tu,walengwa wakuu wa sheria hiyo wameamua kuipuuza na 'misaada' inatolewa kama kawaida katika kujitengenezea mazingira ya ushindi kwenye uchaguzi. Dk. Nkya kujitosa ubunge Morogoro Kusini Mashariki
na Joseph Malembeka, Morogoro
NAIBU Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Lucy Nkya, ametangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Morogoro Kusini Mashariki.
Dk. Nkya alitangaza nia hiyo akiwa katika ziara ya kukagua maenndeleo na utekelezaji wa ahadi alizotoa baada ya kuchanguliwa kuwa mbunge wa Viti Maalum.
“Nawatakeni wanachama wenzangu ndani ya CCM muelewe kuwa na mimi nakuja huku mbali na kuwa kuna wenzangu waliotangaza nia hii,” alisema Dk.Nkya.
Dk. Nkya ambaye kwa nyakati tofauti alikabidhi vitu mbalimbali yakiwemo mabati, vipaza sauti, saruji, vyerehani, misumari, baiskeli na fedha taslimu sh 1,500,000 kwa wananchi na wana CCM katika kata mbalimbali aliwataka wana CCM kukiimarisha chama na wao kiuchumi.
“Sasa hivi tunakwenda kwenye hekaheka za uchaguzi ila nawatakeni mbali na siasa jiimarisheni kiuchumi kwa kulima mazao yanayokomaa kwa muda mfupi na yanayostahimili ukame tuepukane na janga la njaa,” alitahadharisha Dk. Nkya.
Dk. Lucy Nkya anakuwa miongoni mwa watu saba walioonyesha nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo. Wengine ni mbunge wa sasa wa jimbo hilo (Samir Lotto), Jamira Mohamed, Amani Mwenigoha, Gabriel Mkwawe, Semindu Pawa na Salumu Salum Mkangala.
CHANZO: Tanzania Daima.
Thursday, 8 April 2010
Related Posts:
Bloga Nkwazi Mhango anituhumu kuwa nimehongwa na Lowassa...kisa SHAIRIMmoja ya mabloga ninaowaheshimu,Bwana Nkwazi Mhango (pichani juu) amenishushia tuhuma nzito akidai nimepokea hongo ya mafisadi kama inavyoonekana kwenye baruapepe ifuatayo (BONYEZA PICHA KUIKUZA)Kama hukuweza kuisoma vizuri b… Read More
Huku Madaktari Wakigoma Kudai Maslahi Bora,Sh Bilioni 86 Zafisadiwa SerikaliniWAFANYAKAZI WA HAZINA, TANESCO NA WIZARA YA NISHATI WAHUSIKA, NGELEJA ATHIBITISHA UCHUNGUZI KUFANYWAMwandishi WetuSERIKALI inawachunguza baadhi ya maofisa wake waandamizi kwa tuhuma za wizi wa dola50 milioni za Marekani saw… Read More
Duh,Yaani Hata "Marejesho ya Fedha za Kifisadi za EPA" Yafisadiwa Pia!!Vigogo watafuna marejesho ya EPA Thursday, 03 November 2011 21:27 Leon Bahati na Furaha MaugoKAMATI ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imebaini ufisadi mwingine wa mabilioni ya fedha kwenye marejesho ya zile zilizochotwa … Read More
Tafakari Simulizi Ifuatayo Kisha Ilinganishe na Malipo kwa DowansNimetumiwa na mdau Tluway Tsere,nami naiwasilisha kama ilivyo Habari za asubuhi Ndg. zanguTutafakari hii hadithi fupi, kwani mimi sikulala usingizijana baada ya kusikia kuwa Tuzo ya Rostam Aziz imekubaliwaena mahakama kuu. W… Read More
Kama JK alifanya Haya Akiwa Waziri,Ameshafanya Mangapi Zaidi Tangu Awe Rais?Balozi Mahalu amlipua JK mahakamani Wednesday, 29 February 2012 07:31Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa MahaluANIKA ALIVYOSHIRIKI KATIKA MCHAKATO KIPINDI AKIWA WAZIRI MAMBO YA NJE, ASEMA ALIKUTANA … Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment