SOURCEJuly 9, 2007Weirdest workplace disputesLast week, the Employment Appeal Tribunal celebrated its 30th anniversary. We marked the occasion by trawling the archives and dusting off some of the more colourful UK employment disputes from the past few years.Alex Wade and Alex Spence14. CSI: Farnham. Tony Price, the managing director of WStore UK, an IT company based in Surrey, demanded that his 80 staff submit to a DNA test after a piece of chewing gum got stuck to a directors’ suit trousers. When his global e-mail pointing out the firm's chewing gum ban leaked to the media, Price cheekily suggested he would force staff to take lie detector tests to flush out the culprit.13. Hands on treatment. A 34-year-old masseuse sued the prestigious Old Course Hotel at St Andrews for unfair dismissal and sexual discrimination after she was allegedly fired for accusing an A-list celebrity client of lewd conduct; the employment tribunal later identified the celebrity as Kevin Costner after his name was posted all over the internet. According to the masseuse, the Dances With Wolves star removed his towel and asked her to "touch him everywhere". Costner, who was on his honeymoon and taking part in a golf tournament, denied the accusation vehemently. The hotel later settled with the woman.12. Porn at sea? No thanks. The cliché of men in the armed serves cheering themselves up with top-shelf literature is well established, but it was too much for the Reverend Mark Sharpe, 37. The trainee chaplain left the Royal Navy declaring himself “horrified” by the amount of pornography below decks and issued a claim for sexual harassment and discrimination on the ground of his religious beliefs. At a tribunal in Exeter, the Navy admitted sexual harassment but denied the religious discrimination charge. Reverend Sharpe accepted an undisclosed sum in damages and is now a rural rector.11. Fine whine. A Muslim insurance salesman took offence when his employer began offering bottles of wine for good performance. Imran Khan, 25, said that Direct Line’s incentivisation scheme put him at a disadvantage because his religion forbade him to drink alcohol, and he sought damages for “hurt feelings”. He lost.10. Witches have rights, too. Sommer de la Rosa, a former teaching assistant at the Dorothy Stringer School in Brighton, accused the school of unfairly dismissing her because she was a witch. The 34-year-old claimed she had been made to “feel like a freak” after she was forbidden from wearing a pentagram and colleagues compared her Wiccan beliefs to communism. The school claimed she had been let go because of her poor attendance. The dispute was settled out of court.9. Chard is for lovers. Sally Bing, a 31-year-old town clerk, won her claim for sexual discrimination and victimisation against the mayor of Chard, Tony Prior, after the 67-year-old putative lothario became infatuated with her. “We were standing shoulder to shoulder looking at a wall map of Chard,” the mayor explained. “When she stood close to me, it sent a sexual thrill through me. That was possibly when I wondered whether she had sexual feelings towards me.” The married Prior invited Bing on a walking tour of Andorra, and his advances eventually became so bad she rearranged the furniture in her office to create an escape route in case he appeared. Bing was awarded £25,000 from the council and £33,697 from Prior. And all that from staring at a map of Chard.8. Wicked witchcraft. Sariya Allen, a teaching assistant who quit her job after three years at Durand primary school in Stockwell, London, sued the school for allegedly discriminating against her Pentecostal Christian beliefs. Allen had been disciplined for refusing to let a child read Harry Potter, claiming it glorified witchcraft. She lost.7. Don’t call me ginger. Sarah Primmer, a 41-year-old former waitress at the Rendezvous Café in Plymouth, was awarded a “staggering” £17,618 for unfair dismissal and sexual harassment after suffering taunts over her ginger locks. Primmer alleged the café’s night manager had made a series of lewd and embarrassing comments in front of other staff because “they wanted to know if the colour of my hair matched the rest of my body”. Despite her vindication in the eyes of the law, Primmer was intent on ridding herself of her affliction. “I am going to try and get it lighter and lighter,” she said. “It is not nice to be ginger.”6. Man’s best friend. David Portman successfully sued the Royal Mail for unfair dismissal after he lost his job for taking time off to mourn the death of his dog. The postman had missed 137 days in five years for reasons including breaking his foot when pushing mail through a letter box, spraining his ankle when standing on a piece of wood and being injured in a car accident. Throughout, his faithful hound Brandy had provided unstinting companionship. When one morning he found her dead at the foot of his bed, Portman took her demise badly and failed to show up to work for a week. He returned to find he had been sacked. A tribunal found that “none of the claimant’s absences were for other than wholly legitimate and genuine reasons”.5. Foamy sales pitch. Wayne Simpson, an EDF Energy salesman, lost his £28,000-a-year job after he sent a customer a picture of himself sitting naked drinking whisky in a bubble bath. Simpson had met the female customer while selling door-to-door on Tyneside; he obtained her number and later sent the picture with a message saying, “Fancy going out for a drink sometime?” The woman didn’t and instead reported him to the company and the police. Simpson accused EDF of lacking a sense of humour. “I wasn’t even showing off my naughty bits,” he said.4. The farting chair. Sue Storer, a 48-year-old teacher at Bedminster Down Secondary School in Bristol, sought damages of £1 million for sex discrimination and constructive dismissal claiming she had been forced to sit in a chair that made embarrassing sounds every time she moved. “It was a regular joke that my chair would make these farting sounds and I regularly had to apologise that it wasn’t me, it was my chair,” she said. Requests for a new chair had been repeatedly ignored while male colleagues were given sleek, executive-style chairs, she said. Her claim was thrown out.3. Look out for the flour. Caroline Gardener, a lesbian shop worker at a Booker Cash and Carry, won her claim for unfair dismissal after she was fired following an altercation with a customer. Gardner, of Eastleigh, Hampshire, claimed a customer abused her because he couldn't find any lime cordial, telling her to "Get your sex life sorted out." She responded by throwing a bag of flour at him. “When he called me a filthy dyke I had a pack of flour in my hand and, although I regret it now, I threw it at the back of his head,” she admitted. “He then turned round and said, ‘You are a dyke and you’re going to get the sack’.” Gardner lost other claims for breach of contract and discrimination on the grounds of her sexual orientation.2. Legal tender? Fred Raine was awarded £2,300 after an industrial tribunal agreed that his former employer, Lee’s Coaches, in Langley Moor, had underpaid him when he left the company due to illness in 2005. Nothing out of the ordinary in that, but the same can't be said for his former boss Malcolm Lee's chosen method of payment. The first £1,000 of Raine's severance pay was paid by cheque, but the remaining £1,300 turned up at his door in the form of a crate full of coins weighing 11 stone. Raine described the gesture as "unacceptable" and said he was consulting his lawyer.1. An axe to grind. James Robertson, a convicted murderer who had served his time and was working as a health inspector for Preston City Council, found himself back behind bars after threatening a colleague with an axe during an argument at an Indian restaurant in 2001. The council (not unreasonably, you might feel) terminated his employment without notice, but Robertson sued for breach of contract. The employment tribunal ruled that the Council had acted illegally in not giving Robertson sufficient notice and ordered it to pay him two weeks’ wages as compensation, amounting to £807.50.
Monday, 30 May 2011
20:22
Unknown
WEIRD STUFF
No comments
Sunday, 29 May 2011
JG: CAN YOU PLEASE INTRODUCE YOURSELF?
ALEX: My name is Alex Kajumulo. I was born in Muleba, Bukoba, Tanzania. Currently, I live in the U.S. (Seattle, Washington) where I coach youth soccer and run my own soccer training program. It's the only soccer program run by an African in Washington State. When I am not coaching soccer, I am making music, writing books, and designing sports clothing and gear.
JG: WHEN DID YOU START DOING MUSIC & WHAT KIND OF MUSIC DO YOU DO?
ALEX: I have loved music my whole life especially when I was a child. I began making music professionally in 1998, collaborating with my good friend Kool James "Mtoto wa Dandu" and the amazing singer Mbilia Bell, from DRCongo. My music can not be labelled by anyone, it is it's own new style. That's why I called my first album "Never Before." You can find this album and all of my music on I-tunes, Spotify, Amazon, and anywhere digital music is sold.
JG: WHAT DO YOU THINK OF BONGO FLAVA & THE KILI MUSIC AWARDS?
ALEX: As a Tanzanian, I love Bongo Flava music. But I don't think Bongo Flava will translate to an international market. If Bongo Flava musicians want to get world wide appeal, they have to do something more original. Someone like Remi Ongallo, who was a true original, his music is still being listened to in the international world music market even today. The music is so good they listen even if they don't understand the language.
You know the Kili Music Awards started from my vision. I wrote up a plan for the Tanzanian Music Awards and gave the plan to James Dandu in 1999. It's not an original idea, it is just a copy of the American Music Awards. James and I presented the first Tanzanian Music Awards. After James died, his wife, Devota, was able to put on one more Tanzanian Music Awards but then she returned to Europe.
The people who are running the Kili Music Awards took the event over and are continuing to this day. They changed the name of the Awards and I do not have anything to do with it. I don't like the way they manage the awards, the awards are only given to insiders and I don't think it is fair and open to all Tanzanian musicians. Our original vision was to recognize original talent no matter who they were, who they knew, or how much money they had. Especially young musicians.
I am working to restart the Tanzanian Music Awards so that I can realize mine and my friend James's vision of making it for all people of Tanzania.
JG: IS THERE ANYTHING THAT YOU THINK SHOULD BE DOEN TO MAKE THINGS BETTER OR IS IT OK THAT WAY?
ALEX: I am happy for them to continue to hold the Kili Music Awards according to their own vision. But it is not my vision and I would like to bring back the Tanzanian Music Awards for the people. One of the awards I am looking forward to presenting is the JAMES DANDU ORIGINAL ARTIST AWARD for the most original Tanzanian musician each year.
JG: WHAT ADVICE WOULD YOU GIVE TO OTHER UPCOMING ARTISTS & YOUNG PEOPLE OUT THERE?
ALEX: You've got to be original. These days anyone can make music and record with digital equipment so in order to stand out you must be original.
JG: WHO HAS BEEN YOUR INSPIRATION?
ALEX: My inspiration is me! I grew with a lot of problems and no one to rely on. I rely on myself for inspiration and I have gone far, but I always put God in front of me for everything I do, but I am not religious.
JG: WHAT DIFFICULTIES DOU YOU FACE & WHAT ARE YOUR ACHIEVEMENTS SO FAR?
ALEX: The most difficult part of being an independant musician is marketing your music and making enough money to eat.
JG: WHERE DO YOU PERFORM IF ONE WOULD LIKE TO SEE YOU PERFOM LIVE?
ALEX: I only really perform for special events that involve social justice. When I do perform, I perform with a large band, at least 8 members. I perform mostly at College venues, Festivals, and big Theatres.
I am currently organizing a large event to promote Malaria Awareness in Kyela District, Tanzania. The "Malaria is Dangerous" concert will be held on Saba Saba Day (July 7) 2011. This will be my second big "Malaria is Dangerous" Concert. The first was held in November of 2010 here in the U.S. YOu can find clips from the concert on my youtube channel. It was also televised locally and broadcast live on the internet to an audience of over 8 million people.
JG: APART FROM MUSIC WHAT OTHER THINGS ARE YOU INVOLVED IN?
ALEX: Soccer is a big part of my life. I have written a book for children called "Soccer Monster" you can see it at www.soccermonster.org. At that website you can also find information about my training program. You can see my youth soccer team at www.kajumulofc.org. You can find out more about me and my music at www.babukaju.com and www.alexkajumulo.com or become my friend on facebook, look for Alex Kajumulo. You can also find me on myspace at www.myspace.com/alexkajumulo. I have over 85 songs on the market, you can buy them at I-tunes or anywhere else and you can see my videos on my youtube channel at www.youtube.com/user/alexkajumulo.
JG: I HAVE HEARD THAT YOU HAVE A BOOK COMING OUT SOON, CAN YOU PLESE TELL US ABOUT IT AND WHERE WE CAN GET OUR COPIES?
ALEX: My latest book is called FADHAA and will be released this summer. It is a novel (fiction) that asks the question, When love ends, does life continue? I wrote my first novel in Swahili because that is my native language and I love my language. I have written this story for the people of my country. Later, FADHAA will be made into a movie, but I am currently shooting a movie called "Searching for Love" which will be released next summer (2012). Of course, I also have the Soccer Monster book for the children of the world. It is written in English because it is a universal sport. I am planning more Soccer Monster books and translations into different languages.
SOURCE: The interview was conducted by Miss Jestina George.You can read the full interview in HER BLOG WHICH IS AVAILABLE HERE (CLICK THIS LINK)
Saturday, 28 May 2011
19:11
Unknown
ADELINA MAPANGO
5 comments
Ilikuwa dakika,masaa,siku,wiki,mwezi,miezi,mwaka na sasa ni mwaka wa tatu tangu mama yangu mpendwa Adelina Mapango alipotuacha na majonzi ambayo kamwe hayatafutika.
Mara ya mwisho kuonana na mama akiwa hai ni mwaka 2005 nilipokwenda nyumbani kwa ajili ya fieldwork yangu.Novemba mwaka huo,ndoa ya Baba Mzee Philemon Chahali na Mama ilitimiza miaka 50,yaani nusu karne.Niliwarekodi kwenye video na kila ninapojaribu kuangalia mkanda huo naishia kububujikwa na machozi.Bila kujua kuwa ananiachia wosia,mama alisisitiza sana kuhusu upendo.Aliniambia kuwa nikiwa mcha Mungu nitaweza kuwapenda watu wote.Alinisisitiza kumtanguliza Mungu katika kila nifanyalo.Alininiambia pia kuwa zawadi kubwa nitakayoweza kumpa yeye na mumewe ni kufanikiwa katika masomo na maisha yangu kwa ujumla,kuwatunza wazazi na ndugu zangu,kwathamini marafiki na jamaa zangu,kuheshimu kazi na pindi nikioa,nimpe upendo mke wangu na watoto kama ambavyo yeye na baba walivyonipenda.
Mama alikuwa na upendo usioelezeka.Nakumbuka nikiwa mdogo huko Kigoma timu ya Pan Africa ilifanya ziara huko.Wakati huo,binamu yangu Gordian Mapango alikuwa bado anacheza mpira (kama winga machachari wa Pan Africa).Basi Gordian alikuja kututembelea nyumbani akiwa na rafiki zake marehemu Ibrahimu Kiswabi na mchezaji mwingine jina limenitoka.Walipoingia tu ndani mama akakaa chini na kumpakata Gordian kama mwanae mchanga vile.Japo nilikuwa mdogo lakini bado nakumbuka jinsi marehemu Kiswabi na yule mchzaji mwingine walivyoguswa na upendo wa mama kwa mtoto wa kaka yake (Gordian).
Kwa vile mwaka 2005 nilikaa Tanzania kwa takriban miezi sita hivi,nilikuwa nikienda nyumbani Ifakara mara kwa mara,kila nilipopata fursa nje ya fieldwork yangu.Kila nilipokuwa hapo nyumbani mama alisisitiza kunichemshia maji ya kuoga,kunifulia na kunitunza kama mtoto mchanga.Mama,upendo ulionipa nitaendelea kuukumbuka hadi naungana nawe huko uliko.
Nilimeshahudhuria misiba mbalimbali lakini kufiwa na mzazi ni kitu kisichoelezeka.Nakumbuka nilikuwa Kinondoni Mtaa wa Isisi pamoja na binamu yangu Gordian na marafiki wengine,na majira ya saa 4.30 usiku nikapigiwa simu kutoka Ifakara (maana wakati huo nilikuwa Dar kwa muda).Ile kupokea tu nikamsikia sista (wa kanisani) aliyekuwa mmoja ya masista waliokuwa wanamsaidia sista mwenzao (mdogo wangu) Sr Maria-Solana kumuuguza mama.Huku akilia,sista huyo akaniambia "Kaka Evarist,mama hatunaye".Nikamuuliza "unamaanisha nini?"Akaendela kusema "mama hatunaye,ametutoka".Nikawa kama nimepigwa ganzi vile.Yani ilinichukua kama nusu saa hivi,baada ya kuondoka Kinondoni na kurejea Sinza (nilipokuwa nimefikia)
kupata fahamu kuwa hatimaye mama yangu mpendwa Adelina Mapango amefariki.
kupata fahamu kuwa hatimaye mama yangu mpendwa Adelina Mapango amefariki.
Niliongea na mama mara ya mwisho mwezi Februari 2008.Nilipiga simu nilipopata taarifa kuwa mama mkubwa (dada yake mama) alikuwa amefariki.Japo hali ya mama wakati huo haikuwa nzuri sana,alisistiza kuwa lazima aende kumzika dada yake.Nikamsihi mama kuwa kwa hali aliyonayo,na kwa jinsi alivyompenda dada yake,ni vema asiende msibani.Kumbe siku hiyo ndio nilikuwa naongea nae kwa mara ya mwisho.Siku chache baadaye akapata stroke na akapoteza fahamu.Wiki chache baadaye nikaenda Tanzania kumuuguza lakini kwa bahati mbaya hadi anafariki hakuweza kufumbua mdomo kuongea nami.
Kinachonitia uchungu hadi leo ni ukweli kwamba siku nilipomtembelea hospitalini Muhimbili baada ya kufika Dar alitoa kama tabasamu hivi.Hata baadhi ya manesi na ndugu waliokuwa wanamuuguza wakasema inaelekea mama amefurahi mwanae nimekwenda kumuuguza.Niliendelea kuwa na matumaini kuwa ipo siku atapata fahamu na hatimaye kurejea kwenye hali yake ya kawaida.Kwa bahati mbaya haikutokea hivyo hadi anafariki.
Kwa kweli bado nina uchungu mkubwa sana.Kuzidisha machungu hayo ni ndoto za mara kwa mara ambapo mama namuona mama.Pengine ni kwa vile namuwaza sana,au pengine ni kwa vile alifariki bila kuniambia chochote.Majonzi niliyonayo moyoni hayaelezeki.
Kuna tatizo jingine.Wakati mama anafariki,baba alikuwa amemzidi kama miaka 10 hivi.Ikumbukwe pia kuwa walikuwa kwenye ndoa kwa miaka 53 wakati mama anafariki.Sasa baba hadi leo hii anaendelea kuona kama yeye ndiye alistahili kutangulia kabla ya mkewe kwa vile alikuwa amemzidi umri.Baba na marehemu mama walikuwa zaidi ya mke na mume.Walikuwa best friends.Baba yangu si mzungumzaji sana,na muda mwingi aliutumia nyumbani na mkewe.Kifo cha mama kinamtesa sana baba na kila ninapoongea nae anakumbushia uchungu alionao.
Kuna tatizo jingine pia.Wadogo zangu wa mwisho ni mapacha.Baba na mama walijaliwa kuwapata mapacha hawa wakati umri umeshawatupa mkono.Kwahiyo,Kulwa na Doto wamekuwa kama wajukuu kwa baba na mama.Kwa wadogo zangu hawa,mama alikuwa ni za zaidi ya mzazi wao.Alikuwa ni mwalimu wao (akiwafundisha kupika,sala,nk),alikuwa kama bibi yao (walikuwa wanapenda sana kumtania na yeye alipenda kuwatania pia),alikuwa ni rafiki yao mkubwa kwa vile madogo hao walikuwa wanamwongopa baba,kwahiyo siri zao,habari zao na kila kitu chao walikuwa wanashea na marehemu mama.Kwa ndugu zangu hawa,kifo cha mama ni pigo kubwa sana sana.
Naweza kuandika kitabu kizima kuelezea tukio hili la kusikitisha kupita kiasi.Lakini yote ni mipango ya Mungu.Nakumbuka katika misa ya kabla ya mazishi ya mama,padre alijaribu kutuliwaza kwa kutuambia kwamba "sote tulimpenda Adelina lakini Baba yake aliyepo Mbinguni amemependa zaidi na hivyo ameamua kumchukua mwanae".
Basi,mama mpendwa,leo tunaadhimisha mwaka wa tatu tangu utuache.Pengo lako haliwezi kuzibika.Tunakukumbuka kila siku.Upendo wako,tabasamu lako la muda wote na huruma uliyokuwa nayo ni vitu tunavyoendela kuvienzi.Mafundisho uliyotupa ndio mwongozo wetu wa kila siku.
PUMZIKO LA MILELE AKUPE BWANA NA MWANGA WA MILELE AKUANGAZIE,UPUMZIKE KWA AMANI.AMINA
Thursday, 26 May 2011
Mrs Agnes Atim Apea - Motivation Speaker, PhD Student, Gender and HIV, Reading University; Dr. Bunmi Arogunmat - Motivation Speaker; Terrence Higgins Trust;Mama Balozi, Tanzania; Mama Waziri Mkuu, Tanzania; Dr. Sylvia Anie, Director, Social Transformation Programmes Division, Commonwealth Secretariat, Sponsors of the prommmae and Mama Balozi, Kenya.
MAMA BALOZI JOYCE KALLAGHE AKIKARIBISHA WAKINA MAMA
MARIAM MUNGULA NA MAMA PINDA
MJUMBE WA NEC ASHA BARAKA AKIWA NA JESTINA GEORGE
/MKE WA BALOZI WA KENYA AKISALIMIA WAKINA MAMA
MKE WA WAZIRI MKUU MAMA TUNU PINDA AKIONGEA NA WAKINA MAMA
WAKINA MAMA KATIKA POSE NA MGENI RASMI
WAKINA MAMA KATIKA PICHA YA PAMOJA
TA-UK ikishirikiana na TAWA waliandaa semina ya akina mama iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Tanzania Uingereza, Jumamosi, 21 Mei 2011.Mgeni Rasmi alikuwa Mama Pinda Mke wa Waziri Mkuu, Tanzania.
Mada ya Semina ilikuwa “Wanawake kama Wakala wa Mabadiliko” na mkazo zaidi kwenye - Mwamsho kuhusu Waafrika waishio Uingereza wanaoishi au walio adhirika na UKIMWI” “HIV and AIDS Awareness Seminar: for African communities affected by HIV and AIDS in the United Kingdom.
Kusudu na Mategemeo ya Semina:
Makusudi ya semina yalikuwa: kuwakumbusha/mwamko kuhusu Ukimwi, kuzungumzia maswala ya stigma, ubaguzi, watu kutokukubali (denial), kukubali na kuweza kujitokeza. Inategemewa hatimaye kuweza kuwa na vikundi vya kusaidiana baini ya Waafrika hususani Watanzania waishio Uingereza.
Objectives:
The seminar aims to: Raise HIV and AIDS awareness, discuss issues of stigma, discrimination, denial, acceptance and disclosure of HIV status, training needs, develop support and social network groups among the African communities living in the UK.
Semina ilikuwa katika sehemu mbili:
Sehemu ya kwanza ilikuwa kwa Kiingereza na wazungumzaji wakuu walitoa changamoto kuhusu:
Akina Mama kama Wakili wa Mabaliko:
- Akina mama walikumbushwa kwamba afya ni jambo la mhimu kwa kila mtu. Maendeleo au mabadiliko yeyote yale yana leletwa na watu wenye afya nzuri. Kwa hiyo ni vema mama kujali afya yako ikiwa ni pamoja na kuungalia mwili wako kama vile kwenda hospital na kupimwa kwa magonjwa mbali mbali, kubadilisha mwenendo wako. Mama akiweza kujali na kubadilisha mwenendo wake yeye atakua mfano na kuwa taa kwa watu waliokaribu naye – familia pamoja na jamii kwa ujumla.
- Kuishi kwa mategemeo –“Living positively with HIV” – Hii ilikuwa changamoto sana kwa wajumbe, watu walielezwa kuwa ukiwa na UKIMWI siyo mwisho wa maisha. Mtoa mada kwanza aliuza swali hivi nani anaweza kumtumbua mtu aliyeaidhirika kwa Ukimwi yuko vipi au unaweza kumtambua vipi? Jibu hakuna mtu ambaye anaweza kutambua labda mtu akiwa mahututi kitandani. Jibu ni kwamba mtu ye yote Yule anaweza kuwa ana Ukimwi lakini hakuna anayejua. Mtoa mada alisema kuwa yeye ameadhirika tangu akiwa mdogo lakini sasa hivi ameolewa na ana watoto. Amesoma na anafanya PhD na anaishi maisha ya furaha kama watu wote. Fundisho jamani ukiwa na UKIMWI siyo mwisho wa maisha. Lakini unaweza kufanikiwa kuishi haya maisha kama utapimwa na ikajulikana mapema kuwa umeadhirika ili ukapata msaada.
Sehemu ya pili:
Mama Balozi alimkaribisha Mama Waziri Mkuu. Mama Pinda alisema kuwa amefurahishwa sana na kitendo cha akina mama kukutana na kuwa na semina nzuri sana iliyoelimisha, kufumbua watu kuelewa mambo zaidi. Vile vile alimshukuru Mama Balozi kwa kuweza kuwakaribisha wanawake nyumbani kwake.Aliahidi kuwa endapo atapata nafasi ya kuja Uingereza tena atajihidi kukutana na akina mama. Semina za uamusho kwa
Vile vile wakati huu wajumbe walipata nafasi ya kupata changamoto nyingine toka kwa mtu ambaye vile vile amejitokeza kuwa yeye ameadhiriwa na Ukimwi, alisema siyo jambo rahisi kujitokeza kwani kuna mambo mengi sana kama vile– dharau, kukataliwa na ndugu, kuogopa kuondolewa etc. Alisema ameweza kufika hapa kwa sababu alitambua mapema kuwa ameadhiriwa. Kwa hiyo changomoto ilikuwa jamani tujitahidi kupimwa mara kwa mara.
Kusudu na Mategemeo ya Semina
Makusudu ya semina yalikuwa: kuwakumbusha/mwamko kuhusu Ukumwi, na kuzungumzia maswala ya stigma, ubaguzi, watu kutokukubali (denial), kukubali na kuweza kujitokeza na na hatimaye kuweza kuwa na vikundi vya kusaidiana baini ya Waafrika hususani Watanzania waishio Uingereza.TA-UK itaendelea kuandaaa hizi semina kwa kushirikiano na vikundi mbali mbali vya Kitanzania, Africa Mashariki vilivyopo nchini Uingereza. Hizi Semina zinadhaminiwa na msaada kutoka Commonwealth Secretariat
CHANZO: Miss Jestina
CHANZO: Miss Jestina
Sio siri kwamba Jeshi la Polisi Tanzania lina sifa chafu na yayumkinika kuamini kuwa ni taasisi inayochukiwa sana na walalahoi.Sifa kuu mbili za jeshi hili linaloongozwa na IGP Saidi Mwema ni RUSHWA ILIYOKUBUHU na UBABE WA KUPINDUKIA.
Sifa hizo zinahusiana kwa karibu.Rushwa ya polisi inachangiwa zaidi na kipato duni kisichoendana na wajibu wao (ambao kwa asilimia kubwa hawautekelezi).Kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili,ambao tegemeo kubwa la kuutatua ni kwa kulazimisha rushwa (wakinyimwa hawakawii kumbambikia mtu kesi),askari wa jeshi la polisi wanakuwa na hasira muda wote.Lakini badala ya kuelekeza hasira hizo kwa mwajiri wao-yaani serikali-wao wanaelekeza hasira hizo kwa wananchi wanyonge wasio na watetezi (sambamba na wanasiasa wa vyama vya upinzani hususan Chadema).
Kingine kinacholifanya jeshi la polisi lifanane na Nazi Police wa Hitler ni uhaba wa elimu.Polisi limekuwa kimbilio la vilaza (watu wenye uwezo duni kimasomo) na kwa upande mwingine jeshi hilo limegeuzwa mahala pa vigogo kupeleka watoto wao watukutu.Kimsingi,jeshi hili halina nidhamu isipokuwa kwa vigogo na mafisadi wanaowatunza.
Inafahamika kuwa Rais Jakaya Kikwete na IGP Said Mwema wana mahusiano ya kibinafsi zaid ya hayo ya kiserikali.Na hili ndio tatizo la kuendesha nchi kiushkaji.Kinachompa jeuri kubwa IGP Mwema ni ukweli kwamba moja ya sababu zilizopelekea kupewa wadhifa huo ni ukaribu wake na Kikwete.Kwa maana hiyo anajua wazi kuwa Kikwete hawezi kumtosa hasa kwa vile uteuzi huo ni wa misingi ya nilinde nikulinde.
Lakini Kikwete akae akitambua kuwa moja ya sababu zilizopeleka dikteta Hosni Mubarak kung'olewa madarakani huko Misri ni unyama wa jeshi lake la polisi.Jeshi hilo ndilo lililopelekea vifo vingi wakati wa maandamano ya kudai mageuzi nchini humo.Kama wenzao wa Tanzania,polisi wa Mubarak walikuwa wanafahamu lugha moja tu:UBABE.
Kikwete atambue kuwa kuwaachia wahuni waliovaa yunifomu za polisi wanyanyase wananchi wapendavyo,waue wanachi kila wanapojiskia na waendelee kuwabambikia kesi walalahoi,siku ya siku wananchi hao wataamua liwalo na liwe.Ubabe sio ufumbuzi wa kila kitu.Kulikuwa na tawala ngapi za kibabe zilizoishia kuwa historia?
Kikwete na serikali yake ya CCM hawawezi kukemea uhuni na ukatili wa polisi kwa vile jeshi hilo,kama zilivyo taasisi nyingine za dola,limeendelea kuwa tawi lislo rasmi la chama tawala.Laiti Kikwete angekuwa anathamini haki za binadamu asingeruhusu jeshi hilo litangulize nguvu hata pale panapohitaji diplomasia.Kwanini awakemee ilhali wanawakomoa Chadema na walalahoi wengine?Unadhani Kikwete asingechukua hatua laiti polisi wangelalamikiwa na mafisadi?
Enewei,soma habari zifuatazo zinazohusu jeshi hilo la polisi
Polisi wapambana na raia DarWednesday, 25 May 2011 21:56Felix Mwagara na Ellen ManyanguVURUGU kubwa zilizuka usiku wa kuamkia jana katika eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, baada ya maofisa wa Manispaa ya Temeke kuendesha operesheni ya kubomoa vibanda vya wafanyabiashara wadogo kwenye hifadhi ya barabara.Ilibidi polisi kuingilia kati kuwatawanya wafanyabiashara hao waliokuwa na hasira, wakipinga uharibifu wa mali zao wakidai kuwa mkakati huo umetekelezwa bila wahusika kupewa taarifa.Zaidi ya mabanda 50 ya wafanyabiashara hao yalibololewa katika agizo hilo kwenye eneo lililopo karibu na Feri, ambalo mji wa Kigamboni unakua kwa kasi.Baadhi ya walioshuhudia vurugu ambazo ziliandamana na vitendo vya uporaji wa mali na fedha, walisema wafanyabiashara wapatao 50, walikamatwa. Hadi jana mchana, kulikuwa na idadi kubwa ya polisi kwenye eneo hilo wakiwazuia wafanyabiashara hao wasifanye fujo huku maofisa wa manispaa wakibeba bidhaa mbalimbali zilizozagaa hapo.Wafanyabiashara hao walisema kwamba walilazimika kupambana na askari hao ili kunusuru mali zao katika mpango huo uliotekelezwa bila notisi."Ilitulazimu kupambana ili kuokoa japo mali kidogo kwani ubomoaji huo umefanyika usiku wa manane pasipo taarifa yoyote. Hatujapewa notisi yoyote ya kuhama katika eneo hili," alisema Rajabu Mohamed.Mwenyekiti wa wafanyabiashara katika eneo hilo, Omary Mkwesu alisema tukio hilo ni la kusikitisha kwa sababu wamepoteza mali nyingi.Alihoji kuwa kama ubomoaji huo ulikua wa haki kwa nini wasingewapa notisi ili walau watoe mali zao katika mabanda hayo?Alidai kwamba hatua hiyo ni njama za diwani wa eneo hilo: "Zoezi hili limesimamiwa na diwani wetu ambaye amekuwa akitutishia kwa muda mrefu kuwa ipo siku atatubomolea na kwa kuthibitisha hilo, tumemuona akisimamia zoezi hili la ibomoaji hovyo saa nane usiku."Hata hivyo, Diwani wa eneo hilo, Dotto Msama alikanusha kuhusika na tukio hilo akisema Manispaa ya Temeke ilishatoa notisi zaidi ya sita kuwataka wafanyabiashara hao waondoke katika eneo hilo."Jambo hili limenisikitisha hata mimi na sasa hivi naelekea manispaa kuongea na uongozi wake juu ya tukio hili. Ni kweli sikuwa na taarifa za zoezi hili kufanywa leo, tena usiku wa manane, ila notisi zilishatolewa na nakala yake iko kwa mtendaji na mwanasheria wa manispaa.Polisi kwa upande wake, wamekanusha kuwanyanyasa wananchi hao na kusema walikuwepo kwa ajili ya kulinda usalama hasa baada ya wananchi hao kufunga barabara.
CHANZO: Mwananchi
Na habari ifuatayo ni kuhusu moja ya SIFA KUU MBILI za Jeshi la Polisi,yani RUSHWA (nyingine ni UKATILI)
CHANZO: MwananchiPolisi, mahakama zazidi kutajwa kwa rushwaWednesday, 25 May 2011 21:54Minael MsuyaIDARA za POLISI na Mahakama zimetajwa tena kuwa ni taasisi sugu zinazoongoza kwa kudai rushwa nchini.Kituo cha Sheria na Haki za binadamu (LHCR) katika taarifa yake imezitaja idara hizo kwamba ndizo kinara kwa kudai rushwa.Hivi karibuni, Taasisi ya Kupambana na kuzuia Rushwa Takukuru) nayo ilizitaja idara hizo kwamba ndizo zilizo mstari wa mbele kudai rushwa nchini.Ripoti ya mwaka 2010 ya LHCR iliyofanywa katika mikoa 26 nchini na kuhoji watu zaidi ya 5,000, ilibainisha kuwa polisi inaongoza kwa asilimia 65.1 huku Mahakama ikifuatia ikiwa na asilimia 56.4. Akisoma ripoti hiyo, Mwanasheria wa LHCR, Pasience Mlowe alisema polisi na mahakama zinaongoza kwa rushwa na matumizi mabaya ya ofisi na kwamba zinashika nafasi ya 10 kwa Afrika Mashariki.“Utafiti wa LHCR ulibaini kuwa polisi na mahakama ni taasisi sugu zinazoongoza kwa rushwa na zinashika nafasi ya 10 kwa Afrika Mashariki,” alisema Mlowe.Alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) nayo inafuatia kwa asilimia 37.8 na kwamba inaendelea kushuka kiwango kila siku ikilinganishwa na 2009 ambapo ilikuwa katika nafasi ya tano. “Hali hii inayonyesha ni jinsi gani baadhi ya watu walivyozitelekeza sheria na haki za binadamu, wananchi wengi wanataabika usiku na mchana, lakini hawapati haki zao stahiki, tunaomba marekebisho ya vifungu vya sheria yafanyiwe kazi ili haki ya binadamu iweze kupatikana,”alisema.Mlowe alisema, matatizo hayo ya taasisi hizo nyeti za serikali yanachangia kwa kiasi kikubwa kuzorotesha uchumi wa nchi na kwamba serikali inatakiwa kusimamia sheria muhimu. Kwa upande wake ,Mtafiti na Mwanasheria wa LHCR, Onesmo Olengurumwa alieleza kuwa, utafiti huo ulibaini kuwa mauaji ya raia wengi yanasababishwa na vyombo vya dola kutokana na wao kujichukulia sheria mikononi.“Vifo vya watu 52 vilivyotokea mwaka 2010 vilisababishwa na walinzi wa kampuni mbalimbali na polisi kwa kujichukulia sheria mikononi badala ya kutumia sheria inayowaongoza,”alisema Olengurumwa na kuongeza: ”Mfano mzuri ni wananchi wanaoishi kando ya Mgodi wa North Mara kule Tarime wanauawa bila sababu na ukichunguza utakuta sheria za mgodi, walinzi wa kampuni ndio wanaopaswa kulinda eneo lote sasa serikali inaingiliaje huko,”alisema.Alisema mauaji ya watu yaliyotokana na mgodi huo, serikali haiwezi kujitetea kwa lolote na kwamba utetezi wake ni wakisiasa. Alisema serikali ikisimamia tume ya sheria na haki za binadamu nchi itaweza kuondokana na changamoto za ukiukwaji wa haki hizo zinazoikabili.
Wednesday, 25 May 2011
Hatimaye tovuti hii imeamua kushiriki kuwania tuzo za blogu za Kitanzania zijulikanazo kama TANZANIAN BLOGS AWARDS.
Blogu hii inawania tuzo kwenye kundi la BLOGU BORA YA SIASA au kwa kimombo BEST POLITICAL BLOG.
Cha kufanya,nenda kwenye link hii http://www.tanzanianblogawards.com/2011/04/faqs.html
Kisha jaza kama ifuatavyo (nimeweka picha za vipengele vilivyopo kwenye fomu ya kuchagulia blogu uipendayo
Hapa wanahitaji jina la mwandishi wa blogu.Kwahiyo kama unaona Kulikoni Ughaibuni inastahili basi jina linalotakiwa hapa chini ni EVARIST CHAHALI
Hapa chini wanahitaji jina la makazi.Makazi yangu ni GLASGOW, SCOTLAND
Hapa chini wanahitaji jina la blogu.Kama ujuavyo,blogu hii inaitwa KULIKONI UGHAIBUNI
Hapa wanakupa fursa ya kuchagua ni kundi gani unadhani blogu uipendayo inastahili tuzo.Tovuti hii inaomba kura yako katika kundi la blogu za siasa,yaani hapo chini walipoandika BEST POLITICAL BLOG.Weka tiki hapo kwenye kipengele cha 19
Hapa wanauliza kama blogu uliyoipigia kura ina "mambo ya kiutu uzima/ngono".Na kama unavyofahamu,huo ni mwiko kwa tovuti hii.Kwahiyo,kama unaona tovuti hii inastahili tuzo,tiki hapo kwenye NO
Malizia kwa kubonyeza kitufe kilichoandikwa SUBMIT
NATANGULIZA SHUKRANI ZANGU ZA DHATI
Tuesday, 24 May 2011
Askari wa Kikosi cha Kuzuwia Ghasia (FFU) wakiwa tayari kuvunja haki za binadamu nchini Tanzania.Picha hii haihusiani na habari ifuatayo. |
Tanzania yetu inaelekea wapi?Tangu lini kupiga picha jeneza imekuwa kosa linalopelekea polisi kukamata waandishi wa habari waliopiga picha majeneza?
Kwa kweli Jeshi la Polisi linafanya kila jitihada kuhakikisha amani na utulivu vinaondoka nchini.Jeshi hilo limekuwa likiendeshwa kibabe pasipo kujali haki za binadamu.Inachukiza kuona polisi wanakurupuka kumkamata mtu yeyote yule wanapojisikia lakini wanakuwa wagumu kuchukua hatua dhidi ya wabaka uchumi wanaotenda uhalifumkubwa kwa taifa kuliko raia wema hao wasio na hatia.
Kadhalika,jeshi hilo limekuwa halina heshima yoyote kwa wanasiasa na wanachama wa vyama vya upinzani ambapo polisi wanawakamata ovyo ovyo.Wito wa tovuti hii ni kwa wanaokamatwa kufungua kesi za madai wanapoachiwa bila kufunguliwa mashtaka.Tkuwaacha wahuni hawa waliokabidhiwa jukumu la usalama kwa raia lakini badala yake wanapelekea adha kwa raia wasio na hatia tutaishia kujilaumu huko mbeleni.Violence begets violence,wananchi watafika mahala wakaamua liwalo na liwe na hao polisi waonevu hawatakuwa salama.
Ubabe sio ufumbuzi wa matatizo kwani kama tumeshuhudia tawala kadhaa za kibabe zikiondoka madarakani pale wananchi wanapoamua kuwa imetosha,enough is enough.Soma habari ifuatayo na utaelewa ninacholalamikia hapa
Polisi wadaiwa kupora maiti TarimeTuesday, 24 May 2011 22:44WADAIWA KUVAMIA MOCHWARI USIKU,WABUNGE CHADEMA WATUPWA RUMANDEWaandishi WetuPOLISI Kanda Maalumu ya Tarime, wanadaiwa kuvamia chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime, Mara kuchukua maiti za watu wanne waliouawa katika tukio la uvamizi wa Mgodi wa Nyamongo na kuziweka chini ya ulinzi.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa tukio hilo lilikwenda sambamba na kukamatwa kwa watu 12 wakiwemo wabunge wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).Waliokamatwa katika tukio hilo ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Viti Maalumu, Ester Matiko. Wengine ni kada wa Chadema, Waitara Mwita na wakazi wengine sita wa Tarime ambao majina yao hayakupatikana mara moja.Chanzo kimoja cha habari kilisema jana kwamba watu hao walikamatwa majira ya saa 3:23 juzi usiku baada ya polisi kupiga mabomu ya machozi eneo la chumba cha kuhifadhia maiti kuwatawanya watu waliojitokeza kuzuia polisi kuchukua miili ya marehemu usiku huo.Taarifa zilisema kuwa mbali na watu hao kukamatwa juzi, jana majira ya saa 4:30 asubuhi waandishi wa habari watatu; Anthony Mayunga (Mwananchi), Beldina Nyakeke (The Citizen) na Anna Mroso (Nipashe), walikamatwa.Waandishi hao walikamatwa jana na mbunge huyo wa viti maalumu wa Chadema katika Kijiji cha Nyakunguru na kuhojiwa kwa muda katika Kituo cha Polisi Nyamwaga kabla ya kupelekwa kwa Kamanda wa Operesheni Maalumu, Paul Chagonja. Waliachiwa kwa kujidhamini wenyewe saa 9:30 jioni.Hata hivyo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema alipotafutwa kuzungumzia suala hilo simu yake ya mkononi ilipokewa na msaidizi wake ambaye alisema anayeweza kulitolea ufafanuzi ni msemaji wa jeshi hilo, Advera Senso.Senso alipotafutwa naye alisema hawezi kulizungumzia akimtupia mpira Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Tarime, Constantine Massawe.Hata hivyo, Massawe alikanusha madai hayo ya kupora maiti akisema kwamba walipata taarifa kutoka kwa ndugu wa marehemu kwamba kuna baadhi ya watu waliokuwa wakiwazuia kuchukua miili ya ndugu zao."Jana baada ya kufanyika uchunguzi kama walivyotaka, miili yote ilikuwa chini ya familia. Sasa uamuzi wa kuzika ulikuwa juu yao, lakini majira ya saa mbili usiku tulipata taarifa kuwa kuna watu wako mochwari wamezuia ndugu wanaotaka kuzika wasichukue miili ya jamaa zao," alisema Kamanda Massawe na kuongeza:"Tulipofika tulikuta wapo watu wanane, wanne walikuwa ni wakazi wa Singida na wengine wanne wakiwa ni wakazi wa Tarime. Tuliwakamata na kusimamia ulinzi wa ndugu waliotaka kuchukua miili ya jamaa zao wakachukua."Alisema baada ya miili hiyo kuchukuliwa, polisi ililitoa msaada wa kuwasafirishia ndugu hao hadi majumbani kwao na walikuwa wanaishusha kadri walivyokuwa wameambiwa na ndugu hao.‘Sasa asubuhi hii (jana), tumeelezwa kuwa kuna kundi la watu wengine lilikuwa likipita nyumba hadi nyumba kuwahamasisha wafiwa kutokubali kuzika maiti za ndugu zao baada ya kufuatilia tuliwakamata na hawa waandishi wakiwa wanapiga picha jeneza," alisema Kamanda Massawe.Awali, Katibu wa Chadema Tarime Mjini, Paschal Warioba alidai kuwa polisi walipora maiti hizo na kwamba viongozi wa chama chake walikamatwa juzi usiku majira ya saa nne."Lissu yuko 'lockup' (rumande) hapa Nyamongo, walikuwa wakifuatilia maiti za watu waliouawa katika vurugu mgodini ili leo (jana) ziende kuzikwa, lakini kabla ya kufanikisha zoezi hilo jana (juzi), polisi walizipora maiti hizo kwa kuwadanganya baadhi ya ndugu kwa kuwapa fedha ili waende kuzizika," alisema.Warioba alidai kuwa baadhi ya maiti tayari wamezikwa, lakini wengine wameonekana katika maeneo karibu na walipokuwa wakiishi.Juzi alasiri, maiti hao walifanyiwa uchunguzi wa mwisho tayari kwa ajili ya maandalizi ya mazishi yaliyokuwa yamepangwa kufanyika jana chini ya uratibu wa Chadema kabla ya vurugu kubwa kuibuka katika chumba cha maiti baada ya polisi kufika na kukuta umati wa watu uliokuwa tayari umekusanyika kuanzia saa 1:30 jioni ili kuchukua miili hiyo kwa ajili ya mazishi yaliyokuwa yamepangwa kufanyika leo.Hata hivyo, Chadema kinadai kwamba baadhi ya ndugu wa wafiwa waliona maofisa wa polisi wakinunua majeneza manne na kuyapakia katika gari lao kabla ya kufika hospitali hapo kuchukua miili hiyo.Kutokana na taarifa hiyo, Lissu, Waitara na makada wengine wa Chadema wakiwa na wananchi wengine waliamua kufika katika eneo la mochwari na muda mfupi baadaye, idadi ya watu iliongezeka kwa lengo la kuzuia Polisi kubeba miili hiyo."Wakati tukio hilo hapo mochwari polisi walifika majira ya saa mbili usiku na kukuta timu kubwa ya watu ambao walikuwa wamejitolea kulinda maiti hao wasichukuliwe," alisema mkazi wa Tarime aliyejitambilisha kwa jina la Mwita Nyankaira na kuongeza:"Walianza (polisi) kupiga mabomu ya machozi kuwatawanya watu na ndipo walipowakamata kina Lissu na wengine. Sisi tulifanikiwa kukimbia."Alisema baada ya polisi kuwasambaratisha wananchi, walirudi hospitalini hapo na kuchukua maiti hao na kuanza kuwapeleka usiku huohuo kwenye familia za wafiwa.Habari zimeeleza maiti ya Chawali Bhoke ilipelekwa katika Kijiji cha Bonchugu, wilayani Serengeti na Mwenyekiti wa kijiji hicho, Mwikwabe Makena alisema kulikuwa na vurugu kubwa jana asubuhi kijijini hapo baada ya polisi kuwalazimisha ndugu kupokea mwili huo kwa ajili ya kuuzika."Kumekuwa na vurugu kubwa iliyoambatana na polisi kurusha mabomu ya machozi," alisema mwenyekiti huyo.Maiti nyingine ilipelekwa katika Kijiji cha Nyakunguru, Kata ya Kibasuka. Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nyamanche kilichoko kwenye kijiji hicho, Isaack Marara alisema jana saa 12:00 asubuhi, alifuatwa na mkazi wa eneo hilo, Kisabo Ghati na kumweleza kuwa kuna jeneza limewekwa barabarani lakini hawajui kuna nini ndani yake."Watu walishtuka sana kwani hawajawahi kuona tukio hilo. Baba mdogo wa marehemu Emmanuel Magige, Ambrose Nyabwanya alidai kuwa saa 6:00 usiku wa juzi, magari mawili ya polisi yalisimama na kushusha jeneza mita 200 kutoka nyumbani kwao kisha magari hayo yakaondoa haraka.”Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, Mwanasheria na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mabere Marando alisema kitendo cha polisi kuchukua kinguvu miili ya watu hao wanne kwa lengo la kwenda kuizika ni kinyume na walivyokubaliana.Marando alisema walikubaliana na polisi pamoja na ndugu wa marehemu Jumapili iliyopita kwamba shughuli za mazishi zifanyike leo katika Uwanja wa Sabasaba.“Chadema siyo kama tumeshikilia kidedea msiba huu. Tunafanya hivi kwa kuwa waliouawa ni makada wa Chadema na hiyo ndiyo siasa."Ripoti ya uchunguzi wa miili yawekwa hadharaniUchunguzi wa miili ya maiti wanne waliopigwa risasi na askari polisi katika Mgodi wa African Barrick North Mara uliofanywa na daktari bingwa kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Makatta imebaini kuwa marehemu wote walipigwa risasi maeneo ambayo hayakulenga kujeruhi, bali kuua.Uchunguzi huo uliochukua saa 4:27 ulianza saa 5.20 asubuhi hadi saa 9.47 alasiri. Upande wa familia za wafiwa ulisimamiwa na Dk Greyson Nyakarungu kutoka Hospitali ya Wilaya ya Tarime na askari wawili. Taarifa hiyo itakabidhiwa kwa hospitaliDk Nyakarungu alisema Emmanuel Magige mwenye jalada la uchunguzi wa kidaktari namba za PM1/5/2011 (TGH), alipigwa risasi katika nyonga ya kushoto ambako kulikuwa na tundu la duara llilokuwa na upana wa sentimita 0.5 ilipoingilia na sentimita 2.5 ilipotokea.“Mishipa ya damu iliharibiwa, kibofu cha mkojo, mishipa ya fahamu, mfupa wa nyonga ulisagika, damu ikavia ndani ya tumbo, lakini chini ya mgongo karibu na risasi ilipotokea kulikuwa na tundu linaloonyesha kuwa alichomwa na kitu chenye ncha kali kama singa ya bunduki,” alisema na kuongeza:“Tumebishana sana kwa hilo wenzangu wakidai huenda aliangukia kitu kikamchoma, ikumbukwe kuwa alipigwa kwa nyuma akikimbia hivyo asingeweza kuanguka chali zaidi ya kifudifudi,” alisema.Kuhusu Chacha Ngoka mwenye jalada la uchunguzi wa kidaktari PM 2/5/11 (TGH), uchunguzi ulibaini kuwa alipigwa risasi mgongoni karibu na kiuno na kutokea katikati ya mbavu chini ya titi, tundu la kuingilia likiwa ni sentimita za duara 0.3 na ukubwa wa tundu pa kutokea ikiwa ni sentimita tano.Mishipa mikubwa ya damu iliharibiwa, ini likasagwasagwa, damu iligandia kwenye mfumo wa upumuaji hali ambayo inadhihirisha kuwa alipumua kwa nguvu, damu ilikwisha mwilini na kuwa alipigiwa risasi kwa mbali.Alisema marehemu Bhoke mwenye jalada la uchunguzi wa kidaktari PM/3/5/11(TGH) alipigwa risasi ya kichwani karibu na sikio na kidonda chake pakuingilia ni sentimita za duara 0.2 ,pa kutokea sentimita tano za duara kwenye paji la uso hivyo kuharibu ubongo, fuvu na mifupa yote kubomolewa.Kuhusu uchunguzi wa Mwikwabe Marwa Mwita mwenye jalada la uchunguzi wa kidaktari PM/4/11 (TGH) alisema alipigwa risasi karibu na nyonga na kuacha tundu la sentimita za duara 3,5 na risasi haikutoka nje na kuharibu mifupa yote ya nyonga, misuli ikawa imeharibiwa na kipande cha risasi kilikutwa katikati ya misuli (PSOAS), damu ikiwa imevia tumboni.“Kilichoonekana hapo ni kuwa walipigwa risasi kwa mbali tena kwa nyuma maana wote zimeingilia kwa nyuma na maeneo waliyopigwa risasi ni yale ya kuua si kuwapunguza nguvu kama walikuwa wamegoma kusalimu amri,” alisema daktari huyo.Kuzuiwa kwa maziko ya pamojaAwali, Chadema kilipanga kuendesha ibada ya maziko katika Uwanja wa Sabasaba leo kuanzia saa 2:00 asubuhi kabla ya kupelekwa katika vijiji vyao kwa ajili ya mazishi ya kifamilia.Lissu alisema juzi usiku kuwa licha ya kukubaliana na wanafamilia na Kamishina wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja, jeshi la polisi lilibatilisha kibali hicho baadaye."Tumekuwa katika maandalizi ya mazishi hayo tangu jana jioni. Hata hivyo, jioni hii tumeletewa barua ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Tarime kututaarifu kwamba haturuhusiwi tena kuwaaga marehemu wetu kama ilivyokubaliwa jana," alieleza Lissu.Waandishi waeleza walivyokamatwaBaadhi ya waandishi waliokamatwa katika sakata hilo walieleza kuwa walikuwa kazini kutekeleza majukumu yao.Mmoja wa waandishi waliokamatwa, alisema baada ya kusikia taarifa juzi usiku juu ya polisi kupiga mabomu na kuchukua miili ya marehemu aliamua kuingia kazini kufuatilia tukio hilo.“Tulipofika hapo kijijini tulikuta pia kuna mbunge wa viti maalum wa Chadema, sasa wakati tukiwa tunamhoji, polisi wakafika na kutukamata wakieleza kuwa tumekuwa tukichochea ndugu wasizike miili ya marehemu," alisemaAlisema kitendo cha polisi kuwahoji jana kuanzia saa 5:10 asubuhi hadi saa 6:20 mchana kimewafanya washindwe kuwajibika ipasavyo jambo ambalo linapaswa kulaaniwa na wadau wote wa habari.“Tulihojiwa hapa kwa zaidi ya saa moja na ilipofika saa 6:20 mchana walituambia tusubiri maelekezo kutoka kwa kamanda wa polisi…" alisema.Mei 16, mwaka huu polisi wilayani Tarime iliwaua kwa kuwapiga risasi watu wanne kati ya zaidi ya watu 1,000 waliovamia mgodi wa Nyamongo wilayani humo kwa lengo la kupora mchanga wa dhahabu.Tukio hilo lililotokea katika Kijiji cha Matongo, lilizua msuguano baina ya polisi, Chadema na wananchi wa eneo hilo ambao juzi waligoma kuzika miili ya marehemu hao na kukataa rambirambi ya polisi.Habari hii imeandaliwa na Antony Mayunga, Tarime,Frederick Katulanda, Mwanza na Fidelis Butahe Dar
CHANZO: Mwananchi
Monday, 23 May 2011
![]() |
Mwangalie kwanza.Hivi abiria watasafiri kwenye hilo lijinembo lisilo na mvuto?Au anamaanisha wapande kwenye mkono wake alioinua?Hovyoooo!!!! |
Unajua,baadhi ya viongozi nchini Tanzania wanatuona sie kama machizi vile.How come mtu anayeamua kuondoka katika shirika mfu ajigambe kwa kubadilisha nembo?Huu ni uhuni wa hali ya juu.Lakini uhuni huu unasababishwa na anayeteua wahuni wa aina hii,I mean Rais Jakaya Kikwete.
Hivi Kikwete anajisikiaje kumsikia rafiki yake Mattaka akiwatusi Watanzania kwa kujivunia mafanikio ya nembo mpya ilhali ATC haina ndege hata moja inayoruka?Majuzi tu,Kikwete kaendelezakulialia kuhusu wasaidizi wake anaodai ni mzigo-kana kwamba walimshikia mtutu wa bunduki awateue,na wameendelea kumshikia mtutu wa bunduki asiwatimue.Hii misemina elekezi ya kila kukicha inasaidia nini katika mazingira haya ya mchezo wa kuigiza wa kisiasa ambapo watu wanaosifika kwa tabia zao chafu kuliko ufanisi wao wanaruhusiwa kula fedha za walipa kodi,only kuondoka kwa matusi dhidi ya walipa kodi hao hao?
It's sooo disgusting.Enewei,soma kichekesho hiki kinachoudhi
Mattaka ang'oka ATCLMonday, 23 May 2011 21:56Fredy AzzahMKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mattaka ametangaza kustaafu kazi huku akijivunia kubadilisha nembo, ingawa ameliacha likiwa halina hata ndege moja inayoruka.Mattaka aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuwa alistaafu rasmi Mei 11, mwaka huu baada ya kufika umri wa miaka 60 na kwamba alishindwa kulifufua shirika hilo la umma kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo wa menejimenti. Alitaja moja ya sababu hizo kuwa ni mzigo wa madeni.“Naondoka lakini najivunia kuiondoa ATCL chini ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) waliokuwa wameingia ubia, pia najivunia kuleta nembo mpya ambayo inatumika sasa,” alisema Mattaka.Desemba 2002, Shirika la Ndege Tanzania (ATC), lilibinafsishwa kwa kuingia ubia na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) na kubadilisha jina lake kuwa “Air Tanzania Company Limited” (ATCL). “Wanasema najiuzulu.Hii siyo kweli, nastaafu kwa mujibu wa sheria, ingetakiwa nistaafu kuanzia Mei 11, lakini ni barua tu ndiyo ilichelewa kuja, nimeomba kustaafu na nimekubaliwa,” alisema Mattaka. Mattaka alisema tangu kuteuliwa kwake kuliendesha shirika hilo mwaka 2007, walikuwa na nia ya kulifufua lakini sababu zilizokuwa nje ya uwezo wao zilikuwa kikwazo.“Shirika lolote la ndege linahitaji mtaji ili liweze kujiendesha, sisi tumechukua shirika likiwa na mtaji hasi wa Sh43 bilioni na madeni yaliyofikia Sh23 bilioni,” alisema Mattaka.Alisema katika kujitahidi kulifufua shirika hilo, kuanzia mwaka 2007 mpaka mwishoni mwa 2008, walifanya kazi nzuri ikiwa ni pamoja na kununua ndege moja yenye uwezo wa kubeba abiria 50 na kukodi nyingine aina ya Air Bus, shughuli ambayo alisema waliifanya katika mazingira magumu.Alisema baada ya mwaka huo, mafuta ya ndege yalipanda kwa zaidi ya asilimia 50, jambo lililoyafanya mashirika mengi ya ndege yaliyokuwa yakiendeshwa bila ruzuku ya serikali kuanguka.“Mwishoni mwa 2009 ndipo serikali ikaanza kutoa fedha kidogo kidogo ambazo hata hivyo, ilizielekeza kwenye kulipa madeni. Napenda tu kusema kuwa sasa serikali inatakiwa kuwa na shirika lake la ndege,” alisema Mattaka na kuongeza: “Unapokuwa katika shirika la umma ukastaafu bila matatizo ni jambo la kumshukuru Mungu, kwa hiyo kwa sasa napenda tu kumshukuru Mungu kwa kunifikisha hapa.”Amlaumu MkapaAwali, Mattaka alisema katika uongozi wake ndani ya mashirika ya umma, kamwe hatamsahau Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ambaye alimsimamisha alipokuwa Mkurugunzi wa Mfuko wa Jamii wa (PPF) kutokana na kashfa mbalimbali, ikiwamo ya rushwa na ubadhirifu wa fedha.Anasema kitendo cha kusimamishwa kwake ghafla kilimuumiza sana, ingawa anadai kuwa baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Usalama wa Taifa kuchunguza, walibaini kuwa hapakuwa na ukweli wowote wa kashfa zilizomfanya asimamishwe kazi.“Unajua bwana siku zote mti wenye matunda ndiyo hurushiwa mawe, waliona majengo yanaibuka tu, mara PPF House, PPF Tower na kile Kijiji cha PPF kule Arusha, wakasema lazima hizi ni 10 percent.” “Walichunguza wakakuta yote yale hayana ukweli wowote na wakanilipa stahili zangu ambazo ndizo zilinifanya nikae takribani miaka ninne mpaka nilivyokuja tena huku ATCL.”Alisema ameondoka ATCL na kuliacha likiwa halina hata ndege moja inayoruka akidokeza kwamba moja ipo Afrika Kusini ikifanyiwa matengenezo ambayo anasema yamekamilika na kinachosubiriwa ni Serikali kulipa fedha za matengenezo.Alisema ndege nyingine ipo nchini lakini haifanyi kazi kutokana na kuhitaji matengenezo ya lazima. Mattaka alisema, serikali imemteua William Haji, kukaimu nafasi anayoiacha.
CHANZO: Mwananchi
Sunday, 22 May 2011
URBAN PULSE CREATIVE Ilipata fursa ya kufanya mahojiano maalum na MH Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipokuja katika Ziara yake hapa nchini Uingereza siku chache zilizopita. Mahojiano hayo maalum yalilenga zaidi kuelemisha jamii yetu ya kitanzania, vile vile kutoa Msimamo kutoka katika serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusiana na mambo mbalimbali yanayomhusu Mtanzania .
Mahojiano hayo yaligusa maeneo tofauti yakiwepo majukumu pamoja na changamoto anazokumbana nazo Mh waziri mkuu, Suala la katiba, Uchumi, Rushwa na Ufisadi, Miundo Mbinu, Maendeleo, Chakula, Nishati, Jumuiya ya Africa mashariki pamoja na mambo mengine mengi.Mahojiano yalifanywa na Baraka Baraka Kutoka URBAN PULSE CREATIVE MEDIA na yatarushwa hewani mda sio mrefu.
MUNGU IBARIKI AFRICA, MUNGU IBARIKI TANZANIA
Asanteni,
URBAN PULSE CREATIVE MEDIA
Subscribe to:
Posts (Atom)