Tuesday, 11 November 2008


Serikali imewataka wanafunzi wote wa vyuo vya elimu ya juu nchini kuingia madarasani mara moja ifikapo saa moja asubuhi leo. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe alisema sera ya uchangiaji huduma za jamii ikiwamo elimu, halikwepeki katika mazingira haya ya kiuchumi. 

“Sera yoyote ile haiwezi kubadilishwa mara moja bila ya majadiliano ya kina yanahusisha wadau wote,” alisisitiza Profesa Maghembe, katika kujibu madai ya wanafunzi hao wanaopinga sera ya uchangiaji elimu ya juu hasa suala la mikopo wakitaka kulipwa asilimia 100. 

Waziri huyo wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi alisema matatizo yote ya kiutendaji katika utekelezaji wa sera ya elimu yatatafutiwa ufumbuzi. “Itaundwa kamati itakayowashirikisha wadau wote mkiwamo wanafunzi,” alisema Profesa Maghembe, ingawa hakufafanua hatua zitakazochukuliwa endapo wanafunzi watakataa kutii agizo hilo la kurejea madarasani leo. 

Akiahirisha Bunge mjini Dodoma Ijumaa iliyopita, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema hivi sasa serikali inabeba gharama za kuchangia elimu ya juu, na haitawezekana kutoa mikopo kwa asilimia 100. “Kwa hali ya kawaida, hii mikopo ilitakiwa ilipiwe riba kwa wanafunzi, lakini kwa sasa serikali inabeba mzigo huo. 

Hatuna uchaguzi mwingine, bali kuendelea kuchangia gharama za elimu ili wanafunzi wengi zaidi wapate elimu ya juu,” alisema Pinda bungeni na kuongeza: “Napenda nirudie kusema kwamba serikali wakati wote itakuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanafunzi wanapata kile wanachostahili kujiendeleza kielimu. 

Naomba nitamke kuwa wanafunzi wale wanaotaka wanafunzi wote kupewa mikopo asilimia 100 haiwezekani.” Awali, jana wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani wameendelea kusisitiza kuendelea na mgomo leo baada ya Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutotokea chuoni hapo. 

Akihutubia wanafunzi waliokusanyika kwa shauku katika Ukumbi wa Nkrumah kusubiri tamko la serikali, Rais wa Serikali ya Wanafunzi (DARUSO), Anthony Machibya alidai amepata taarifa kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu pamoja na wasaidizi wake waliitwa Ikulu na Rais kwenda kujadili matatizo yao. 

“Profesa Mukandala ameondoka kimya kimya na wasaidizi wake wameenda Ikulu kujadili mgomo wetu, nimepigiwa simu na Karani wake, kwa hiyo tusikate tamaa tuendelee na msimamo wetu mpaka tuone hatima yetu,” alisema Machibya na kuongeza kuwa mgomo utaendelea kama kawaida hawatarudi nyuma. Aidha, magari matatu yakiwa na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), yalikuwa yakirandaranda katika maeneo ya chuo hicho tangu juzi na jana kuhakikisha usalama wa mali na watu unakuwapo.

CHANZO: Habari Leo

Related Posts:

  • SERIKALI YAAMURU WANAFUNZI MLIMANI WAINGIE MADARASANISerikali imewataka wanafunzi wote wa vyuo vya elimu ya juu nchini kuingia madarasani mara moja ifikapo saa moja asubuhi leo. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya … Read More
  • CHUO KIKUU MKWAWA NACHO CHAFUNGWANa Francis Godwin, Iringa SIKU moja baada ya askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mkoa wa Iringa kulazimika kutumia mabomu ya machozi kutuliza vurugu za wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE), uongozi… Read More
  • UBABE HAUWEZI KUTATUA MATATIZO YA MLIMANI (UDSM) Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wakifanya patrol hapo Mlimani (UDSM).Picha kwa hisani ya MICHUZI JR.Nilimaliza ngwe yangu hapo Mlimani (UDSM) takriban miaka kumi iliyopita.Kuna yaliyobadilika kwa kipindi cha miaka mitat… Read More
  • CHUO KIKUU CHA USHIRIKA NA BIASHARA CHATIMUA WANAFUNZIChuo Kikuu cha Ushirika na Biashara mkoani Kilimanjaro (MUCCoBS) kimewatimua wanafunzi 595 wa mwaka wa kwanza kutokana na kuanzisha mgomo chuoni hapo. Aidha wanafunzi hao pamoja na mgomo huo,wametuhumiwa pia kuhatarisha maish… Read More
  • WIMBI LA MIGOMO: "DAR TECH" NAYO YAFUNGWAUONGOZI wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) umekifunga chuo hicho kwa muda usiojulikana kutokana na mgomo wa wanafunzi.Uongozi wa chuo hicho umefikia uamuzi huo, baada ya wanafunzi katika chuo hicho kufanya mgomo kui… Read More

0 comments:

Post a Comment

Categories

Unordered List

Sample Text

Blog Archive

Labels

Follow Us on FaceBook

Popular Posts

Recent Posts

Recent Comments

Recent Premium Themes

Your Links

Flickr

Powered by Blogger.

Blog Archive

Followers

Download

Your Links

Blogger Tricks

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget